Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Jasson Samson Rweikiza
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukoba Vijijini
Primary Question
MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Barabara ya kuanzia Kanazi, Kata ya Kemondo kupitia Ibwera kwenda Katoro, Rubale na Izimbya ipo chini ya TANROADS, na ni muhimu kwa wakazi wa Bukoba na kwa uchumi wa Taifa:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 1
MHE. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ina kata 29. Kati ya hizo, kata 20 zinahudumiwa na barabara niliyoitaja. Kata hizo ni Katerero, Kemondo, Ibwera, Nakibimbiri, Kasharu, Kisogo, Kaibanja, Katoro, Kyamuraire, Ruhunga, Mugajalwe, Izimbya, Kibirizi, Kaitoke, Kikomero, Rukoma, Rubare, Buterakuzi, Mikoni na Bujugo. Aidha, Bukoba kuna mvua nyingi sana barabara ya udongo inaharibika, mara nyingi inakuwa haipitiki na huko ndiyo kuna mazao mengi kama kahawa na ndiyo uchumi mzima uko kule. Kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kujenga lami barabara hii? (Makofi)
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rweikiza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua maeneo haya ni muhimu sana katika uzalishaji na pia tunatambua kwamba ziko mvua nyingi na kumekuwa na uharibifu wa mara kwa mara. Nampongeza tu Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu mara nyingi tumezungumza juu ya kuhakikisha kwamba barabara hizi tunazitengeneza na kwa kweli kama alivyosema, hizi ni kata nyingi sana, kata 20 kati ya kata 29.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge ikiwa ni pamoja na wananchi wa maeneo ya Kata hizi ikiwemo Kata za Katerero, Kemondo, Ibwera na kata nyingine kwamba baada ya kukamilisha kuunganisha mkoa na mikoa mingine nguvu kubwa tutailekeza katika maeneo haya ya barabara ambazo zinapita kwenye wilaya zetu ikiwemo maeneo haya aliyoyataja ili sasa tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa Bukoba Vijijini kwamba maeneo haya tutayatazama na tutayaweka katika mpango ili siku za usoni tuweze kuitengeneza barabara kwa kiwango cha lami.
Name
Abdallah Majurah Bulembo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nominated
Primary Question
MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Barabara ya kuanzia Kanazi, Kata ya Kemondo kupitia Ibwera kwenda Katoro, Rubale na Izimbya ipo chini ya TANROADS, na ni muhimu kwa wakazi wa Bukoba na kwa uchumi wa Taifa:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 2
MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri kuhusu swali lililopita, naomba kuiuliza Serikali, barabara ya Kyaka 2 kutoka Katoro - Ishembulilo - Kashamba - Kyaka; eneo lile ni bovu sana kila mwezi Aprili barabara haipitiki. Pamoja na kwamba amesema inahudumiwa na TANROADS, naomba commitment ya Serikali ya kuweka madaraja kwenye maeneo yale ili mwezi wa Aprili kuwe kunapitika kama sehemu nyingine. (Makofi)
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bulembo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu nimhakikishie Mheshimiwa Bulembo kwamba nimemsikia, nami nimwelekeze tu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kagera aende kuangalia eneo hili na kushauri tufanye nini juu ya kutengeneza daraja eneo hili korofi. Kama ilivyo kawaida, maeneo yote korofi nchi nzima tunaendelea kuyashughulikia wakati tukiendelea na harakati za kuboresha barabara kuhakikisha wananchi wetu wanapita muda wote katika maeneo yao.
Name
Venance Methusalah Mwamoto
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilolo
Primary Question
MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Barabara ya kuanzia Kanazi, Kata ya Kemondo kupitia Ibwera kwenda Katoro, Rubale na Izimbya ipo chini ya TANROADS, na ni muhimu kwa wakazi wa Bukoba na kwa uchumi wa Taifa:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 3
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa Rais mwezi Mei alifika Iringa katika Wilaya ya Kilolo na akatoa ahadi kwamba barabara ile ya kutoka Ipogolo - Kilolo ambayo inaitwa sasa barabara ya Mfugale ianze kujengwa mara moja. Je, ni lini barabara hiyo itaanza kujengwa ili ahadi ile ya Rais aliyotoa kwa wananchi iweze kutimia? (Makofi)
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwamoto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana kwa sababu tumezungumza sana juu ya barabara hii hata kabla ya ahadi ya Mheshimiwa Rais. Kwa vile Mheshimiwa Rais ametoa ahadi kuitengeneza barabara hii, tulikubaliana kwamba baada ya Bunge hili nitatembelea huko ili tuweze kuweka msisitizo kuhakikisha kwamba barabara hii inajengwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi natambua kwamba barabara hii ilishasanifiwa. Kwa hiyo, harakati za ujenzi wa barabara hii, napenda wananchi wa Kilolo wajue ujenzi ulishaanza kwa sababu hatua za awali tumeshaanza, sasa ni zoezi la kupata fedha ili barabara ijengwe. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mwamoto asiwe na wasiwasi barabara hii itajengwa na kwa msisitizo wa Mheshimiwa Rais tutakwenda kuijenga barabara hii. (Makofi)
Name
Willy Qulwi Qambalo
Sex
Male
Party
CHADEMA
Constituent
Karatu
Primary Question
MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Barabara ya kuanzia Kanazi, Kata ya Kemondo kupitia Ibwera kwenda Katoro, Rubale na Izimbya ipo chini ya TANROADS, na ni muhimu kwa wakazi wa Bukoba na kwa uchumi wa Taifa:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 4
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ujenzi wa barabara ya Oldian Junction – Mang’ola – Matala - Kolandoto umeshakamilika miaka miwili iliyopita na barabara hiyo ni muhimu sana kwa sababu inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu. Je, ni lini sasa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hiyo utaanza?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Qambalo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ukiotokea upande wa Lalago ukivuka Sibiti kwa kushoto kule iko barabara hii ambayo itakuwa inakwenda Karatu ambayo michoro na usanifu wake umeshakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ina interest kubwa sana kwa sababu kuna uzalishaji mkubwa, historia muhimu na pia kuna utalii mkubwa katika maeneo haya. Kwa hiyo, kwa sababu hatua hii imeshakamilika, tuko kwenye hatua ya kutafuta fedha, wakati wowote tukipata fedha ujenzi utaendelea. Ahsante sana.
Name
Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bagamoyo
Primary Question
MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Barabara ya kuanzia Kanazi, Kata ya Kemondo kupitia Ibwera kwenda Katoro, Rubale na Izimbya ipo chini ya TANROADS, na ni muhimu kwa wakazi wa Bukoba na kwa uchumi wa Taifa:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 5
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Makofia - Mlandizi ni muhimu sana ambayo inaunganisha wananchi wa Halmashauri ya Bagamoyo na Kibaha Vijijini. Barabara hiyo sasa hivi ina matatizo sana ya kupitika hasa baada ya mvua hizi nyingi zilizopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii barabara ni ahadi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi mwaka 2005, 2010 na 2015 kujengwa kwa kiwango cha lami. Ni lini fidia italipwa kwa ajili ya barabara hiyo na lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kawambwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Kawambwa ni shahidi kwamba tumezungumza muda mwingi sana juu ya barabara hii. Barabara itakuwa na urefu wa kilometa zaidi ya 30 kuja Mlandizi. Kuhusu fidia tulishafanya tathmini tayari, tutaendelea kuwasiliana na wenzetu Wizara ya Fedha hizi fedha zipatikane ili wananchi hawa walipwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi watalipwa kwa sababu tulikuwa na fidia nyingi nchi nzima katika maeneo mbalimbali, lakini tumefika hatua nzuri, maeneo mengi tumeshalipa fidia. Kwa hiyo, Mheshimiwa Dkt. Kawambwa asiwe na wasiwasi. Nafikiri baadaye tuzungumze na tuongee na wataalam tuone hatua hii imefika wapi ili tuweze kulipa mara moja hii fidia ya wananchi wake.