Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:- Je, Serikali imechukua hatua gani kwa walioruhusu korosho zilizochanganywa na mawe kusafirishwa nje ya nchi bila kuchanguliwa?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa korosho ambazo zimegundulika kuwa zimechanganywa na mawe zilipitia Bandari ya Dar es Salaam na tatizo hilo halipo katika Bandari ya Mtwara: Kwa nini Serikali isitoe kauli kwamba kwa korosho za Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ni marufuku kupitishwa katika Bandari ya Dar es Salaam?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, huu uchunguzi unaonekana umechukua muda mrefu sana na swali langu niliuliza walioruhusu, ni rahisi sana kukamata walioruhusu korosho hizo ziende kwa sababu kulikuwa na uwezekano kabisa kuzigundua kabla hazijasafirishwa kwenda nje ya nchi. Kwa nini Serikali inasita kuwataja waliohusika ili iwe fundisho kwa wengine katika msimu ujao? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza uhalifu hauna destination lakini sisi Kama Serikali hilo tumelipokea, tutalifanyia tathmini na tuangalie jinsi gani Bandari ya Mtwara inaweza ikatumika pia badala ya ile ya Dar es Salaam ingawa pia hao watu wabeba mizigo hata meli unakuta wakati mwingine anataka apeleke mzigo mahali ambapo pia anaweza akarudi na mzigo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, Serikali sisi sio kwamba tunapata kigugumizi. Tume ya kitaalam ilimaliza kazi yake na tumeshawasilisha hili jambo kwenye vyombo vya dola, inafanyia kazi na mara tu ule uchunguzi wa kina na wa uhakika utakapofanyika wote waliohusika watatajwa na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:- Je, Serikali imechukua hatua gani kwa walioruhusu korosho zilizochanganywa na mawe kusafirishwa nje ya nchi bila kuchanguliwa?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Baada ya tasnia ya korosho mwaka 2017 kufanya vizuri sana msimu uliopita, mwaka huu kumekuwa na matatizo ya mgogoro katika Mkoa wa Lindi kati ya Chama cha Ushirika cha Runali na Bodi ya Korosho. Jambo hili limefanya mpaka sasa hivi sulphur iwe bado haijafika katika Mkoa wa Lindi jambo ambapo limefanya sasa hivi mfuko mmoja wa sulphur kufika shilingi 70,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali itoe tamko, ni lini mtatuletea sulphur ili kupunguza bei ya sulphur ambayo imepanda baada ya kuwa na mgogoro kati ya Runali na Bodi ya Korosho?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna tatizo la kuchelewa kwa sulphur, lakini kutokana na swali lake alilouliza, mpaka sasa hivi ni kwamba Chama kile cha Runali kimeshaagiza tani 128 za sulphur, zimeshafika na zimeshasambazwa. Vilevile kwa faida ya wengine hata TANECU wameshaagiza tani 1,100 na tayari zimeshasambazwa na zinauzwa kwa shilingi 32,000. Nashukuru.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:- Je, Serikali imechukua hatua gani kwa walioruhusu korosho zilizochanganywa na mawe kusafirishwa nje ya nchi bila kuchanguliwa?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba mkulima mdogo wa korosho hawezi kufanya hujuma hizi na hujuma hizi zinafanywa na makampuni makubwa na msimu wa korosho unatarajia kuanza mwezi wa tisa.
Kwa nini Serikali inakuwa na kigugumizi cha kuwataja makampuni hayo ili msimu ujao wasiingie katika soko la korosho? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati najibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dada Hawa Ghasia, nimesema kwamba Serikali hatuoni na hatujapata kigugumizi chochote, ni kwamba tayari tume ya wataalam tumeshawasilisha ile taarifa ya uchunguzi kwenye vyombo vya dola, vinalifanyia kazi na mara tu ule uchunguzi wa uhakiki utakapofanyika na wa kina basi wote watatajwa na hatua kali za kisheria dhidi yao zitachukuliwa. Ahsante.