Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka waganga, watumishi wa afya pamoja na vitendea kazi katika zahanati za Same Magharibi zilizojengwa kwa ushirikiano wa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Kakunda, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, je, atakuwa tayari kufika katika Wilaya ya Same ili kwenda kuona hali ambayo ipo sasa hivi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Wilaya ya Kilolo inajenga hospitali kubwa na nzuri, je, ni kiasi gani cha wahudumu au Madaktari wanaweza kuwatengea kwa msimu huu?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mwamoto na Mheshimiwa Dkt. Mathayo huko aliko kwamba nitafika Same baada tu ya Bunge la bajeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mwamoto kwa kufanya ufuatiliaji wa kina na wa karibu, katika kipindi cha miezi minne au mitano ameweza kufanikiwa na Serikali imepeleka pale zaidi ya shilingi bilioni nne kwa ajili ya kujenga hiyo hospitali ya wilaya na Mheshimiwa Rais juzi ameweka jiwe la msingi. Nimhakikishie tu kwamba tutashirikiana na wenzetu wa utumishi kuhakikisha hospitali ile inapata watumishi wa afya kwa mujibu wa kitange na uwezo wa Serikali.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka waganga, watumishi wa afya pamoja na vitendea kazi katika zahanati za Same Magharibi zilizojengwa kwa ushirikiano wa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi hii. Kwa kweli wananchi wa Wilaya ya Same kwa ujumla wao wanajitahidi sana kujenga zahanati. Ningemwomba Mheshimiwa Waziri aone umuhimu wa Serikali kwenda kuona jitihada zile, naomba atuambie hapa ndani atakwenda lini na atatoa msaada gani kwa sababu hali ya wananchi hasa wa milimani upande wa afya ni mbaya sana?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Anne Kilango Malecela na wananchi wote wa Wilaya ya Same kwamba nitakapokwenda katika Wilaya ya Same sitaishia katika Jimbo la Same Magharibi peke yake bali nitapita mpaka kwenye Jimbo la Same Msahariki. (Makofi)

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka waganga, watumishi wa afya pamoja na vitendea kazi katika zahanati za Same Magharibi zilizojengwa kwa ushirikiano wa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Nini utaratibu wa Serikali katika kuhakikisha wananchi au mashirika mbalimbali wakishajenga zahanati hizi kwa mfano Jimbo la Vunjo Zahanati ya Kochakindo ina zaidi ya miaka mitano ilijengwa na TASAF haina watumishi wala vifaa kwa ajili ya kutoa tiba. Utaratibu wa Serikali ni upi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu kwamba swali la Mheshimiwa James Mbatia linaonekana ni maalum kwa eneo maalum. Kwa hiyo, namwomba sana baada ya kikao hiki leo hii tuweze kuonana ili anipe details.