Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza:- Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF) umemuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuamua kukiboresha Kiwanda cha Tangawizi cha Mamba Miamba kilichoko Wilaya ya Same katika Jimbo la Same Mashariki. Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu sasa kuboresha barabara zinazoelekea Mamba Miamba Kiwandani?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, swali langu kubwa hapa lilikuwa ni barabara zinazoelekea Mamba Miamba Kiwandani, basi naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali moja kubwa kidogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, barabara zinazoelekea Mamba Miamba Kiwandani zipo za aina mbili, ya kwanza ni barabara inayounganisha Kiwanda cha Tangawizi na masoko ya ndani na nje ya nchi na barabara hii inatokea Mkomazi Kisiwani kwenda Same na barabara ya pili ni barabara zinazounganisha walima tangawizi (wakulima) na kiwanda chao.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Rais wa Awamu ya Nne mwaka 2009 alikuja Mamba Miamba yeye mwenyewe akaona jitihada za wananchi, akatoa bilioni 2 za kujenga barabara za kuwaunganisha wakulima na kiwanda chao. Je, Mheshimiwa Waziri huoni kwamba ili uelewe tatizo kubwa la miundombinu ya kiwanda kile ni vyema wewe mwenyewe ukawaahidi wananchi wa Mamba Miamba utakwenda lini kule ili uweze kujibu haya maswali vizuri, ahsante sana. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, kwanza nipo tayari kwenda, lakini uniruhusu nimpongeze tu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu najua kupatikana kwa kiwanda hiki ni pamoja na juhudi zake, lakini niwashukuru na kuwapongeza Mkuu wa Wilaya kwa sababu Mkuu wa Wilaya pia amekuja akiwa na ombi la kutembelea maeneo haya. Natambua kwamba lazima tuboreshe barabara ambazo zinawahudumia wananchi kupeleka malighafi kwenye kiwanda hiki, lakini pia kutoa mazao yanayotokana na kiwanda hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pia barabara hii ambayo nimeizungumza ni muhimu sana kwa sababu inapokwenda kuunganisha Mkomazi pia inatoa huduma kwa ajili ya utalii. kwa hiyo, nipo tayari Mheshimiwa Mbunge nitakuja Same tutembelee maeneo hayo. (Makofi)

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza:- Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF) umemuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuamua kukiboresha Kiwanda cha Tangawizi cha Mamba Miamba kilichoko Wilaya ya Same katika Jimbo la Same Mashariki. Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu sasa kuboresha barabara zinazoelekea Mamba Miamba Kiwandani?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara ya Likuyufusi – Mkenda mpaka Msumbiji ambayo inaunganisha Jimbo la Mheshimiwa Jenista Mhagama na nchi ya Msumbiji ambayo katikati hapa kuna wawekezaji wengi sana wamefungua na viwanda lakini barabara hiyo bado ni ya vumbi.
Je, ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami ili kunufaisha Jimbo la Songea Mjini, Jimbo la Peramiho pamoja na wawekezaji waliopo ikiwa kuleta masoko nchini Msumbiji? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Ndumbaro kwa sababu ukikutana naye yaani ni barabara ya mchepuo, barabara ya Likuyufusi – Mkenda, kwa hiyo, nimpongeze pia Mheshimiwa Jenista kwa sababu mara nyingi sana amefuatilia barabara hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niseme tu tumetenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii ya Likuyufusi – Mkenda lakini pia tumetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja kule Mkenda, najua hii ndio changamoto ilikuwa kubwa sana ya eneo hili kwa maana hiyo kwamba tumetenga fedha. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nitaendelea tu kukupa mrejesho na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo Mheshimiwa Jenista usiwe na wasiwasi eneo hili tumelitengea fedha.
Mheshimiwa Spika, pia daraja hili la Mkenda ni muhimu sana pia kwa wananchi ambao wanakwenda Mbamba Bay kwa sababu ukitoka Mkenda kwenda kule Tingi hii ni muhimu sana wanaitegemea barabara hii ili waweze pia kutembea na kuvuka kuja upande huu wa Peramiho. Kwa hiyo, tumejipanga vizuri. (Makofi)