Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa Mawakala wa Pembejeo za Kilimo fedha zao ambazo walikopesha Serikali tangu mwaka 2014/2015?

Supplementary Question 1

MHE. JACQULINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikitishwa sana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jambo kubwa hili la Mawakala wa Pembejeo. Pamoja na majibu hayo, naomba niulize swali moja dogo la nyongeza lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
• Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokuwalipa Mawakala kwa wakati kwa kisingizio cha uhakiki kwa kipindi cha miaka minne ambapo Mawakala hao wamekuwa wakiishi kwa shida, wamekuwa wakifilisiwa mali zao na wengine wamekuwa wakipoteza maisha, naomba sasa commitment ya Serikali, ni lini Serikali itawalipa mawakala hao?
• Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inachelewesha malipo ya mawakala kwa zaidi ya miaka mitatu na thamani ya fedha kwa huduma waliyotoa haitalingana na thamani hiyo endapo wangelipwa kwa wakati. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwalipa mawakala hawa fedha zao ikiwa ni pamoja na riba ya asilimia tano?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaelewa concern ya Mheshimiwa Mbunge, ninaamini pia na Wabunge wengi na hata katika bajeti yetu ya Wizara ya Kilimo alitoa na machozi, nampa pole katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi kabisa ni kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ina nia njema na intention yake siyo kwamba haitaki kuwalipa mawakala hawa wa pembejeo, lakini kwenye jibu langu la msingi kama nilivyosema ni kwamba uhakiki unaendelea na uhakiki huu ni wa kina; na mara utakapofanyika sisi kama Serikali tutatoa taarifa na vilevile kama Wizara ya Kilimo wale wahusika wote ambao walikuwa chini yetu watumishi wa Serikali, tumeshawafukuza kazi.