Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Kata ya Maji Moto wameanza kuwekeza kuitikia kauli mbiu ya viwanda; na kwa kuwa hawana umeme wa uhakika; na kwa kuwa, REA Awamu ya Tatu, round ya kwanza haijulikani itaanza kutekelezwa lini katika Jimbo la Kavuu, je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuharakisha hizi tafiti zao za geothermal kwa ajili ya kuwapatia wananchi wa Maji Moto umeme? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa vijiji vya Kibaoni, Usevya, Ilalangulu na Manga vimefikiwa na umeme unaotoka Sumbawanga, lakini kumekuwa na tatizo kubwa la kukatika kwa umeme katika maeneo hayo na kufanya wananchi katika Kata ya Kibaoni kupata hasara sana kutokana na kukatikakatika kwa umeme. Je, Serikali inawaeleza nini wananchi waliopata umeme huu ambao ni wa Kata ya Kibaoni kupata umeme wa uhakika ambao hauwatii hasara? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda sana kushukuru maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kikwembe, lakini kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika Mkoa mzima wa Katavi na hasa Jimbo la Mheshimiwa Dkt. Kikwembe lina shida na kero za umeme. Katika maswali yake ya msingi mawili, la kwanza ni geothermal. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge, kati ya maeneo ambayo kwa kweli yanafanyiwa tafiti za kutosha katika upande wa geothermal ni pamoja na eneo la Maji Moto katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo 50 ambayo tunatarajia kuyafanyia upembuzi yakinifu kwa ajili ya kujua mashapo ya geothermal ni pamoja na Jimbo lake. Hivi sasa TGDC wanaendelea na kazi hiyo na mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 20 kwa ajili ya kazi hiyo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Dkt. Kikwembe nampongeza sana kwa hoja hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na umeme wa uhakika katika maeneo ya Mheshimiwa Mbunge, Katavi pamoja na Sumbawanga, Serikali imeanza utaratibu wa kujenga njia kuu ya kusafirisha umeme wa kilovoti 400. Katika maeneo ambayo tutayapatia kipaumbele sana ni pamoja na Jimbo la Kavuu ambapo maeneo ya Maji Moto ni maeneo ya kibiashara, kwa hiyo, njia kuu za kusafirisha umeme zitakamilika. na tumetenga shilingi bilioni 664 kwa ajili ya kazi hiyo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Dkt. Kikwembe nampongeza sana, lakini Serikali inalifanyia kazi. Ni matarajio yetu kuanzia Januari miundombinu inaanza kujengwa.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Katika Jimbo la Mbulu Mjini kuna maporomoko ya Haino katika Tarafa ya Nambisi, Kata ya Nambisi. Maporomoko hayo ambayo wataalam kutoka Serikalini na taasisi mbalimbali zisizo za Serikali wameendelea kuyatembelea; na kwa kuwa, tuna mahitaji makubwa ya uzalishaji wa umeme nchini, je, ni lini Mheshimiwa Waziri na Wizara yake watatembelea maporomoko ya Haino ili yaweze kutoa mchango wake katika sekta ya umeme kwa nchi nzima na hususan Jimbo la Mbulu Mjini?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issaay, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali tunatambua uwepo wa maporomoko haya ambayo kwa mujibu wa tafiti mbalimbali yana uwezo hata wa kuzalisha Megawati 5,000. Kupitia Serikali na TGDC tuna mpango wa kuhakikisha kwamba tunazalisha Megawati 200 kupitia maporomoko mbalimbali ambayo yataleta nishati ya joto ardhi ifikapo 2025, naomba nimkubalie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama Serikali kupitia Wizara ya Nishati tutafanya ziara katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema Mheshimiwa Waziri kwenye jibu lake kwamba kwa mwaka huu kuna maeneo kama 50 ambayo yatafanyiwa tafiti likiwemo eneo la maporomoko hayo katika Jimbo la Mbulu Mjini. Ahsante sana.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ujenzi wa miradi ya umeme awamu ya pili na awamu ya tatu bado utekelezaji wake hauendi kasi kama ilivyopangwa hasa katika Mkoa wa Rukwa, Jimbo la Kwela na tatizo kubwa ikiwa ni upatikanaji wa nguzo. Mkoa wa Rukwa unahitaji nguzo 13,000. Pamoja na jitihada zote, ni nguzo 350 tu zilizopatikana. Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hilo ili miradi ya umeme iweze kutekelezwa haraka?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge na kweli nilitembelea eneo lake. Nimhakikishie tu kwamba kero ya nguzo kwa sasa kimsingi haipo. Mwanzoni mwa mwaka 2017 tulisitisha kuingiza nguzo kutoka nje ambapo ndiyo lilikuwa tatizo la Wizara kwa muda mrefu. Waagizaji wa nguzo walikuwa wanachukua miezi sita hadi nane kufikisha hapa nchini, hivi sasa nguzo zinapatikana. Mahitaji yetu ya nguzo kwa mwaka ni 200,800 wakati nguzo zinazopatikana kwa wazalishaji wa ndani ni nguzo 2,000,872. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge miradi hii itatekelezeka kwa kiasi kikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimetembelea Jimbo la Mheshimiwa Mbunge na nampongeza sana anavyohangaikia maendeleo ya wananchi wake. Ni kweli mkandarasi anasuasua na jana tumemwelekeza, hivi sasa anaendelea katika Kijiji cha Maendeleo ili kusudi aanze kuwapatia wananchi umeme. Kwa hiyo, tunampongeza sana Mheshimiwa Mbunge lakini suala la nguzo hivi sasa siyo kero kubwa. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kitunda, Mvute, Mbondole, Nzasa na Iyongwa kote huko kuna sekondari. Maeneo yote haya ambayo nimeyataja hayana umeme. Naomba nijue ni lini maeneo haya ya umma yenye zahanati, shule na wananchi watapelekewa umeme wa uhakika? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Waitara. Mimi kwanza ni mpiga kura wake katika Jimbo lake, naelewa sana maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti ni kweli kabisa maeneo ya Mbondole na maeneo mengi sana ya Chanika hayana umeme, lakini maeneo yote 27 yameingia kwenye Mpango mahususi wa Peri-Urban ambao utekelezaji wake umeshaanza. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge utekelezaji huu unaanza mwezi Julai na utakamilika mwezi Machi mwakani. Kwa hiyo, ni matarajio yetu ndani ya miezi mitano vijiji vyote vitakuwa vimeshapata umeme maeneo ya Mbondole.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 5

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa nami niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme unaotokana na joto ardhi ama geothermal ni endelevu na sustainable ama renewable na Serikali ingeweza kutumia vyanzo vyote tungepata zaidi ya Megawati 5,000. Je, ni lini Serikali itaweza kukamilisha mradi wake ambao ilikuwa inaendelea kuufanya wa kuchoronga visima katika Ziwa Ngosi lililopo Wilayani Rungwe pamoja na Mto Mbaka uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa swali zuri. Kusema ukweli kati ya maeneo ambayo tunayafanyia upembuzi yakinifu kwa ajili ya kujua mashapo ya geothermal, yako zaidi ya 50. Tunachofanya sasa hivi, tunapitia marejeo ya takwimu sahihi katika Ziwa Ngosi ambao liko Mbozi, maeneo ya Katavi pamoja na Rukwa. Tathmini za awali zinaonesha kwamba mashapo yaliyopo ya geothermal yanaweza kutupa jumla ya Megawati 5,000 kwa wakati mmoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa tunakwenda hatua kwa hatua, tunataka kuanza Megawati 20 hadi Megawati 100. Kwa hiyo, ni matarajio yetu kwamba ndani ya miaka hii miwili tutakuwa tumeshapata mashapo sahihi ili tuanze sasa na Megawati 100 kwa ajili ya geothermal.

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 6

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Mradi wa REA III kuna Kitengo kimeanzishwa kinaitwa Peri-urban katika Halmashauri ambazo bado zina maeneo ya vijiji na vitongoji. Je, ni lini kitengo hiki kitaanza kufanya kazi katika Halmashauri zetu kwenye Kata za Kilare, Mzizima, Pongwe, Marungu na Maweni ili tuweze kupata huduma hii ya umeme wa REA III?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimeeleza katika ufafanuzi wangu uliotangulia, ni kweli tunatekeleza miradi miwili kwa mijini. Uko mradi wa urbanisation unaotekelezwa na TANESCO lakini uko mradi wa Peri-urban ambao unatekelezwa kimtindo wa REA, ingawa katika mitaa ya mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Mheshimiwa Mbunge kule Tanga Mjini yako maeneo 17 ambayo tumeshaainisha ikiwemo na Izizima pamoja na Majani Mapana. Utekelezaji umeanza kufanyika, ndani ya miezi sita ni matarajio yetu utakamilika na maeneo yake yataanza kupata umeme kwa utaratibu wa Peri-urban.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 7

MHE. DANIEL K. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwulize Mheshimkiwa Waziri, Mikoa ya Katavi na Kigoma, REA III haijaanza kwa sababu ya migogoro iliyoko Mahakamani, lakini taarifa tulizonazo ni kwamba ruling imeshatoka. Ni lini sasa mkandarasi ataanza kazi katika Mikoa ya Kigoma na Katavi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Nzanzugwanko. Ni kweli kabisa Mikoa miwili ya Katavi na Kigoma ilikuwa na migogoro katika Mahakama zetu. Napenda kutoa taarifa mbele ya Bunge lako Tukufu kwamba mgogoro huo kimsingi kwa upande wa Ujiji umetatuliwa, mgogoro uliobaki ni ile kesi ya kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe taarifa tu kwa upande wa Mkoa wa Kigoma, namshukuru sana Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ijumaa ametupa mwelekeo na sisi kuanzia Jumatano ijao, mkandarasi tunamkabidhi rasmi mkoa nzima wa Kigoma. Mkandarasi kwa upande wa Katavi tunakamilisha maandalizi ya manunuzi ili mwisho wa mwezi huu naye akabidhiwe. Ufikapo mwezi Julai, utekelezaji wa REA III kwa mikoa miwili ya Katavi na Kigoma utakuwa umeshaanza na tayari kukabidhiwa kwa wananchi.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Katika Bunge lililopita la 2010 – 2015 Serikali iliongelea kuhusu mpango wa kuwekeza umeme unaotumia chemchemi ya maji ya moto yanayopatikana katika Kata ta Maji Moto:- a) Je, mpango huo umefikia wapi? b) Je, ni lini sasa Jimbo la Kavuu litapata umeme kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo?

Supplementary Question 8

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tarafa ya Ilongero iliyopo Wilaya ya Singida Vijijini ambayo iko kwenye bonde la ufa haijawahi kupata umeme tangu REA I na II na ya sasa imeanza kutekelezwa. Kuna Kituo cha Afya ambacho hawawezi kutoa huduma kwa sababu hakuna umeme. Je, ni lini sasa Serikali itawapatia umeme wananchi wale au Waziri aongozane tu nami twende kwenye Tarafa ile akashuhudie ili aweze kuwahimiza wakandarasi waweze kukamilisha umeme katika bonde lile? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mlata, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa natambua kwamba Kata ya Ilongero iko kwenye mpango wa upelekaji umeme katika awamu inayoendelea. Hivi sasa mkandarasi ameshakaribia maeneo yale, ametoka Marendi kwa Mheshimiwa Mwigulu na wiki ijayo atakwenda Ilongero ambapo kuna Kituo cha Afya. Kwa hiyo, nimpe uhakika Mheshimiwa Mlata kwamba atafika kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuongezana na Mheshimiwa Mlata, mimi sina wasiwasi, kama kawaida yangu nitaambatana na Mheshimiwa Mlata tukatatue kero za wananchi. Ahsante sana.