Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama iliyoko Mkoani Singida hupata mvua chini ya wastani na maji yote ya mvua hutiririka na kupotea. i. Je, Serikali inachukua hatua zipi kutoa kipaumbele kwa Wilaya ya Mkalama kujengewa mabwawa makubwa hasa ikizingatiwa kuwa fedha za ndani (own sorce) za Halmashauri haziwezi kutosheleza ujenzi wa huduma hii? ii. Je, ni lini Serikali itafanya utafiti kuona kiwango cha maji kinachopotea wakati wa mvua na kutoa ushauri wenye tija?

Supplementary Question 1

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa sababu catch line ni kwamba Halmashauri haina uwezo wa kujenga mabwawa, Serikali ipo tayari kutoa pesa hata bwawa moja moja kujenga mabwawa Mkalama katika maeneo yaliyotajwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa sababu ni ukweli usiopingika kwamba Halmashauri hazina uwezo wa kufanya utafiti, Serikali iko tayari kunipa watafiti nikaondoka nao kwenda kufanya utafiti na mimi nitakuwa nao huko?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyowapigania wananchi wake. Kwa kutambua changamoto kubwa sana ya maji katika Jimbo la Mkalama, Mheshimiwa Waziri wangu aliona haja ya kumsaidia Mheshimiwa Mbunge, akaagiza Mamlaka kwa Wakala wa Uchimbaji Visima (DCCA) kumchimbia visima 20 katika Jimbo lake katika kutatua tatizo la maji. Namwomba Mheshimiwa Mbunge wakati Serikali ikiangalia namna ya kumchimbia mabwawa, asimamie visima hivi ili wananchi wake wapunguze adha ya maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kumpatia watalaam, sisi kama Wizara ya Maji hatutokuwa na kikwazo chochote kumpatia watalaam aende nao katika kuhakikisha wanafanya utafiti, wananchi wake waendele kupata maji. (Makofi)

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama iliyoko Mkoani Singida hupata mvua chini ya wastani na maji yote ya mvua hutiririka na kupotea. i. Je, Serikali inachukua hatua zipi kutoa kipaumbele kwa Wilaya ya Mkalama kujengewa mabwawa makubwa hasa ikizingatiwa kuwa fedha za ndani (own sorce) za Halmashauri haziwezi kutosheleza ujenzi wa huduma hii? ii. Je, ni lini Serikali itafanya utafiti kuona kiwango cha maji kinachopotea wakati wa mvua na kutoa ushauri wenye tija?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru. Ukiachilia mbali Mkoa wa Kagera uko karibu zaidi na Ziwa Victoria, lakini Mkoa wa Kagera una uhaba mkubwa wa maji. Ni lini sasa Wizara itaamua kubuni mradi mkubwa wa maji kama ule unaotoa maji Ziwa Victoria kwenda Tabora, ukizingatia Mkoa wa Kagera uko karibu zaidi na Ziwa Victoria? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua maji ni uhai nasi kama Wizara ya Maji jukumu letu ni kuhakikisha tunawapatia wananchi maji. Tumefanya jitihada mbalimbali wananchi ambao ni wakazi wanaoishi pembezoni na maziwa kuhakikisha wanapata maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mkurugenzi wa eneo husika aandae mradi ambao sisi kama Wizara tutaangalia namna ya ku-support kwa haraka wananchi wake waweze kupata maji kwa haraka safi, salama na yenye kuwatosheleza.

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama iliyoko Mkoani Singida hupata mvua chini ya wastani na maji yote ya mvua hutiririka na kupotea. i. Je, Serikali inachukua hatua zipi kutoa kipaumbele kwa Wilaya ya Mkalama kujengewa mabwawa makubwa hasa ikizingatiwa kuwa fedha za ndani (own sorce) za Halmashauri haziwezi kutosheleza ujenzi wa huduma hii? ii. Je, ni lini Serikali itafanya utafiti kuona kiwango cha maji kinachopotea wakati wa mvua na kutoa ushauri wenye tija?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. IMMACULATA S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Jimbo la Kondoa la Vijijini pia lina uhaba wa mkubwa wa mabwawa na yale yaliyopo yanahitaji ukarabati mkubwa hususan katika bwawa la Kisaki ambalo linahudumia mifugo na wanadamu.
Sasa Serikali ina mpango gani pia wa kuweka jicho la ziada katika Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa Vijijini? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yetu ya Maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imekuwa ikichimba mabwawa na hata visima virefu katika maeneo yenye ukame mkubwa sana. Labda nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwa kuendelea kushirikiana na wafadhili wetu, tutaangalia namna ya kuweza kuondoa tatizo hilo na kuwachimbia mabwawa. Ahsante sana. (Makofi)