Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. SEIF K.S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuipongeza Wizara hii ya Nishati ikiongozwa na Mheshimiwa Medard Kalemani pamoja na Mheshimiwa Subira Mgalu kwa kazi kubwa wanasozifanya kuhakikisha kwamba umeme unapatikana katika maeneo yenye shida ya umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu msingi ambalo nilitaka kujua kwa sababu tumeshaanza utelezaji wa uzambazaji wa umeme katika baadhi ya maeneo yaliyotajwa lakini tumeanza kwa kusuasua. Je, ni lini sasa kama Wizara; Mheshimiwa Waziri pamoja Mheshimiwa Naibu Waziri wataweza kuja kuona maendeleo ya mradi huu katika maeneo hayo yaliyotajwa kwa sababu uzambazaji wa umeme huo mwisho wake ni Juni, 2019? Ujio wao utasababisha msukumo kuwa mkubwa na kazi hii itafanyika kwa haraka zaidi. Je, ni lini wataweza kufika katika maeneo hayo tajwa? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nampongeza sana Mheshimiwa Gulamali kwa jinsi ambavyo anatupa ushirikiano katika kupeleka umeme kwenyeJimbo lake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa katika Jimbo la Gulamali mkandarasi yuko katika Kijiji cha Matinje ambacho pia ni cha wachimbaji wadogo wa madini. Nimpe tu taarifa Mheshimiwa Mbunge, wakandarasi watakapotoka Matinje wanakwenda Nsimbo na ili wafike Nsimbo ni lazima wapite Mwamala, Tambarale, Uswaya na Igoweko. Kwa hiyo, vijiji vyake ambavyo amevitaja kimsingi vitapata umeme kwa wakati mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ni lini tutakwenda tena, napenda kutumia nafasi hii kumwambia Mheshimiwa Gulamali kwamba mara baada ya Bunge tutatembelea maeneo yake kwa sababu tunataka tutembelee maeneo yote ya Mkoa wa Tabora. Mkoa wa Tabora unahitaji umeme wa nishati wa kutosha kwa sababu ni mkubwa. Kwa hiyo, tutakwenda Roya kwa Mheshimiwa Ntimizi, tutakwenda Mswaki pamoja na maeneo mengine ya Waheshimiwa Wabunge wa Tabora. Ahsante.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wilaya ya Hanang ilipata vijiji vichache sana awamu ya kwanza ya REA na awamu ya pili. Hii awamu ya tatu Mheshimiwa Waziri ameniahidi atanipa vijiji vingi lakini vile tulivyokubaliana ameacha Gocho, Dumbeta, Gisambalang’ na Getasam. Mheshimiwa Waziri amesema atakwenda na mimi sasa anaahidi kila mmoja, sijui kama atapata nafasi ya kwenda na mama yake. Ahsante. (Kicheko)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ni kweli nilimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba nitakwenda Hanang, lakini kabla sijaenda Hanang tulimpa vijiji 47 vya kuanzia na tukamwongezea vijiji vingine 12, kwa hiyo, lazima tuvitembelee. Kati ya vijiji ambavyo tumeviongeza ni pamoja na Gocha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwahakikishie wananchi wa Hanang mbali tu na kuongozana na Mheshimiwa Mbunge lakini nitawatuma wakandarasi waanze kufanya kazi hizo ili wakati tunakwenda, tunakwenda kuwasha na wala siyo kukagua peke yake.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli REA III ni vijiji 10 tu kati ya 42 ndivyo vimewekwa kwenye mpango. Je, ni lini Serikali itaongeza vijiji vingine katika REA III katika Halmashauri yetu ya Wilaya ya Monduli?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeze Mheshimiwa Mbunge. Tumekaa na Mheshimiwa Mbunge wiki iliyopita. Ni kweli kabisa tulipopitia katika Jimbo la Monduli tulikuta ni vijiji 10 tu ambavyo tumevipangia umeme. Baada ya kufanya mapitio kwa nchi nzima, tumeongeza vijiji 1,442 na vijiji 12 vya Mheshimiwa Mbunge wa Monduli vimo. Kwa hiyo, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa wazo lake zuri lakini tumefanya mapitio na tumeongeza vijiji zaidi ya 1,542 kwa nchi mzima. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge maeneo yote ambayo tulikuwa tumeyaruka hivi sasa kwa kiasi kikubwa tumeyaingiza ili nao wapelekewe umeme kwa pamoja.

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. HASNA S.K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru kwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni timu ikiongozwa na Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kigoma walienda Tarafa ya Nguruka kukagua vijiji vyote vitakavyopatiwa umeme REA III lakini hadi leo hii tunavyoongea, mkandarasi alikuwa afike tarehe 2 Juni, 2018 hajakanyaga kwenye vijiji hivyo ambavyo vinatakiwa vipate umeme kwenye Tarafa yangu ya Nguruka. Je, ni lini sasa mkandarasi atafika na kuanza kazi kuingiza umeme kwenye vijiji vyangu vya Tarafa ya Nguruka?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati namjibu Mheshimiwa Nsanzugwanko nimesema, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge anavyofuatilia maeneo hayo. Jumatano ijayo mkandarasi kwa Mkoa wa Kigoma tunamkabidhi site nasi tutafuatilia utekelezaji wake. Nampongeza Mheshimiwa Mbunge wa Uvinza, eneo la Nguruka litakuwemo kwenye mpango huu pamoja na eneo la Ilagala na maeneo mengine. Kwa hiyo, Jumatano ijayo Mheshimiwa Mbunge wa Uvinza mkandarasi pia atafika na maeneo yake yataanza kupelekewa umeme kwa wakati mmoja.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 5

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Kata ya Lyamkena, Kijiji cha Kiumba Makatani Kilabuni, Mheshimiwa Waziri anajua, walichomeka nguzo na baadaye wakaziondoa. Ni lini mtawarudisha nguzo zile ili wananchi waendelee kupata umeme? Nataka kauli ya Serikali. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa nilifika Jimbo la Mheshimiwa Sanga na kwa kweli nilitembelea maeneo yale, eneo la Makatani, leo asubuhi kabla sijaja hapa wamepeleka nguzo nyingine 20. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakandarasi wako site wanaendelea na kwa vile amenikumbusha pia kesho nitamwagiza Meneja akafuatilie utekelezaji wa maeneo hayo ambayo ameyataja.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 6

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Manispaa ya Mtwara Mikindani ina mitaa mingi ambazo nguzo za umeme hazijafika na nimekuwa nikiitaja hapa Bungeni kwa muda mrefu sana, kwa mfano, Kijiji cha Mbwala Chini, Mtaa wa Naulongo, Mkunja Nguo, Kata ya Magomeni, Kata ya Ufukoni na Kata ya Mitengo maeneo mengi hayana nguzo za umeme. Nilikuwa naomba kujua kwa sababu nimeongea kwa muda mrefu ndani ya Bunge hili, kwa nini Serikali haitaki kuwapatia wananchi hawa umeme? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Maftaha, lakini kusema kwamba Serikali haitaki, siyo kweli, ukweli ni kwamba Serikali inataka kuwapelekea umeme wananchi wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge, wiki iliyopita niliongea naye, Kijiji cha Mkunja Nguo tayari mkandarasi tumeshamtuma na ameshafanya survey. Maeneo mengine ya Mbwala Chini bado wanafanya survey. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge maeneo yote ya Mtwara Mjini ambayo ameyataja yatapelekewa umeme na mara baada ya Bunge hili tutakwenda kukagua. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge vijiji 12 na mitaa nane ya Mtwara Mjini tutaipelekea umeme kupitia mradi huo unaoendelea.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 7

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa mradi wa uzambazaji wa umeme REA III katika Jimbo la Lulindi ni wa kusuasua sana na mkandarasi hadi jana alikuwa hajafunguliwa LC. Je, Mheshimiwa Waziri anataka kuwaambia nini wananchi wa Jimbo la Lulindi ambao wanasubiri kwa hamu umeme huo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Bwanausi anavyofuatilia maendeleo ya wananchi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tumeshafanya uzinduzi kwa Mheshimiwa Bwanausi na kijiji cha Kalipinde tayari kilishawashwa umeme na baada ya kutoka Kalipinde inakwenda kata inayofuata. Ni kweli kabisa mkandarasi hatua ya kwanza alianza kwa kusuasua kwa sababu kulikuwa na masuala ya kiutawala na kiusimamizi yaliyokuwa yanaendelea. Hivi sasa naipongeza Wizara ya Fedha imeshafungua LC, advance payments zimelipwa, ni matumaini yetu sasa mkandarasi atakwenda kwa speed. Nimhakikishie Mheshimiwa Bwanausi kwamba mara baada ya Bunge tutamfuatilia mkandarasi huyu ili awashe umeme vijiji vingi kwenye jimbo lako.

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:- Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Supplementary Question 8

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niulize swali la nyongeza. Kampuni ya East Africa Fossils Limited inakamilisha kazi ambayo iliachwa na Spencon ya kupeleka umeme awamu ya pili katika Tarafa ya Nkoko, Jimbo langu la Manyoni Mashariki. Kutokana na kasi kubwa ya kampuni hii kumekuwa na uhaba mkubwa sana wa nguzo za umeme. Mpaka navyozungumza hapa wameshachimbia mashimo karibu kilomita 10 nguzo hamna, kila wanapoulizwa wanasema Mufindi imezidiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini nguzo zitapelekwa katika kampuni hii ili tuweze kukamilisha suala la umeme katika Tarafa ya Nkoko?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampa pole kwa msiba alioupata hivi karibuni lakini tunafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa sana na Mheshimiwa Mtuka na ana kata nne ambazo hatujazigusa. Mkandarasi ameagiza nguzo 2,278 na amenipa taarifa kwamba kuanzia wiki ijayo nguzo zitaanza kwenda site. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mtuka kwamba maeneo yote ya kata zake 12 na hizi nne tulizoongeza yatapelekewa umeme kwa sababu sasa nguzo zinapatikana. (Makofi)