Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y MHE. RASHID A. AKBAR) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuipatia Hospitali ya Wilaya ya Newala watumishi pamoja na vifaa tiba?

Supplementary Question 1

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Vifaa tiba ni tatizo kubwa kwenye hospitali nyingi nchini na utajiri mkubwa tulionao kuliko wote ni afya za mwanadamu.
Mheshimiwa Spika, swali, Wizara hii ina upungufu wa zaidi ya sekta ya afya zaidi ya asilimia 50 ya watumishi. Serikali inaji-commit nini kuhusu kuhakikisha watumishi wa kutosha wa Hospitali ya Newala wanapatikana kwa wakati ili waweze kutoa huduma zinazostahiki?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, Hospitali ya Kilema iliyoko Vunjo au ya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ina tatizo la vifaa tiba na watumishi wake kwa wakati huu nesi mmoja anahudumia zaidi ya watu 30 wodini. Serikali inatoa kauli gani hapa ili hospitali hii nayo ipate watumishi wa kutosha pamoja na vifaa tiba kwa ajili ya afya za binadamu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kuhusiana na commitment ya Serikali ili kuhakikisha kwamba watumishi wa afya wanapelekwa wa kutosha Newala ni kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi. Maombi yao ni kupatiwa watumishi 60 na hii naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbatia kwa niaba ya Mheshimiwa Ajali Akbar kwamba ni commitment ya Serikali kuhakikisha pindi fursa za ajira zitakapokuwa zimetolewa hatutaisahau Newala.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Hospitali yake ya Kilema ambayo anasema wastani Nesi mmoja anahudumu wagonjwa 30 ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba tunaweka vifaa vya kutosha lakini pia na watumishi wa kutosha. Ndio maana wakati Mheshimiwa Waziri wa dhamana ya ajira alivyokuwa anahitimisha alisema ndani ya Bunge hili tunategemea kuajiri watumishi wa kutosha. Katika watumishi 59,000 watakaoajiriwa sehemu kubwa ni upande wa elimu na afya, naomba nimuhakikishie ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba tunapunguza mzigo mkubwa kwa wahudumu kwa maana ya manesi ili na wao wawe na fursa ya kuweza kuhudumia wagonjwa kwa uzuri zaidi.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie na Hospitali ya Kilema tutaikumbuka.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y MHE. RASHID A. AKBAR) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuipatia Hospitali ya Wilaya ya Newala watumishi pamoja na vifaa tiba?

Supplementary Question 2


MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Katika sekta iliyoathirika sana wakati wa zoezi la uhakiki wa vyeti, suala zima la vyeti fake ni sekta ya afya. Jimboni Mtama baadhi ya zahanati tumelazimika kuzifunga kabisa kwa sababu watu wameondolewa.
Mheshimiwa Spika, sasa kwa nini Serikali isichukue hatua za dharura kwenye haya maeneo ambayo zahanati zimefungwa badala ya kusubiri process hii ya kuajiri watumishi wapya wa afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Spika, katika maeneo ambayo nilifanikiwa kupita na kuona kazi nzuri ambayo imefanyika katika suala zima la ujenzi wa vituo vya afya ni pamoja na Jimbo lake la Mtama, kwanza naomba nimpongeze.
Mheshimiwa Spika, tukiwa hapa ndani bungeni Mheshimiwa Mkuchika alitoa taarifa kwamba kama yuko Mbunge yeyote, wa eneo lolote ambalo tumelazimika kufunga zahanati au kituo cha afya kwa sababu ya ukosefu wa watoa huduma aandike barua ampelekee ili tatizo hili lisiweze kutokea.
Mheshimiwa Spika, naomba kama Mheshimiwa Mbunge hakuwepo siku hiyo atumie fursa na bahati nzuri yeye yuko jirani sana na Mheshimiwa Mkuchika ili hicho anachokisema kisiweze kutokea.