Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATHIFAH H. CHANDE aliuliza:- Serikali ilitenga jumla ya shilingi bilioni 6.4 kwa mwaka 2012 mpaka mwaka 2015 kwa ajili ya ukarabati wa kawaida wa barabara ya Nangurukuru – Liwale yenye urefu wa kilometa 230 na barabara hii inawaunganisha watu wa Liwale na Wilaya za Lindi na Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam:- Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali la kwanza, kwa sababu ni Sera ya Serikali kuunganisha mikoa kwa barabara ambazo ndizo tunazitegemea kwa ajili ya maendeleo yetu. Ni lini tutegemee Serikali itaunganisha barabara inayotokea Liwale Mkoa wa Lindi kuweza kufika Morogoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, kwa muda mrefu sana Serikali imekuwa ikijificha kwa kusema kwamba kumekuwa na upembuzi yakinifu ukiwa unafanyika na mara nyingi upembuzi huu umekuwa ukichukua muda mrefu na wakati mwingine inaweza kufika hata miaka 10 tunakuwa kwenye upembuzi yakinifu. Ni lini tutegemee Serikali itaweza kuweka limitation au taratibu ambapo kutakuwa na muda maalum wa upembuzi yakinifu kufanyika ili ujenzi wa barabara uwe unaanza kufanyika mapema? Ahsante. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lathifah, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba ni Sera ya Serikali kuunganisha mikoa. Kama nilivyojibu wiki iliyopita wakati nikijibu swali la Mheshimiwa Mlinga, nilisema kwamba tutakwenda kutazama kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Lindi kwa maana ya Liwale na Mahenge, lakini hii ni siku za usoni, kwa sababu ziko logistics nyingi lazima zifanyike kwa sababu barabara hiyo itapita katika Hifadhi ya Selous lakini pia structures zake zinahitaji fedha nyingi. Kwa hiyo, tutaendelea kuitazama na Serikali inajua umuhimu wa kipande hiki cha barabara kuunganisha kuja Mahenge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwamba Serikali inajificha kwa kusema inasanifu na kutengeneza michoro; hili siyo kweli. Niseme kwamba mpaka sasa hivi barabara za lami zinazounganisha mikoa karibu mikoa yote tunakamilisha. Barabara zaidi ya kilometa 13,000 tumeshatengeneza kwa lami kwa maana ya kuunganisha mikoa na nchi za jirani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata katika bajeti hii ya mwaka 2018/2019, tumependekeza kufanya usanifu wa barabara kilometa 3,856. Hizi ni kilometa nyingi sana na hii ni kuonesha jinsi namna gani Serikali ya Chama cha Mapinduzi iko committed kuhakikisha kwamba kila tunapokamilisha barabara fulani ni mwanzo wa kuendelea kusanifu barabara nyingine. Kwa hiyo, Mheshimiwa Lathifah ataendelea kusikia tukisanifu na kutengeneza michoro ya barabara kila wakati kwa sababu kila wakati tunavyokamilisha ujenzi wa barabara, kwetu sisi kama Serikali ni fursa ya kutengeneza barabara nyingine. Ahsante sana.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATHIFAH H. CHANDE aliuliza:- Serikali ilitenga jumla ya shilingi bilioni 6.4 kwa mwaka 2012 mpaka mwaka 2015 kwa ajili ya ukarabati wa kawaida wa barabara ya Nangurukuru – Liwale yenye urefu wa kilometa 230 na barabara hii inawaunganisha watu wa Liwale na Wilaya za Lindi na Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam:- Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, barabara inayotokea Singida Mjini – Ilongero – Mtinko – Mudida – Kidarafa – Ikungi - Haydom yenye urefu wa kilometa 93.4 ujenzi wake kwa kiwango cha lami umekuwa ukisuasua. Kukamilika kwa barabara hii kutaharakisha sana shughuli za maendeleo kwa Singida Vijijini. Barabara hii ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne…
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia iko katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015. Je, ni lini sasa barabara hii itakamilika kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuharakisha shughuli za maendeleo kwa wananchi wa Singida Vijijini? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aisharose Matembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara hii imekuwa ikitengenezwa kidogo kidogo lakini nimfahamishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba matengenezo yale aliyoyaona yalitokana na usimamizi mzuri wa Meneja wa TANROADS Mkoa wa Singida. Kila alivyobakiza fedha ameendelea kutengeneza kilometa moja, kilometa mbili na takriban sasa tuna kilometa 10 zimetengenezwa kwa mtindo huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua umuhimu, mwaka huu wa fedha 2018/2019, tumetenga shilingi milioni 200 kuanza usanifu wa kilometa hizi 93 kwenda Haydom. Nami wiki zilizopita nimepita kwenye barabara hii kuweka msisitizo kwamba usanifu uanze mara moja mara baada ya kupata fedha ili sasa barabara hii iungane na barabara itakayokuwa inatoka Haydom kuja Sibiti, barabara kubwa hii ambayo itajengwa kwa kiwango cha lami ili wananchi wa Singida na maeneo mengine ya jirani waweze kwenda kirahisi kupata huduma katika Hospitali ya Haydom.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. LATHIFAH H. CHANDE aliuliza:- Serikali ilitenga jumla ya shilingi bilioni 6.4 kwa mwaka 2012 mpaka mwaka 2015 kwa ajili ya ukarabati wa kawaida wa barabara ya Nangurukuru – Liwale yenye urefu wa kilometa 230 na barabara hii inawaunganisha watu wa Liwale na Wilaya za Lindi na Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam:- Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL M. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kufahamu kutoka Serikalini kwamba barabara ya Masasi inayopitia Vijiji vya Nangaya – Chikunja – Lukuledi – Naipanga – Mkotokuyana mpaka Nanganga inaelekea kujengwa kwa lami hivi karibuni. Hata hivyo, uthamini wa mali na rasilimali za watu katika maeneo hayo yote niliyoyataja umefanyika zaidi ya miaka mitano iliyopita. Je, Serikali itakwenda kurudia kufanya uthamini au itawalipa watu wale fidia zao kutokana na uthamini uliofanyika miaka mitano iliyopita? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecil Mwambe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimfahamishe tu Mheshimiwa Mwambe pamoja na wananchi kwamba uthamini uliofanyika kama hakuna matatizo makubwa ya kurudia, ndiyo utakaotumika kulipa wananchi hawa. Niwafahamishe tu wananchi kwa ujumla kwamba utaratibu uliopo kuna namna ya kuangalia thamani ya fedha kwa sasa, lakini base itakayotumika ni ule uthamini uliofanyika kipindi ambacho Mheshimiwa Mbunge amekitaja. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi, uko utaratibu mzuri wa kuhakikisha kwamba fedha zile zitalipwa kulingana na hali ya sasa.