Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, ni vigezo vipi ambavyo Serikali imeviweka juu ya kampuni zinazowekeza kwenye michezo nchini kuruhusiwa Ligi husika kubeba majina ya kampuni hizo kama vile Vodacom Premier League badala ya Tanzania Premier League?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Swali la kwanza, kwa kuwa Serikali imekiri kabisa kwenye ligi ya Uingereza ilijulikana kama Backlays English Premier League na siyo Backlays Premier League, pia hata Kagame Cup haikujulikana kama Kagame Cup inajulikana kama CECAFA Kagame Cup. Serikali haioni haja sasa kwamba umefika wakati wa kuitangaza Tanzania kwenye michezo na league yetu ikaitwa Tanzania Vodacom Premier League? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Kampuni ya Azam wameanzisha mashindano makubwa sana yanaitwa Azam Sports Federation Cup, nichukue fursa hii kuwapongeza sana, je, Serikali haioni haja sasa ya kushawishi na makampuni mengine yaweze kuanzisha mashindano ili ku-promote soko la Tanzania? (Makofi

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwalimu Mussa Sima kwa kifupi sana, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza pendekezo la kuweka jina la Tanzania kabla ya jina la mdhamini lina mashiko, tutalifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la kampuni nyingine kuiga mfano wa Azam, nami naunga mkono suala hilo. Natoa wito kwa makampuni mengine yajaribu kuiga mfano wa Azam ili tuweze kukusa soka katika nchi yetu.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, ni vigezo vipi ambavyo Serikali imeviweka juu ya kampuni zinazowekeza kwenye michezo nchini kuruhusiwa Ligi husika kubeba majina ya kampuni hizo kama vile Vodacom Premier League badala ya Tanzania Premier League?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa soka la wanawake limekuwa likifanya vizuri sana hapa nchini na kimataifa, lakini soka hili halina wadhamini wa kulidhamini. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuhamasisha wadau mbalimbali ili waweze kulidhamini soka hili la wanawake nchini? (Makofi)

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Toufiq, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, soka la wanawake pamoja na kwamba limechelewa sana kupewa uzito stahili katika nchi yetu, tayari lina wadhamini. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Toufiq kwamba kila mwaka tunazidi kuongeza juhudi za kuwapata wadhamini. Moja ya nyenzo kuu ya kuwapata wadhamini wengi zaidi ni kuhakikisha kwamba tunaomba au tunaingia mikataba na kampuni mbalimbali za utangazaji ili soka hiyo iweze kuonyeshwa live katika luninga zetu na hata kutangazwa katika redio mbalimbali.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, ni vigezo vipi ambavyo Serikali imeviweka juu ya kampuni zinazowekeza kwenye michezo nchini kuruhusiwa Ligi husika kubeba majina ya kampuni hizo kama vile Vodacom Premier League badala ya Tanzania Premier League?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kweli udhamini katika soka la wanawake hauridhishi na league ya mpira wa miguu ya wanawake inaendeshwa katika mazingira magumu sana. Ni kwa nini isiwe ni lazima kila udhamini unaopatikana kwa league ya wanaume uende sambamba na udhamini pacha wa league ya wanawake? (Makofi)

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtolea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba udhamini kwa timu za wanawake siyo mkubwa kama ulivyokuwa kwenye timu za wanaume, lakini lazima tuangalie historia kwamba league kuu nchi hii miaka 50 iliyopita ilianza kwa wanaume tu na tulianza na timu chache tu kama sita, lakini sasa hivi tuna timu 16 na mwaka ujao tutakuwa na timu 20. Kwa hiyo, imeongezeka ukubwa na udhamini wake lazima tuupiganie nao uwe mkubwa vilevile. Sasa hivi ndiyo tumeanza na ligi ya wanawake, tumepata udhamini mdogo, lakini tunaendelea na juhudi kuongeza ukubwa wa udhamini wa timu za wanawake kulingana na ukubwa wa league yenyewe.