Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN W. HECHE aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Tarime imeelemewa na Wagonjwa kwa sababu inapokea Wagonjwa wengi kutoka Wilaya ya Tarime na Rorya, pamoja na uchache wa Vituo vya Afya, Zahanati na Vifaa katika maeneo mengi ya Wilaya hizo. Je, ni kwa nini Serikali isipandishe hadhi Hospitali hiyo na kuwa Hospitali ya Mkoa?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushuru japo swali hili lilikosewa na kwa sababu hakukuwa na muda wa kufanya marekebisho na bahati nzuri Mheshimiwa Kandege anajua mazingira ya pale vizuri. swali langu Mheshimiwa lilihusu Zahanati ya Nyamwaga ambayo Halmashauri ya Wilaya imejenga majengo kumi wodi theatre, mochwari na tukaiomba iwe-upgraded kuwa Hospitali ya kwanza sasa ya halmashauri kwa sababu ina mazingira yote yanayoruhusu. Wewe tulikwenda pale na Waziri Mkuu unapajua, tumepeleka vifaa vya milioni mia tatu, swali langu linauliza ni lini, Zahanati ya Nyamwaga ambayo inazidi hata Hospitali ya Wilaya itafanywa kuwa Hospitali ihudumie wananchi kama hospitali na ipolekewe Wataalamu kwa sababu vifaa vipo? Ndio swali hilo na wewe unapafahamu vizuri pale.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Answer

MWENYEKITI: Lakini silo uliloliuliza, wewe umeuliza swali lingine, na Serikali imekujibu swali lako, sasa wewe umekuja na swali jipya, sasa nakubaliana na wewe, maswali ya Afya ni muhimu jimboni mwako na nakushukuru umelitolea, Mheshimiwa Waziri baadaye kaa na Mheshimiwa Mbunge mueleze majibu namna gani mnaweza ku-coucas na kujibu, hongera kwa swali zuri.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN W. HECHE aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Tarime imeelemewa na Wagonjwa kwa sababu inapokea Wagonjwa wengi kutoka Wilaya ya Tarime na Rorya, pamoja na uchache wa Vituo vya Afya, Zahanati na Vifaa katika maeneo mengi ya Wilaya hizo. Je, ni kwa nini Serikali isipandishe hadhi Hospitali hiyo na kuwa Hospitali ya Mkoa?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza, kwanza naipongeza Serikali kwa kutupatia pesa katika kituo cha Afya cha Sakala milioni mia nne na Usunani milioni mia nne katika Wilaya ya Ngorongoro Mkoa wa Arusha. Nilitaka kufahamu katika kwa kuwa vituo hivi vinakamilika siku si nyingi je Serikali imejipangaje, kuhakikisha inatuletea vifaa tiba na raslimali watu katika vituo hivi viwili vya Afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, niruhusu kwa dhati kabisa nimpongeze Mheshimiwa Catherine jinsi ambavyo amekuwa akiwapigania wananchi wa Mkoa wa Arusha hususani kuhusiana na suala zima la Afya, baada ya pongezi hizo naomba nimjibu Mbunge na kwa Wabunge wote ambao wana maswali kama hayo kuhusiana na lini vifaa na wataalam watapelekwa ili hayo majengo ambayo yamekamilika yaanze kufanya kazi iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ambayo tunaikaribia 2019/2020 sisi Ofisi ya Rais TAMISEMI, fedha nyingi tumetenga ili tuweze kuhakikisha kwamba tunapata vifaa vyote ili Vituo vya Afya vianze kufanya kazi iliyokusudiwa. Kwa sababu utakubaliana na mimi kwamba ukiwa na majengo mazuri bila kuwa na vitendea kazi itabaki kuwa White elephant na sisi Ofisi ya Rais TAMISEMI hatutaki kuwa sehemu ya mzigo huo. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge mchakato uko katika hali nzuri ili tuhakikishe kwamba Vifaa vinapatikana na Watumishi wa kutosha wanapatikana ili majengo yakishakamilika huduma ianze kutolewa.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. JOHN W. HECHE aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Tarime imeelemewa na Wagonjwa kwa sababu inapokea Wagonjwa wengi kutoka Wilaya ya Tarime na Rorya, pamoja na uchache wa Vituo vya Afya, Zahanati na Vifaa katika maeneo mengi ya Wilaya hizo. Je, ni kwa nini Serikali isipandishe hadhi Hospitali hiyo na kuwa Hospitali ya Mkoa?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwenye jimbo la Chalinze hakuna Hospitali ya Wilaya, mwenzi mmoja uliopita tulimsumbua Mheshimiwa Kangi Lugola tulikutana tumepata ajali, magari yetu yakaanza kusoma majeruhi, tukauliza shida ni nini? TAMISEMI kwa nini? Mnaweka hela Kibaha Mjini Kibaha Vijijini na kuna Tumbi? Kwa nini hamuwezi kupeleka hela katika Jimbo la Chalinze kupata Hospitali ya Wilaya kwa sababu kuna umbali mrefu watu wakipata ajali?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, najua iko kiu kubwa sana Waheshimiwa Wabunge maeneo mengi ambayo wangependa Hospitali za Wilaya na tunaita Hospitali za Halmashauri ziweze kujengwa. Sasa katika hii ambayo umesemea kuhusiana na Chalinze kuwa na Hospitali ya Wilaya, sina uhakika katika orodha ya Hospitali za Halmashauri ambazo zimetengewa bilioni 1.9 kama Chalinze ipo au haipo. Kama inakidhi vigezo katika bajeti tunayoenda nayo kuna Hospitali tisa nazo tutaziingiza nje ya zile 67 sasa, kama na Chalinze ni mojawapo hilo sioni kama…

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN W. HECHE aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Tarime imeelemewa na Wagonjwa kwa sababu inapokea Wagonjwa wengi kutoka Wilaya ya Tarime na Rorya, pamoja na uchache wa Vituo vya Afya, Zahanati na Vifaa katika maeneo mengi ya Wilaya hizo. Je, ni kwa nini Serikali isipandishe hadhi Hospitali hiyo na kuwa Hospitali ya Mkoa?

Supplementary Question 4

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Mkuranga mpaka leo kwa muda mrefu haina x-ray.Ni lini sasa Serikali itahakikisha hospitali ile inakuwa na x-ray kusudi kuwasaidia wananchi wa pale Mkuranga?Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ruth Mollel kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika majibu yangu ya nyongeza katika maswali ya nyongeza kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha maeneo yote ambayo majengo yapo, vifaa vinakuwepo na wataalam wa kutosha wanakuwepo. Kwa hiyo, ni vizuri tukajua hii Hospitali ya Mkuranga ambayo naamini ni miongoni mwa hospitali ambazo zinatakiwa ziwe na huduma hiyo, nini kilikosekana ili katika vifaa vitakavyopelekwa na yenyewe ipate hiyo X-ray.