Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:- Shule za Serikali na shule binafsi zina mitaala tofauti, je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwa na mfumo mmoja wa mitaala?

Supplementary Question 1

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Takwimu ya ufaulu zinaonesha kuwa wanafunzi wa Serikali wanapata idadi ndogo ya ufaulu kuliko private. Hiyo inasababisha kupata nafasi ndogo ya udahili katika vyuo na inasababisha kupata watalaam wachache kutokana na uchache wa nafasi zao ya udahili.
Je, Serikali haioni kwamba inaweza ikapoteza watalaam kutokana na uchache wa wanaodahiliwa kwa kuwa wanafunzi wengi wa private wanaachwa kwa dhana kwamba wana uwezo wa kulipia ada za vyuo kutokana na uwezo wao uliokithiri wa kusoma katika shule hizo za private? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, miaka ya nyuma shule zilikuwa za sekondari na msingi zikifundisha masomo ya ufundi mbalimbali; uhonaji, useremala na kadhalika, je, Serikali ina mpango gani ya kuhakikisha inarudisha tena masomo haya ya ushonaji, ufundi mbalimbali kwa vitendo ili kuweza kuwawezesha wanafunzi wanapomaliza masomo yao wajiajiri? (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI (K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Nuru swali lake la kwanza amezungumzia habari ya takwimu ya wanafunzi wanaomaliza kwenye private school na wale wanaomaliza kwenye shule za Serikali. Naomba nimhakikishie kwamba hili suala ni la kitakwimu na anachokisema sidhani kama ana uhakika kwamba wa private ni wengi kuliko wale wa shule za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ni swali la kitakwimu, basi tutalichukua ili tuweze kuleta takwimu sahihi kulingana na alichokizungumza. Kwa imani natambua ya kwamba hakuna ambapo shule za Serikali zimekuwa nyuma sana ukilinganisha na za private kitakwimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili linazungumzia habari ya wanaomaliza ni namna gani wataweza kuendelezwa akirejea kwamba zamani mitaala ilikuwepo ya kufundisha useremala na mambo mengine. Naomba nimhakikishie kwamba Shule zetu au vyuo vyetu vya VETA zinafanya kazi hiyo ya kuweza kufundisha wanafunzi wanaoishia form four au darasa la saba mambo ya ufundi, lakini vile vile tuna vyuo 55 ambavyo vilikuwa ni Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na sasa hivi kati yake karibu vyuo 20 vinakarabatiwa ili kuweza kufundisha ufundi stadi kwa wanafunzi wale ambao wanakuwa wameshindwa kuendelea na masomo ya sekondari aidha kwa A’ level au kwa form one.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:- Shule za Serikali na shule binafsi zina mitaala tofauti, je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwa na mfumo mmoja wa mitaala?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Hivi sasa nchi nzima hatuna vitabu vya elimu ya msingi kwa darasa la nne hasa mitalaa mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wanafunzi hawa wanatarajia kufanya Mitihani ya Taifa hivi punde mwisho wa mwaka huu, Serikali ina utaratibu gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama majibu ya Serikali hayatatosheleza kwa umma wa Watanzania na sisi Wabunge, basi tuahirishe mjadala ulioko mezani tukajadili jambo hili kwa manufaa mapana ya nchi yetu. Naomba majibu ya Serikali.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI (K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokizungumza Mheshimiwa Mbunge sidhani kama ni sahihi, kwa sababu ni karibu wiki mbili au tatu zimepita Wizara imesambaza vitabu vya darasa la kwanza mpaka darasa la nne kwa Halmashauri zote nchini. Sasa kwa hali hiyo, nina imani kwamba vitabu vipo katika mashule na hapana huo upungufu anaozungumza kwa sasa.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:- Shule za Serikali na shule binafsi zina mitaala tofauti, je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwa na mfumo mmoja wa mitaala?

Supplementary Question 3

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri kwamba mtalaa wa shule binafsi na Serikali ni mmoja, lakini kwa zaidi ya miaka kumi shule za binafsi zimekuwa zikiongoza katika ufaulu.
Je, Serikali pamoja na kwamba inasema ina wajibu wa kusimamia kiwango cha ubora elimu nchini, haioni sasa ni wakati muafaka kujifunza kwa watu binafsi ni kwa namna gani wanafundisha watoto wao wanafaulu katika shule zao; badala ya kwamba Serikali inayosimamia ubora lakini shule zake zimekuwa zikifanya vibaya? (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI (K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, siyo kweli kwamba shule za binafsi zinafanya vizuri zaidi ya kuliko shule za Serikali. Ninachotaka kumhakikishia ni kwamba…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia idadi ya wanafunzi wanaokwenda kwenye shule za private ni wachache kuliko wanaokwenda kwenye shule za Serikali. Kwa hiyo, kwa vyovyote unapofanya rating ya wanafunzi, lazima pia uzingatie na wingi wa wanafunzi. Kwa hiyo, asilimia kumi ya wanafunzi 20 huwezi kulinganisha na asilimia kumi ya wanafunzi 1,000 kwa maana ya kwamba idadi inakuwa tofauti. (Makofi)