Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Kilwa ni moja kati ya miji mikongwe katika Afrika Mashariki tangu 900 – 1700 AD ikiwemo Lamu, Mombasa, Sofaa na Zanzibar. Miji hii ilipewa heshima ya jina la urithi wa dunia (World Heritage Sights) na husaidiwa na mataifa mbalimbali kama Marekani, Japan, Ujerumani, Uingereza na Taasisi ya UNICEF; Je, Serikali ya Tanzania inafaidika na nini kutokan kwenye mataifa hayo yanayosaidia nchi zenye Miji ya Urithi wa Dunia?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu ambayo ameyatoa lakini sasa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru wafadhili ambao walijitokeza katika kuja kuendeleza Mji wa Kilwa kwa shughuli mbalimbali ambazo zimetolewa. Hata hivyo urithi wa sasa upo mbioni kutoweka kwa sababu yale yaliyofanyika kama Wizara imeshindwa kuyasimamia katika kuendeleza utalii Kilwa. Kuna shida ya miundombinu ya kutoka Kilwa Mjini kwenda Kilwa Kisiwani,kwa maana ya usafiri wa boti; kumekuwa na boti ile ya kizamani ambayo haina usalama zaidi. Ningependa Serikali sasa kuweka miundombinu sawa ili kuufanya Mji wa Kilwa uweze kuendelea katika upande huo wa utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Kilwa bado kuna maeneo ya Kilwa Kivinje kuna magofu pale ambayo waliishi wakoloni lakini bado hayajaendelezwa kwa ajili ya utalii katika Mji wa Kilwa. Sasa ningeomba kuiuliza Serikali wanatumia njia gani kutangaza kwanza utalii Kilwa lakini ni kwa namna gani wizara hii sasa itakuja Kilwa kuona magofu ambayo wameshindwa kuyaendeleza kwa muda mrefu ili kufanya utalii wa Kilwa kuendelea. Ahsante sana.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza kwa nafasi hii nimpongeze sana Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah kwa juhudi kubwa ambayo amekuwa akiifanya kuulizia namna gani wizara inaendeleza utalii katika Mikoa ya Lindi na Mtwara kwa ujumla na amekuwa akitusumbua sana ofisini ili kuweza kufahamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba eneo hili miundombinu imekuwa ni mibaya kutokana na eneo hili kushindwa kujiendesha kutokana na mapato madogo ambayo yamekuwa yakipatikana kutokana na watalii wachache wanaokwenda maeneo hayo. Kwa hiyo, wizara katika kulitafutia ufumbuzi suala hili, imeyagawa maeneo yote ya malikale ambayo yametambuliwa ambayo ni maeneo 18 kwa taasisi zake nne. Eneo hili la Kilwa tumewapa TAWA; TAWA watachukua eneo hili wataliingiza katika packageyao ya utalii na kwa sababu hiyo watalazimika kulikarabati na kutengeneza miundombinu ili liweze kutumika vizuri na watu waweze kupata huduma zote ambazo Mheshimiwa Mbunge amesema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni kweli kwamba pamekuwa na tatizo la watalii wachache katika maeneo haya na sababu kubwa ni kwamba maeneo haya yamekuwa hayatangazwi. Sasa ili kukabiliana na suala hili, tumeyaingiza mambo haya yote kwenye taasisi na TAWA watakapokuwa wamechukua rasmi watayaingiza katika package zao za utalii ambazo zitakuwa pia zinajumuisha mbuga za wanyama na kwa hali hiyo suala hili la kuongeza mapato na kuongeza usimamizi wa vituo hivi utakuwa umelipa. Naomba nikushukuru.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Kilwa ni moja kati ya miji mikongwe katika Afrika Mashariki tangu 900 – 1700 AD ikiwemo Lamu, Mombasa, Sofaa na Zanzibar. Miji hii ilipewa heshima ya jina la urithi wa dunia (World Heritage Sights) na husaidiwa na mataifa mbalimbali kama Marekani, Japan, Ujerumani, Uingereza na Taasisi ya UNICEF; Je, Serikali ya Tanzania inafaidika na nini kutokan kwenye mataifa hayo yanayosaidia nchi zenye Miji ya Urithi wa Dunia?

Supplementary Question 2

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Katika majibu yake Mheshimiwa Waziri amezungumzia faida tunazozipata kwa kutunza haya maeneo ya urithi wa dunia. Selous ni moja ya world heritage; nilitaka kumuuliza Waziri kwamba serikali imeamua kujenga bwawa la umeme katika eneo hilo na nina amini Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na kuangalia hasara na faida. Anaweza akaliambia Bunge hili ni kwa kiasi gani tutaathirika na UNESCO baada ya sisi kuamua kujenga bwawa hilo na kwamba tunapunguza ile dhana nzima ya urithi wa dunia katika Selous.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali ina mradi wa umeme katika Mbuga ya Selous na kwamba mradi mzima wa umeme katika Mbuga ya Selous unachukua 1.8 ya eneo zima ambalo ni la Selous, na kwa hali hiyo utafiti ulifanyika kwanza hauna madhara yoyote ya uwepo wa Selous na pili hakuna pingamizi lolote ambalo Serikali mpaka leo imepata kutoka UNESCO. Kinachofanyika tu ni kuwaelimisha na kuwafanya waelewe zaidi kwamba uwepo wa bwawa hilo na mradi huo utaiongezea nguvu Serikali namna ya kuifanya Selous iwe mbuga bora zaidi.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Kilwa ni moja kati ya miji mikongwe katika Afrika Mashariki tangu 900 – 1700 AD ikiwemo Lamu, Mombasa, Sofaa na Zanzibar. Miji hii ilipewa heshima ya jina la urithi wa dunia (World Heritage Sights) na husaidiwa na mataifa mbalimbali kama Marekani, Japan, Ujerumani, Uingereza na Taasisi ya UNICEF; Je, Serikali ya Tanzania inafaidika na nini kutokan kwenye mataifa hayo yanayosaidia nchi zenye Miji ya Urithi wa Dunia?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Kondoa kuna michoro ya mapangoni Kolo – Kondoa Irangi,na michoro hii ni urithi wa dunia kama alivyosema yeye mwenyewe Naibu Waziri, na mpaka sasa wananchi wa Kondoa na hata watanzania hatujafaidika vizuri na michoro ile kwa sababu haijatangazwa ipasavyo.

Je, Serikali ina mikakati gani ya kutangaza michoro ya mapangoni pale Kolo-Kondoa Irangi ili wananchi wa Kondoa wafaidike na Watanzania wote kwa ujumla?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye swali la msingi kuhusu Kilwa, maeneo mengi sana haya ya malikale yalikuwa hayatangazwi na sasa wizara yetu imechukua hatua ya kuyagawa kwenye taasisi zake 4 ambazo ni TANAPA, TFS, Ngorongoro pamoja TAWA. Eneo hili la Kolo-Kondoa tumewapa watu waTFS ambao watafanya kazi zote za uendelezaji ikiwa ni pamoja kuandaa mazingira lakini na kutangaza ili kufanya eneo hilo liweze kufikika na kuvutia watalii.