Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Hospitali ya Kibena ni kongwe sana na imechakaa sana:- Je, ni lini Serikali itaifanyia ukarabati?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. imeuliza kuhusu Hospitali ya Kibena; nimepewa majibu kidogo sana juu ya Hospitali ya Kibena lakini zaidi majibu yamejikita kwenye hospitali mpya ya mkoa inayojengwa. Hospitali ile ya Kibena ni hospitali chakavu, ina wodi moja tu ya akinababa. Wanaopata ajali na wanaougua maradhi mbalimbali wote wanalazwa katika wodi moja. Hospitali hii haina fence tangu wakati imerithiwa kutoka Kampuni ya TANWART. Naomba sasa commitment ya Serikali, ni lini Serikali itatusaidia kuboresha hospitali ya Kibena kwa maana ya wodi ya wagonjwa na fence?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali imetusaidia tumepewa fedha kujenga Kituo cha Afya Ihalula, lakini hata sisi katika halmashauri yetu kwa kushirikiana na wananchi katika Kata ya Makoa wamejenga kituo cha afya, Kata ya Kifanya wanaendelea na ujenzi wa kituo cha afya, ndiyo wanakamilisha. Naomba pia commitment ya Serikali, je, ni lini itatusaidia sasa vifaa kwa ajili ya vituo hivi vya afya ambapo viwili vimekaribia kukamilika na kimoja kinakaribia kukamilika?.
Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, katika jibu la msingi nimeeleza kwamba na bahati nzuri nimepata fursa ya kutembelea hospitali zote mbili, hii ambayo ni Hospitali ya Kibena pamoja na hospitali mpya ya rufaa ambayo tunaendelea kujenga. Sisi kama Wizara, msukumo wetu sasa hivi ni kuweka nguvu kwa kuhakikisha kwamba ile Hospitali mpya ya Rufaa ya Njombe inakamilika.
Mheshimiwa Spika, ni kweli tumekuwa na changamoto na mimi binafsi nimeona katika Hospitali ile ya Kibena na ndiyo maana sasa hivi maboresho makubwa ambayo tunayafanya ni kupanua ule wigo wa utoaji huduma. Kwa hiyo nataka nimhakikishie tu kwamba sisi kama Serikali tunataka tukamilishe ile hospitali kubwa na ya kisasa ili huduma za msingi kwa wananchi wa Njombe Mjini ziweze kupatikana pamoja na Mkoa mzima wa Njombe.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na vifaa kwa vituo vipya vya afya ambavyo tunaendelea kuviboresha, Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) inaendelea kununua vifaa hivyo na kadri inavyofika kutoka kwa Washitiri tutakuwa tunavisambaza, ikiwa ni pamoja na vituo hivi ambavyo viko Njombe Mjini.