Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kujibu swali langu vizuri. Swali la kwanza, kama Waziri alivyoeleza ni kwamba mfumo umebadilika lakini kama ilivyo kule Hanang bei bado haijashuka na madhumuni ya kuwa na mfumo huu wa sasa ni kushusha bei. Nataka kujua kwa nini bei haijashuka mpaka sasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, mfumo wa sasa unapaswa kuwafikia wakulima wote badala ya ule wa ruzuku kufikia watu wachache peke yake. Hata hivyo, nataka kujua kwamba huu ununuzi wa pamoja wa mbolea kama kweli umewanufaisha watu kama wanavyotarajia na kama Serikali inavyotaka na kama sivyo watuambie ni msimu upi mfumo huo wa sasa utanufaisha wakulima wote kuliko ilivyokuwa pale awali?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze sana kwa jinsi ambavyo amekuwa akishugghulikia suala zima la mbolea na mfumo wa pamoja na ukizingatia yeye alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati yetu ya Kilimo, Mifugo na Maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye maswali yake mawili ya nyongeza ni kwamba ni kweli bei haijashuka kwa sababu mfumo huu tumeuanza sasa hivi na matokeo yake mazuri tutayaona kuanzia msimu ujao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika lile swali lake la pili ni kwamba mbolea yetu ambayo tunasema ina bei elekezi ya Serikali tunapaswa tuwaambie wananchi wote wasubiri msimu unaotakiwa ili iuzwe kwa pamoja lakini vilevile hata wale wazabuni wetu tunataka wawe wanafanya order kwa wingi kwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba nitoe ushauri, hata wale wafanyabiashara kwenye yale maghala yao wajenge kwa wingi ili maghala yale kulekule katika halmashauri wawe wanazalisha ili huu msimu unapofika basi wananchi na wakulima wetu waweze kupata mbolea zile kwa wakati na kwa pamoja inavyotakiwa.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wakulima wa zao la chai, hasa wakulima wadogowadogo wamekuwa wakinunua pembejeo kwa bei ya juu sana. Ni lini Serikali itatoa mbolea ya ruzuku, kwa maana ya pembejeo ya ruzuku kwa wakulima hawa wadogo kama ilivyo kwenye mazao mengine ya korosho na pamba, ili waweze kupata faida kutokana na kilimo hiki cha chai? Ahsante.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niwaambie kwa faida ya Waheshimiwa Wabunge wote, msimu huu tumeamua kwamba hakutakuwa na bei yoyote ya ruzuku kwenye mbolea. Ndiyo maana hata kwenye sulphur ambayo ilikuwa inatolewa kwa ruzuku, safari hii tumeamua kwamba na yenyewe iwe inauzwa.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Mheshimiwa Naibu Waziri anafanya kazi nzuri, hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa butura ulikuwa unamsaidia sana mkulima wa kahawa Mkoa wa Kagera kupunguza ukali wa maisha wakati anasubiri kuvuna kahawa shambani. Je, Serikali imejipangaje kumsaidia huyu mkulima baada ya kuzuia uuzaji wa butura? Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, butura ni mfumo ambao wakulima wamekuwa wanauza mazao kabla hawajavuna na ni mfumo ambao umewanyonya kwa miaka mingi. Ndiyo, walikuwa wanapata fedha lakini fedha wanayopata hailingani na thamani ya mazao yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, ni mfumo ambao sasa hivi Serikali inahakikisha kwamba hautaendelea. Badala yake Vyama vya Ushirika vimeshawishiwa na tunavisaidia kuweka utaratibu ambao utakuwa unaweza kuwawezesha wakulima wenye shida ndogondogo badala ya kuuza mazao kwa bei za chini sana ambazo wananyonywa.

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 4

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Uti wa mgongo wa nchi hii uko kwenye kilimo. Tunategemea kilimo ili tuweze kupata maendeleo kwenye nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nauliza swali. Shinyanga na Kahama tunaongoza kwa kilimo cha mpunga na mahindi. Mpaka sasa ninapoongea ruzuku imepungua kwa zaidi ya 50%. Nini mpango wa Serikali kuongeza ruzuku ili tuweze ku-improve kwenye kilimo? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza amezungumzia kwenye zao la mpunga na mahindi na juu ya kuongeza ruzuku. Nilipokuwa najibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hongoli nimesema kabisa kwamba hatutakuwa na ruzuku kwa mwaka huu kwa sababu mazao yote yawe ya kimkakati, yawe yale ya nafaka, wote watakuwa wananunua isipokuwa kwa bei elekezi.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 5

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Chama cha Msingi cha Imalamakoye AMCOS kimesababishia hasara kubwa wakulima wa tumbaku katika Wilaya ya Urambo ya zaidi ya Dola 19,500 sawa na Shilingi za Kitanzania milioni 40 na zaidi na hivyo kusababisha kushindwa kununua pembejeo kwa ajili ya kilimo chao cha tumbaku. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wakulima hawa ili Chama hiki cha Imalamakoye kiweze kuwalipa pesa zao waweze kupata pembejeo? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue fursa hii pia na yeye kumpongeza kwa jinsi anavyofuatilia suala zima hili la tumbaku. Ni kweli kwamba hii AMCOS ya Imalamakoye ambayo ameisema imekuwa ina matatizo, kumekuwa na ubadhirifu katika na mpaka sasa hivi tunapozungumza ni kwamba Mwenyekiti wa Bodi ameshashtakiwa na kesi hii iko Polisi, uchunguzi unaendelea kufanyika. Mara itakapobainika basi hatua kali sana za kisheria zitachukuliwa.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Msimu uliopita mbolea na mbegu Mkoa wa Rukwa hazikufika kwa wakati na hazikuwa na impact yoyote. Je, msimu unaokuja atatuhakikishia kwamba mbolea na mbegu zitafika kwa wakati?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jibu langu la msingi la Mheshimiwa Dkt. Nagu, nilijibu kabisa kwamba Serikali imeshajipanga kuhakikisha kwenye msimu ujao mbolea inafika kwa wakati.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 7

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Singida unazalisha kwa wingi mazao ya biashara na chakula kama vitunguu, mahindi, alizeti na viazi vitamu. Tatizo kubwa lililopo kwa wakulima wetu ni bei kubwa ya pembejeo pamoja na zilizopo sokoni kukosa ubora. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha pembejeo zinapatikana kwa bei zilizokuwa nzuri lakini zina ubora wa kutosha? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza pembejeo zinanunuliwa lakini sisi kama Wizara ya Kilimo tuna Mfuko wetu ule wa Pembejeo ambao tunatoa mikopo yake kwa asilimia saba au nane kwa masharti nafuu. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa swali zima limejikita kwenye mambo ya pembejeo; na kwa kuwa wakulima wengi sana wa mazao kama ya pamba, muhogo, chai na hata korosho, wamekumbwa na tatizo la wadudu waharibifu. Kwa mfano, wakulima wa pamba na wakulima wa mahindi wanasumbuliwa na yule fall armyworm wakulima wa muhogo wanasumbuliwa na cassava mealybug.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua ni nini mkakati wa Serikali kumwondolea adha mkulima ambaye anajitahidi kulima sana lakini anasumbuliwa na hawa wadudu au viwavijeshi ambao ni waharibifu zaidi? Nataka tamko la Serikali.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. American fall army worm wameonekana kwa mara ya kwanza nchini mwaka jana. Jitihada ya Serikali iliyofanyika ya kwanza ilikuwa ni kuhakikisha elimu inawafikia wakulima wote namna ya kukabiliana na hawa wadudu. Kwa hivyo, tulichokifanya ni kueneza hii elimu lakini na kufanya utafiti wa haraka kubaini ni aina gani ya dawa inayoweza kuuwa hawa wadudu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dawa hiyo tumekwishaitangaza ili mwananchi akiona mazao yake yanashambuliwa atumie dawa hiyo kuuwa hawa wadudu. Tunafanya hivyohivyo na kwa visumbufu vingine vya mimea.

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha kwa wingi nafaka za mahindi, ngano na shayiri lakini inashangaza kuona kuwa ruzuku ya pembejeo imepungua kutoka vocha 20,000 kwa mwaka 2012/2013 hadi vocha 10,000 mwaka 2014/2015:- • Je, ni kwa nini vocha zimepungua na lini Serikali itaanzisha mfumo mpya wa pembejeo? • Je, Serikali inatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba Mawakala wa pembejeo hawawauzii wananchi kwa bei kubwa kuliko bei ya soko?

Supplementary Question 9

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mheshimiwa Ngombale na siyo Mheshimiwa Katani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali mwaka huu ilijielekeza kwamba sisi wa zao la ufuta tutatumia Stakabadhi Ghalani…
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mheshimiwa Vedasto Ngombale sio Mheshimiwa Katani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Katani hayupo kwa leo. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru baada kuwa sasa umetambua jina langu vizuri. Ninachosema ni kwamba Serikali ilielekeza mwaka huu katika zao la ufuta utaratibu wa manunuzi utafanyika katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani na kwamba mikoa yote inayolima ufuta itatakiwa kuingia katika mfumo huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa ninavyozungumza ufuta umeshakuwa tayari na kuna baadhi ya mikoa tayari wameshaanza kuuza katika mfumo holela na Serikali iko kimya haijasema chochote. Naomba kufahamu, je, tutaingia katika mfumo wa Stakabadhi Ghalani au tutaendelea katika utaratibu ule ambao tulikuwa tumeufanya mwaka jana? Ahsante.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kweli kwamba, ufuta ni moja ya zao ambalo Serikali ilidhani na inatarajia kuliweka kwenye Mfumo wa Stakabadhi Ghalani, lakini ili uingie kwenye huo mfumo yako maandalizi ya msingi ambayo lazima yafanyike vinginevyo mfumo hautafanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunachofanya sasa hivi tunakamilisha hayo maandalizi, tutakuwa na mkutano wa wakuu wa mikoa yote inayolima ufuta ili tujiridhishe kwamba maandalizi hayo yako in place tuweze kuanzisha mfumo wenyewe.