Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Je, kwa nini Serikali haitaki kukarabati Uwanja wa Ndege Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Spika, asante. Nashukuru kwa majibu mafupi na precise ya Mheshimiwa Naibu Waziri, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa utaratibu wa manunuzi ni mchakato na majibu yake hayajaeleza kwamba exactly timeframe ni lini Serikali imempa huyu mkandarasi kukamilisha mchakato wake ili ujenzi na ukarabati uanze mara moja.
Sasa nilikuwa naomba kupata majibu kwamba ni lini hasa, ni baada ya miezi mingapi huyu mkandarasi atakuwa amemaliza?
Mheshimiwa Spika, kumekuwa na utaratibu huko miaka ya nyuma kwamba baadhi ya vitu vinahamishwa mikoa ya Kusini na baada ya uhuru tu mapema ilihamishwa reli lakini pia na taa za Uwanja wa Ndege wa Mtwara. Sasa nilikuwa naomba kujua kwamba ukarabati ambao unatarajiwa kufanyika katika uwanja huu utahusisha pamoja na uwekaji wa taa za kuongozea ndege ambazo zilizoondolewa miaka ya nyuma? Ahsante. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, kwanza niseme ujenzi umeshaanza kwa sababu ujenzi una hatua mbalimbali, kwenye hatua hii mpaka mkataba umesainiwa na tumepata fedha nyingi. Kwa taarifa tu Mheshimiwa Nachuma awali tulikuwa tunakadiria tufanye matengenezo kwa shilingi zipatazo bilioni 39 lakini kwa kuzingatia maboresho na kufanya uwanja uwe na uwezo wa kupokea hata ndege Airbus aina ya A340-200 kwa hiyo, tumezingatia, huwezi kupokea ndege hii bila kuwa na taa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kutakuwa na barabara na kutua na kurukia zenye urefu wa mita 3,000, kutakuwa na maegesho ya ndege, kutakuwa na barabara za kuingilia katika uwanja na jengo la abiria lakini kuweza kutua ndege kubwa kama nilivyosema lakini pia taa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Nachuma usiwe na wasiwasi kwamba ule uwanja nafikiri miezi 20 ijayo utaona huduma zimeongezeka na utaendelea ku-enjoy huduma za ndege.