Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Joram Gidarya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA J. GIDARYA aliuliza:- Mkoa wa Manyara ni moja kati ya maeneo yanayokubaliwa na changamoto ya migogoro ya ardhi katika wananchi wa Babati Vijijini hasa katika Vijiji vya Amayango, Gedamara na Hifadhi ya Tarangire kwa takribani miaka 11 sasa bila ufumbuzi wowote, migogoro hiyo imesababisha wananchi kukosa elimu, afya na uchumi kushuka ambapo majengo ya jamii yaliyopo ni madarasa manne, bweni moja, matundu 13 ya vyoo vya shule na jengo la zahanati na majengo haya yote yamejengwa kwa nguvu za wananchi. • Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza migogoro hiyo iliyodumu kwa muda mrefu na kurudisha maeneo ya wananchi yaliyochukuliwa na hifadhi? • Endapo itabainika mipaka kati ya vijiji na hifadhi iliyooneshwa kwenye ramani ni batili. Je, Serikali husika iko tayari kuwalipa fidia wananchi wote walioathirika na migogoro hiyo kwa muda wa miaka 11?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Spika, asante, nasikitika majibu ya Serikali kwa asilimia 90 ni uongo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, wananchi hawa walikaa kwenye hilo eneo miaka 20 iliyopita, fidia wanayosema ya kifuta jasho katika yale mabanda au tuseme zile nyumba waliwathaminishia TANAPA bila kuwashirikisha, kila mmoja fidia haikuzidi shilingi 300,000.
Mheshimiwa Spika, muda wote huo bila kuangalia riba wananchi walikaa mitaani na watoto wao waliathirika walikosa na masomo kwa sababu walifukuzwa watoto wakawa wanakaa kwenye nyumba za watu baki. Leo hii Serikali inasema imelipa, siamini katika hili. Mheshimiwa Waziri upo tayari kwenda Babati kwa ajili ya kuhakikisha kama mgogoro upo au haupo? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, TANAPA imelazimisha kuweka mipaka ya kudumu bila kuwashirikisha wahusika wenyewe wa mgogoro. Mkurugenzi anayezungumziwa kwamba amelipa, walienda kutoa amri yeye na Mkuu wa Wilaya mipaka ikawekwa, wananchi hawakushirikishwa, mgogoro huo haukuisha mpaka sasa. Lakini ni kwa nini sasa Serikali katika maeneo yenye migogoro ya hifadhi wamekuwa wakatili kupitiliza, wananchi hawa ni Watanzania au sio Watanzania?
Mheshimiwa Spika, tunaomba majibu ya Serikali ili tusiumane umane hapa kila siku tunarudia suala la Ayamango na Gedamar, ahsante. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia kuhusu haya maeneo na mgogoro huu, amekuwepo mstari wa mbele sana, hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema, mgogoro huu umekuwepo kwa muda mrefu, lakini kilichokuwepo mwanzoni, hata hifadhi yenyewe ilikuwa bado haijajua mipaka yake na ndiyo maana mwaka 2004 walipoenda kuhakiki mipaka ilibainika kwamba hata baadhi ya maeneo ya hifadhi yalikuwa yako nje kwa sababu hata hifadhi yenyewe ilikuwa haijui. Lakini waliofanya uhakiki ilikuwa ni Wizara ya Ardhi ambayo ndiyo yenye mamlaka ya kuhakiki mipaka, ndio waliofanya. Sisi hatuhakiki, Wizara ndiyo wanatuonesha mipaka kwa ramani hii kuwa mipaka ni hapa na hapa, kwa hiyo, naamini kabisa kwamba walifanya kazi yake vizuri.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kwenda kuongozana naye, naomba nimhakikishie niko tayari baada ya Kikao cha Bunge tuongozane twende tukaangalie hali halisi iliyopo ili tuone kama bado mgogoro upo tuweze kuutatua kwa pamoja na wananchi waweze kushirikishwa katika utatuzi wa huu mgogoro. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii. Napenda tu kulihakikishia Bunge lako kwamba migogoro ya mipaka hasa katika maeneo ya hifadhi tayari Wizara kwa kushirikiana na TANAPA, tunavyo vijiji vipatavyo 427 katika hifadhi nane ambavyo hatua za uhamasishaji kwa ngazi ya mkoa na wilaya zimeanza, baadaye zitashuka kwenye ngazi ya vijiji na kote huko kutapimwa ili kuweza kupanga pia matumizi bora ya ardhi katika maeneo hayo na tayari pesa, shilingi bilioni nne, zimeshatolewa katika Kitengo chetu kile cha Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi, kwa hiyo, tuna imani na Tarangire ipo, itakwenda kufanyiwa kazi ili kuondoa utata wa mipaka. (Makofi)

Name

Joshua Samwel Nassari

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ANNA J. GIDARYA aliuliza:- Mkoa wa Manyara ni moja kati ya maeneo yanayokubaliwa na changamoto ya migogoro ya ardhi katika wananchi wa Babati Vijijini hasa katika Vijiji vya Amayango, Gedamara na Hifadhi ya Tarangire kwa takribani miaka 11 sasa bila ufumbuzi wowote, migogoro hiyo imesababisha wananchi kukosa elimu, afya na uchumi kushuka ambapo majengo ya jamii yaliyopo ni madarasa manne, bweni moja, matundu 13 ya vyoo vya shule na jengo la zahanati na majengo haya yote yamejengwa kwa nguvu za wananchi. • Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza migogoro hiyo iliyodumu kwa muda mrefu na kurudisha maeneo ya wananchi yaliyochukuliwa na hifadhi? • Endapo itabainika mipaka kati ya vijiji na hifadhi iliyooneshwa kwenye ramani ni batili. Je, Serikali husika iko tayari kuwalipa fidia wananchi wote walioathirika na migogoro hiyo kwa muda wa miaka 11?

Supplementary Question 2

MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Spika, kwanza ni-declare interest, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge hili ya Ardhi, Maliasili na Utalii na unakumbuka ulikuja Meru wewe, siku mimi nimeoa wewe ulikuja Meru ukimwakilisha Mama Makinda, na kwenye harusi ulizungumza ukasema miongoni mwa vilio ambavyo Mbunge wenu Nassari amekuwa akipigia kelele kwenye Bunge ni suala la ardhi.
Mheshimiwa Spika, Kata ya Ngarenanyuki ambayo inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Arusha, hususan Kitongoji cha Momela, wamekuwa na mgogoro wa muda mrefu sana na Serikali na Wizara kwa sababu ya shamba namba 40 na shamba namba 41 yaliyoachwa na walowezi, walowezi ambao watu wa Meru hawa walichomewa nyumba miaka ya 1950, mwaka 1952 wakamtuma mtu UN, leo 2018 tumezungumza kwenye Bunge, aliyekuwa Naibu Waziri wa Wizara hii Mheshimiwa Engineer Ramo Makani akakubali kuondoka hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nikiwa masomoni Uingereza Mheshimiwa Mzee Mbatia huyu wakazungumza na wakakubaliana kwenda Meru kuniwakilisha kunisaidia kumaliza mgogoro. Amefika Wilayani Arumeru kasimamishwa na Mkuu wa Wilaya kutokwenda kwenye mgogoro, Mheshimiwa Mzee Mbatia akarudishwa kutoka kijijini kule ameshatoka Moshi. Huyo Mkuu wa Wilaya ndio aliyekwenda kuweka vigingi bila kushirikisha wananchi na imagine Wizara ya Ardhi hii imetoa hati mwaka huu mwezi wa pili, mwezi wa tatu maaskari wamekwenda kupiga risasi ng’ombe wa wananchi kwenye shamba namba 40 na shamba namba 41. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwenye Kamati mimi nimetaka kulia, mwanaume nikajizuia, sasa swali langu, Naibu Waziri wewe uko tayari baada ya kikao hiki kuongozana na mimi twende ili tukauangalie mgogoro huu na ili tuweze kujenga mahusiano mema kati ya hifadhi na watu wa Momela? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mgogoro huu umedumu kwa muda mrefu na viongozi waliotangulia walishafika katika yale maeneo na wakaona hali halisi na mimi niko tayari kuongozana naye ili twende tukaangalie nijionee mwenyewe ili tuweze kufanya uamuzi unaostahili.
Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuongeza tu ni kwamba, kama tulivyosema, Serikali iliunda Kamati ya Kitaifa ya kubaini aina yoyote ya migogoro nchini na Kamati hiyo imeshamaliza kazi yake na imeleta mapendekezo Serikalini ambayo Wizara zinazohusika zinayafanyia kazi na kufikia uamuzi, tukishafikia uamuzi nina imani kabisa tatizo hili la Meru litakuwa nalo ni mojawapo ambalo litaisha kabisa.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. ANNA J. GIDARYA aliuliza:- Mkoa wa Manyara ni moja kati ya maeneo yanayokubaliwa na changamoto ya migogoro ya ardhi katika wananchi wa Babati Vijijini hasa katika Vijiji vya Amayango, Gedamara na Hifadhi ya Tarangire kwa takribani miaka 11 sasa bila ufumbuzi wowote, migogoro hiyo imesababisha wananchi kukosa elimu, afya na uchumi kushuka ambapo majengo ya jamii yaliyopo ni madarasa manne, bweni moja, matundu 13 ya vyoo vya shule na jengo la zahanati na majengo haya yote yamejengwa kwa nguvu za wananchi. • Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza migogoro hiyo iliyodumu kwa muda mrefu na kurudisha maeneo ya wananchi yaliyochukuliwa na hifadhi? • Endapo itabainika mipaka kati ya vijiji na hifadhi iliyooneshwa kwenye ramani ni batili. Je, Serikali husika iko tayari kuwalipa fidia wananchi wote walioathirika na migogoro hiyo kwa muda wa miaka 11?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, mgogoro uliopo Manyara unafanana na mgogoro uliopo Ulanga kati ya Selous Game Reserve na wananchi wa Kata za Ketaketa, Ilonga na Mbuga, Mheshimiwa Waziri analifahamu vizuri. Sasa wananchi wameendelea kukamatwa na kupigwa, huku siyo tu kuwachokoza wananchi, ni kunichokoza hata na mimi mwenyewe.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba majibu ya Mheshimiwa Waziri, lini yuko tayari kwenda kwa ajili ya kumaliza huu mgogoro kati ya Selous Game Reserve na wananchi wa hizi kata?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, niko tayari kuongozana naye kwa sababu tulishakubaliana kwamba baada ya wiki hii Jumamosi inayofuata twende tukaangalie hali halisi katika eneo lile ambako kuna mgogoro. Kwa hiyo, tutakwenda, tutabainisha na tutakaa na wananchi ili tuone kwamba tatizo ni nini na tulipatie ufumbuzi.