Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Hali ya barabara zinazosimamiwa na halmashauri ni mbaya sana kutokana na fedha zinazotolewa na Mfuko wa Barabara kukaa kwa muda mrefu na hali ya kuongezeka kwa magari binafsi na yale ya biashara ambapo kila tarafa ina zaidi ya magari 20 na hivyo, kufanya barabara hizo kuharibika na kuwa vigumu kupitika nyakati za masika:- (a) Je, Serikali haioni haja ya kuleta mapendekezo mapya ya mgao wa fedha za barabara? (b) Barabara nyingi za Halmashauri ya Mji wa Mbulu zimejifunga katika Tarafa za Nambis na Daudi. Je, kwa nini wataalam kutoka Wizarani wasifike kuzikagua na kutoa ushauri stahili? (c) Je, kwa nini BQ za tenda za barabara ngazi ya mkoa zisiwekwe kwenye kitabu cha RRB, ili Waheshimiwa Wabunge na wananchi wafahamu shughuli zitakazofanywa na makandarasi waliopewa kazi?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza maswali madogo ya nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa sababu swali hili lilikuwa la mwezi wa Pili mwaka huu. Hivi sasa ni kweli, barabara hizo nilizozitaja zimefanyiwa matengenezo, lakini kwa kuwa, sasa fedha zinazotengwa kwa wenzetu wa TARURA kutengeneza hizi barabara za vijijini ni kidogo sana je, Serikali haioni umuhimu mkubwa wa kutafuta vyanzo vingine na kuhakikisha kuwa, barabara zote zinazohudumiwa na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini, anaweza kupatiwa fedha za kutosha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sisi wote Wabunge humu ndani ni mashahidi, maeneo mengi yanayopata makorongo makubwa katika halmashauri zetu na majimbo yetu yanahitaji mdaraja makubwa. Fedha zinazotolewa kwa wenzetu wa TARURA ni kidogo sana kiasi kwamba, hata kama wangepewa fedha makorongo hayo hayapo katika jiografia au mtandao wa barabara wanazohudumia wenzetu wa TARURA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa je, Serikali haioni ni wakati wa kuja na mpango mkakati wa kuhakikisha kuwa maeneo yote yanayohitaji madaraja makubwa ambayo ni kikwazo kwa huduma za kijamii zikiwemo kliniki za akinamama, huduma za afya na elimu zinapatiwa mpango mkakati wa kujengewa madaraja hata ya chuma? Kwa kuwa, eneo hilo ni tete na…

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ni kweli, fedha ambazo tunazipata kwa ajili ya matengenezo ya barabara nchi nzima, ikiwemo pesa za TANROADS na TARURA ni kidogo. Sasa hivi uwezo wa fedha tunazopata ni asilimia 57 ya mahitaji. Hata hivyo niseme tu kwamba, kati ya fedha tunazozipata asilimia 90 zinakwenda kufanya matengenezo ya barabara, kwa hiyo, utaona kwamba ni asilimia 10 tu ndiyo inayokwenda kujenga barabara mpya. Kwa hiyo iko haja ya kuongeza fedha kwenye matengenezo ya barabara zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba, lile zoezi la kutambua network ya barabara kwa upande wa wenzetu wa TARURA, limefanyika, lakini kulikuwa na changamoto ya data ambazo zilipatikana; ikalazimika TARURA waende maeneo husika ili tuweze kuzitambua barabara zote ili sasa mgawo wa fedha na mahitaji ya fedha tuweze kuyaona kwa uhakika zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vigezo ambavyo vinatumika ni pamoja na urefu wa mtandao wa barabara, tunatumia vigezo pia vya aina ya barabara, kama ni barabara ya lami, barabara ya changarawe, barabara ya udongo na hali ya barabara ilivyo na idadi ya magari yanayopita katika maeneo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumejipanga na TARURA wanafanya kazi nzuri na ni kesho tu tunategemea taarifa itawasilishwa TAMISEMI, itawasilishwa kwenye Mfuko wa Barabara na upande wa kwetu kwenye Wizara, ili tuangalie mahitaji yetu halisi na tuweze kuomba fedha zaidi kukamilisha maeneo ambayo ni korofi. Kwa hiyo, kazi inaendelea ya kuhakikisha barabara zetu tunaziboresha.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Hali ya barabara zinazosimamiwa na halmashauri ni mbaya sana kutokana na fedha zinazotolewa na Mfuko wa Barabara kukaa kwa muda mrefu na hali ya kuongezeka kwa magari binafsi na yale ya biashara ambapo kila tarafa ina zaidi ya magari 20 na hivyo, kufanya barabara hizo kuharibika na kuwa vigumu kupitika nyakati za masika:- (a) Je, Serikali haioni haja ya kuleta mapendekezo mapya ya mgao wa fedha za barabara? (b) Barabara nyingi za Halmashauri ya Mji wa Mbulu zimejifunga katika Tarafa za Nambis na Daudi. Je, kwa nini wataalam kutoka Wizarani wasifike kuzikagua na kutoa ushauri stahili? (c) Je, kwa nini BQ za tenda za barabara ngazi ya mkoa zisiwekwe kwenye kitabu cha RRB, ili Waheshimiwa Wabunge na wananchi wafahamu shughuli zitakazofanywa na makandarasi waliopewa kazi?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, Mheshimiwa Waziri amesema fedha za TARURA ni kidogo na yeye amepita barabara za Mbulu, hasa Tumati kwenda Martado ni mbaya sana. Je, atatusaidiaje kwenye kipindi hiki ili barabara zile ziweze kutengenezwa na wananchi wakaondoa ile adha ya kupita kwenye barabara ambayo haipitiki kwa sasa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyoeleza katika jibu la msingi na kama ambavyo amejibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa muuliza swali la msingi, Mheshimiwa Kwandikwa Naibu Waziri wa Ujenzi; taarifa ya tathmini ile ya kina ambayo tutaipata kuanzia kesho, hiyo ndiyo itakayotupatia taarifa sahihi ya barabara zote ikiwemo barabara ile ya kwenda Tumati ambayo tulipita na Mheshimiwa Mbunge kuanzia Yaeda Chini mpaka Tumati kule barabara si nzuri sana. Kwa hiyo, tutaiwekea utaratibu mzuri sana wa kipaumbele baada ya kuwa tumekubaliana vizuri zaidi na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Hali ya barabara zinazosimamiwa na halmashauri ni mbaya sana kutokana na fedha zinazotolewa na Mfuko wa Barabara kukaa kwa muda mrefu na hali ya kuongezeka kwa magari binafsi na yale ya biashara ambapo kila tarafa ina zaidi ya magari 20 na hivyo, kufanya barabara hizo kuharibika na kuwa vigumu kupitika nyakati za masika:- (a) Je, Serikali haioni haja ya kuleta mapendekezo mapya ya mgao wa fedha za barabara? (b) Barabara nyingi za Halmashauri ya Mji wa Mbulu zimejifunga katika Tarafa za Nambis na Daudi. Je, kwa nini wataalam kutoka Wizarani wasifike kuzikagua na kutoa ushauri stahili? (c) Je, kwa nini BQ za tenda za barabara ngazi ya mkoa zisiwekwe kwenye kitabu cha RRB, ili Waheshimiwa Wabunge na wananchi wafahamu shughuli zitakazofanywa na makandarasi waliopewa kazi?

Supplementary Question 3

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tatizo la barabara katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu linafanana kabisa na tatizo la barabara katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mlowo katika Jimbo la Mbozi. Naomba kuuliza, ni lini sasa Serikali itatengeneza barabara ambazo zipo katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mlowo, Jimbo la Mbozi, ambazo wakati wa mvua mara nyingi zimekuwa hazipitiki?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli. Tatizo alilolisema Mheshimiwa Mbunge katika eneo lake ni tatizo ambalo limekuwa likiikabili nchi nzima wakati wa masika wakati mvua kubwa zikinyesha, hasa barabara zetu ambazo huwa zinaathirika sana ni barabara za udongo na barabara za changarawe, ukiacha barabara za lami ambazo maeneo machache, hasa ya madaraja ndio huwa yanaathirika zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nimpe ndugu yangu comfort kwamba, suala hilo linatambulika Serikalini. Katika tathmini ambayo tunaifanya tumezingatia hilo ili tuwe na backup ya kutosha wakati wa mvua kuweza kukabiliana na changamoto ambazo huwa zinajitokeza wakati wa masika.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Hali ya barabara zinazosimamiwa na halmashauri ni mbaya sana kutokana na fedha zinazotolewa na Mfuko wa Barabara kukaa kwa muda mrefu na hali ya kuongezeka kwa magari binafsi na yale ya biashara ambapo kila tarafa ina zaidi ya magari 20 na hivyo, kufanya barabara hizo kuharibika na kuwa vigumu kupitika nyakati za masika:- (a) Je, Serikali haioni haja ya kuleta mapendekezo mapya ya mgao wa fedha za barabara? (b) Barabara nyingi za Halmashauri ya Mji wa Mbulu zimejifunga katika Tarafa za Nambis na Daudi. Je, kwa nini wataalam kutoka Wizarani wasifike kuzikagua na kutoa ushauri stahili? (c) Je, kwa nini BQ za tenda za barabara ngazi ya mkoa zisiwekwe kwenye kitabu cha RRB, ili Waheshimiwa Wabunge na wananchi wafahamu shughuli zitakazofanywa na makandarasi waliopewa kazi?

Supplementary Question 4

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa, wananchi wa Yulansoni, Lelembo hadi Kitumbili ni wazalishaji wakubwa na barabara hiyo haimo kabisa kwenye mtandao na TARURA haiwezi kutengeneza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI alishatembelea huko na kutoa ahadi ya kutafuta pesa ili barabara hiyo itengenezwe. Je, ni lini barabara hiyo itatengenezwa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kiula, Mbunge wa Iramba Mashariki ambako tunaita maarufu Mkalama, lakini wenyewe tu hawajaleta ombi la kubadilisha jina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba, kuna changamoto kubwa sana katika eneo hilo lote la Mkalama. Wiki mbili zijazo nitatembelea Mkalama, tutapita mpaka hiyo barabara anayoitaja. Hata hivyo kwa hali halisi nitoe tu comfort kwa Bunge lako Tukufu na Wabunge wote, kwamba wenzetu Wahandisi, taaluma yao ni ya kuaminika kwa sababu wanajenga vitu vya kuonekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa si kwamba tunadharau taaluma nyingine, ila ni kwa sababu wanajenga vitu ambavyo vinaonekana. Kwa hiyo ili kusudi wafanye kazi zao vizuri, mazingira ambayo tunayaandaa kupitia tathmini ambayo tumeifanya ni kuhakikisha kwamba, tunaweka mazingira mazuri ili kazi zao watakazozifanya ziweze kuonekana vizuri zaidi kwa wananchi.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Hali ya barabara zinazosimamiwa na halmashauri ni mbaya sana kutokana na fedha zinazotolewa na Mfuko wa Barabara kukaa kwa muda mrefu na hali ya kuongezeka kwa magari binafsi na yale ya biashara ambapo kila tarafa ina zaidi ya magari 20 na hivyo, kufanya barabara hizo kuharibika na kuwa vigumu kupitika nyakati za masika:- (a) Je, Serikali haioni haja ya kuleta mapendekezo mapya ya mgao wa fedha za barabara? (b) Barabara nyingi za Halmashauri ya Mji wa Mbulu zimejifunga katika Tarafa za Nambis na Daudi. Je, kwa nini wataalam kutoka Wizarani wasifike kuzikagua na kutoa ushauri stahili? (c) Je, kwa nini BQ za tenda za barabara ngazi ya mkoa zisiwekwe kwenye kitabu cha RRB, ili Waheshimiwa Wabunge na wananchi wafahamu shughuli zitakazofanywa na makandarasi waliopewa kazi?

Supplementary Question 5

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa Chombo cha TARURA ni kipya na kilipoandaliwa kilipewa fedha ndogo; na kwa kuwa fedha iliyotengwa na Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo, anazifahamu sana barabara za Mpwapwa, barabara za mjini na barabara za Mima; je, TARURA iko tayari kuongezwa fedha ili zile barabara za Mpwapwa Mjini na Mima ziweze kutengenezwa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, kwanza katika sehemu ya kwanza ya swali lake, maana kauliza kama maswali mawili; ni kwamba TARURA iko tayari kuongezwa fedha, hiyo, niseme wazi. Pia jambo la msingi la pili ni kwamba tunajua mazingira yote katika Tarafa ya Mpwapwa na Tarafa ya Mima kwa sababu, aliuliza swali la msingi hapa na katika swali la msingi tukamuahidi kwamba, tutatuma wataalam. Wataalam wamekwenda kule wakiwemo Wahandisi walioko kwenye jimbo lake, wamefanya tathmini na wametuletea ofisini, hivyo, tutaifanyia kazi katika mwaka ujao wa fedha.