Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Gereza la Wilaya ya Mlele?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Wilaya ya Mlele inakaa Mahabusu kidogo sana, wanakaa watu takribani kumi, lakini kutokana na uhaba wanakaa watu kuanzia 30 mpaka 40 na wale ni binadamu na sisi binadamu tuna maradhi mengi wanaambukizana, wanakula mle ndani. Kwa nini Serikali wale watu wenye makosa madogo madogo wanaotakiwa kupewa dhamana, wasipewe dhamana ili waende kufanya shughuli zao zingine ili Mahabusu isikose watu kwa sababu mhalifu anajulikana na mhalifu ni Mtanzania anajulikana katika maeneo anayoishi. Je, ni kwa nini wasiwe wanapenda kutoa dhamana ili Mahabusu hizi zisiwe na watu ili msongamano uweze kupotea?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Wilaya ya Mlele katika kile Kituo cha Polisi hakuna magari, hakuna magari sasa unakuta Mahabusu wale wanakaa wiki nzima wakibanana mle ndani; je, ni lini Serikali itatununulia magari kwa ajili ya uboreshaji zaidi kwa sababu wanatolewa Mlele wanapelekwa Mpanda? Ahsante.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anna Richard Lupembe Mbunge wa Viti Maalum ambaye ni Mtumishi wa Mungu. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Anna Lupembe ambaye ni Mtumishi wa Mungu kwa namna ambavyo amekuwa akiwahamasisha Watanzania na waumini katika kulinda amani na kufanya doria za kiroho. Kwa hiyo nimpongeze sana kushiriki kwenye ujenzi na ulinzi wa amani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba pale Mlele kuna tatizo la Gereza na kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi kwamba Serikali iko kwenye mchakato wa kuhakikisha hizi Wilaya mpya tunajenga Magereza na Magereza mengine kwenye mikoa mipya. Tatizo ni kwamba ni kitu ambacho hakiwezekani kupangisha Gereza kwamba unaweza ukaenda kwenye nyumba ya mtu ukasema tumekuja tupangishe kwa ajili ya Gereza. Kwa hiyo kwa vyovyote vile lazima sisi kama Serikali tuendelee na mipango yetu ya kuhakikisha kwamba tunajenga Gereza. Ndiyo maana tumeanza kupunguza msongamano kwa kutumia Sheria mbalimbali ikiwa ni pamoja na mawazo yake aliyoyasema ya dhamana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye swali la gari, Wilaya zote tumezipa gari kwa ajili ya kuhakikisha kwamba gari zile zinasaidia kubeba Mahabusu. Kwa kesi ya Mlele Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi nichukue fursa hii kumpongeza ameshaanza juhudi kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya kuhamasisha wananchi na tayari ameshatoa mifuko 200 kwa ajili ya kuanza kujenga Gereza la Mlele na tayari tumeshampatia ramani. Kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya tutakapokwenda Mlele tutashirikiana pamoja na wananchi. Ahsante.