Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGAMBALE aliuliza:- Hifadhi ya Akiba ya Selous imekuwa ikihamisha alama za mipaka na kuchukua eneo la ardhi ya vijiji katika Jimbo la Kilwa Kaskazini bila ya kushirikisha Serikali ya Vijiji:- Je, Serikali iko tayari kusimamia Mamlaka ya Hifadhi hiyo kurudisha alama za mipaka katika maeneo ya awali ili kuepusha mgogoro unaoweza kutokea?

Supplementary Question 1

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Vipo vijiji vingine. Ukiacha Mtepera na Zinga, kuna Vijiji vya Miguruo na Ngarambi, navyo vinapakana na Pori la Akiba la Selous. Ni lini zoezi hili litafanyika katika vijiji hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, uhamishaji umefanyika, wananchi wana uelewa wa mipaka yao kwa kutumia alama zile za asili kama milima na mabonde. Kwa mfano, katika Kijiji cha Zinga pale pana mlima mkubwa unaitwa Nandanga, sasa Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufuatana nami ili kwenda kurekebisha mipaka ile kwa kuzingatia alama zile za asili kama milima na mabonde?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Vijiji vya Miguruo na Ngarambi, zoezi hili tutalifanya wakati tukipitia upya. Zoezi la kwanza lilikuwa ni kuweka alama kulingana na GN inavyosoma, lakini kuna maeneo mengi ambayo tuligundua yana migogoro. Kinachofuata sasa ni kupitia upya kuangalia ni maeneo gani ambayo migogoro ina faida kwetu au kwa wanakijiji na tutaangalia namna ambavyo tunaweza tukaisuluhisha. Kwa hiyo, tutakapoanza zoezi hili ambalo tunakwenda kulifanya, tutapita katika vijiji hivi viwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili; ni kweli kwamba alama nyingi ambazo zimetumika kama mipaka ya vijiji zilikuwa ni alama za asili; miti mikubwa, labda mto fulani, alama ambazo zimekuwa zikitoweka. Kwa hiyo, tumepata taabu katika kuelewa mipaka ya vijiji na pia mipaka ya mapori haya ya akiba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia Mheshimiwa Ngombale kwamba nitakuwa tayari kuambatana naye ili kwenda kuona hizi sehemu zenye mgogoro.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGAMBALE aliuliza:- Hifadhi ya Akiba ya Selous imekuwa ikihamisha alama za mipaka na kuchukua eneo la ardhi ya vijiji katika Jimbo la Kilwa Kaskazini bila ya kushirikisha Serikali ya Vijiji:- Je, Serikali iko tayari kusimamia Mamlaka ya Hifadhi hiyo kurudisha alama za mipaka katika maeneo ya awali ili kuepusha mgogoro unaoweza kutokea?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, kwa kuwa msingi wa swali ni kuhamishwa kwa mipaka ambayo imesababisha mpaka na wanyama wamechanganyikiwa, matokeo yake wanyama sasa wanavamia makazi ya wananchi na hasa wanyama waharibifu kama tembo na viboko: Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba maeneo kama ya Vijereshi, Longalombogo na maeneo mengine ambayo yanaathiriwa na tembo kuongezeka kuja katika makazi ya wananchi yatadhibitiwa?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, kimsingi sisi tunapokwenda kuweka mipaka tunafuata GN. Kwa sababu wananchi katika maeneo mengi walikuwa wanatambua mipaka yao kwa alama za asili, ndiyo wamekuwa wakifikiri kwamba tunaingia kwenye maeneo ya vijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetambua maeneo mengi yenye migogoro na Wizara yetu sasa baada ya kumaliza zoezi la kuweka vigingi, inapitia upya kuangalia ni kwa namna gani migogoro hii itaisha? Kwa hiyo, tutafika Kijereshi na Longalombogo ili kwenda kuangalia ni kwa kiwango gani tunaweza tukatengeneza mipaka ili kuhakikisha kwamba wanyama hawa hawaleti tena madhara kwa wananchi.