Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Kisiwa cha Mafia kinapata umeme kutoka kwenye jenereta kubwa ya TANESCO ambayo nayo inatumia mafuta mengi yenye gharama kubwa. Je, ni lini Serikali itavusha umeme chini ya bahari (submarine cables) kutoka Nyamisati kwenda Kilindoni takribani kilometa 50?

Supplementary Question 1

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Mheshimiwa Naibu Waziri anasema mshauri elekezi ataanza kazi mwezi Julai na itachukua kama miezi saba. Sasa nataka atuhakikishie watu wa Mafia, baada ya miezi saba ya mshauri kumaliza kazi, je, ujenzi rasmi wa hizi hybrid utaanza lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa sasa hivi kuna tatizo kubwa sana Mafia la kukatikakatika umeme na vyanzo ni vya mafuta, hivyo vimekuwa havitoshelezi na kwa kuwa Mikoa ya Lindi na Mtwara imeshaingizwa kwenye Gridi ya Taifa na kuna majenereta pale kama manane hivi ya two megawatts, je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni sasa kwa kipindi hiki cha mpito wakati tukisubiri hizo jitihada nyingine kuwa tayari, tupatiwe angalau majenereta mawili yale ya Lindi na Mtwara?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Mheshimiwa Mbaraka Dau, swali lake la kwanza ameuliza baada ya upembuzi yakinifu kuanza na kukamilika, nimthibitishie kwamba ni kweli mradi huo utaanza ndani ya hiyo miezi saba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumweleza Mheshimiwa Dau kwamba kwa mujibu wa swali langu la msingi tumesema kabisa kwamba Benki ya Maendeleo ya Ufaransa imeonesha nia ya kufadhili mradi huu na kinachosubiriwa ni upembuzi yakinifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa eneo tumelipata na kazi itaanza mwezi wa saba, naomba nimthibitishie kwamba kwa kudra za Mwenyezi Mungu kwa kipindi cha miezi saba hiyo na kwa kuwa tunayo benki tayari imeonesha nia, kazi hiyo itaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ameuliza kwamba sasa baada ya mafanikio makubwa ya kuunganisha Mikoa ya Mtwara na Lindi kwenye Gridi ya Taifa, amewasilisha ombi kwa niaba ya wananchi wake na naomba nimpongeze, ni lini kwamba tunaweza tukapeleka yale majenereta?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kama Serikali tumelipokea hilo jambo lake na linazungumzika, lakini kwa sasa tunajaribu kwa sababu uzinduzi wenyewe wa kuunganisha umeme wa gridi umefanyika tu juzi, tunajaribu kuangalia upatikaji wa umeme baada ya kuunganisha mikoa hii kwenye gridi, lakini hapo baadaye tutakapoona umeme umetulia unapatikana kwa ukamilifu, basi nalo linazungumzika na tutalipokea. Ahsante. (Makofi)

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Kisiwa cha Mafia kinapata umeme kutoka kwenye jenereta kubwa ya TANESCO ambayo nayo inatumia mafuta mengi yenye gharama kubwa. Je, ni lini Serikali itavusha umeme chini ya bahari (submarine cables) kutoka Nyamisati kwenda Kilindoni takribani kilometa 50?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu umeme kupelekwa Mafia, naomba kujua nini harakati na mkakati wa Serikali wa kupeleka umeme katika Visiwa vya Jibondo, Chole na Jiwani huko huko Mafia? Kwa sababu Jibondo, Chole na Jiwani vyote hivyo ni visiwa ndani ya Kisiwa kikuu cha Mafia. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa, kwa kuwa REA kupitia miradi ya kupeleka umeme vijijini upo mradi wa kupeleka umeme katika maeneo ya off-grid ikiwemo visiwa; visiwa alivyovitaja Jibondo, Jiwani na Chole vipo katika mkakati huo na kama miezi minne iliyopita REA ilifanya tathmini katika maeneo mbalimbali ya visiwa vikiwemo Visiwa vya Kibiti, Mkiongoroni, Mbuchi, Salale, Saninga, Koma na maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka nimthibitishie mradi huo upo na bahati nzuri wafadhili ambao ni Serikali ya Norway pamoja na Sweden wapo ku-support maeneo yote ya visiwa ikiwemo hata Visiwa vya Ukerewe na maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilithibitishie Bunge lako tukufu kwamba mradi huo upo. (Makofi)