Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika kampeni za uchaguzi mwaka 2010 Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga Kituo cha Afya katika Mji wa Nalasi na kutoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka:- (a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nalasi? (b) Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa ujenzi wa kituo kile cha afya ulitokana na ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea katika Kata zile mbili za Nalasi zilizoko katika kijiji kimoja na kuagiza kwamba kipatikane Kituo cha Afya; na kwa kuwa Halmashauri imekuwa ikipanga kila mwaka bajeti ya kujenga kituo kile kwa shilingi milioni 80 na shilingi milioni 75, lakini mpaka leo hii bado wameshindwa kujenga kituo kile. Je, Serikali haioni haja sasa ya kutimiza ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne kwa kutoa fedha kwa ajili ya kujenga kituo kile cha afya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, kwa kuwa Serikali imekiri kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina gari moja ambalo ni bovu tangu 2007, mpaka leo ni zaidi ya miaka 11; na kwa kuwa eneo la Tunduru ni kubwa sana, lina Majimbo mawili (Kusini na Kaskazini), je, Serikali haioni umuhimu sasa kutoa gari mbili za wagonjwa upande wa Kaskazini na Kusini ili kuweza kuhudumia wananchi wa Wilaya ya Tunduru ambao eneo lao ni zaidi ya square kilometer 18,000? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mpakate, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza anaulizia Serikali kutoa nguvu ili kumalizia hicho kituo cha afya. Pesa ambayo imepelekwa, shilingi milioni 400 na shilingi milioni 500 inaashiria dhamira njema ya Serikali ya kuhakikisha kwamba vituo vya afya vinajengwa hususan katika Halmashauri ya Tunduru. Halmashauri nayo ina vyanzo vyake, kwa bajeti ambayo inaisha mwaka 2017/2018 wameweza kukusanya wastani wa shilingi bilioni 2.78 na katika bajeti inayokuja, wanatarajia kukusanya shilingi bilioni 3.1, ni wazi kabisa hakika wakiweka kipaumbele cha kumalizia hicho kituo cha afya na kwa sababu wamesaidiwa na Serikali, wanaweza kumaliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili kuhusu kupeleka ambulance, ni kweli tangu mwaka 2007 ile gari itakuwa imeshakuwa chakavu kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi. Ni vizuri tukashirikiana na Halmashauri kwa kutumia vyanzo vyao wakati Serikali Kuu tunahangaikia, tukipata, tutakuwa tayari kuwafikiria lakini siyo vizuri nao wakabweteka kwa sababu wana chanzo kizuri na wanakusanya vizuri. Ni vizuri kiasi hicho ambacho kinapatikana wakatenga shilingi milioni 150 kwa ajili ya kununua ambulance, sidhani kama itaathiri sana Halmashauri. (Makofi)

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika kampeni za uchaguzi mwaka 2010 Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga Kituo cha Afya katika Mji wa Nalasi na kutoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka:- (a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nalasi? (b) Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina Vituo vya Afya vinne vya Kichiwa, Lupembe, Sovi na Matembwe. Katika vituo hivi vyote hakuna gari hata moja la wagonjwa, ni lini Serikali itatuletea gari la wagonjwa kwa ajili ya vituo hivi ukizingatia kwamba Kituo cha Lupembe tunafanya operesheni lakini hatuna gari? Inapotokea tatizo la watoto njiti, inakuwa ni shida sana kuwakimbiza Kibena, zaidi ya kilometa 80. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la ndugu yangu Mheshimiwa Hongoli, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nia njema ya Serikali kuhakikisha kwamba huduma za afya zinasogezwa na hasa maeneo ambayo ni mbali kuwe na gari kwa ajili ya kusafirisha wagonjwa. Pia ni ukweli usiopingika kwamba uhitaji ni mkubwa na ndiyo maana tumekuwa tukitoa magari kwa kadri yanavyopatikana na uwezo wa kibajeti unavyoruhusu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kadri fursa itakavyopatikana, tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba kule Lupembe ambako ni mbali nako gari inapatikana.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika kampeni za uchaguzi mwaka 2010 Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga Kituo cha Afya katika Mji wa Nalasi na kutoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka:- (a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nalasi? (b) Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka?

Supplementary Question 3

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Halmashauri nyingi ikiwemo ya Tabora Manispaa uwezo sasa wa kifedha hasa zile zinazotokana na own source umepungua kutokana na baadhi ya mapato ya Halmashauri kwenda kwenye Serikali Kuu na hii imesababisha huduma nyingine kama za afya na hasa vituo vya afya Halmashauri kushindwa kupeleka fedha kule kutokana na upungufu huo. Serikali ina mpango gani wa kuziba pengo hilo ili zile Halmashauri ambazo hazina uwezo ziweze kupata fedha ambazo zinaweza kusaidia vituo vya afya? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakasaka, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata fursa ya kutembelea Manispaa ya Tabora na katika nafasi ile tulitembelea na kuona vyanzo vya mapato vya Manispaa ya Tabora. Nilikuwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge na tukawashauri, vile vyanzo vilivyopo kwanza ni vizuri wakavisimamia wakahakikisha kwamba hakuna hata senti tano ambayo inapotea. Tulitembelea eneo la stendi, jinsi ambavyo wanakusanya hatukuridhika na jitihada ambazo zinatumika katika kukusanya, lakini pia kuna vyoo pale na maeneo mengi ambayo hakika wakisimamia vizuri, bado ni maeneo oevu ambayo pesa zinaweza zikakusanywa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kushirikiana na Halmashauri pamoja na TAMISEMI, nguvu yetu tukiweka pamoja hakika huduma katika vituo vya afya na hospitali zitaweza kuboreshwa. Naye mwenyewe ni shuhuda, ameona jinsi ambavyo bajeti ya afya imeongezeka kutoka shilingi bilioni 31 mpaka shilingi bilioni 269. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ni azma na nia ya Serikali kuhakikisha kwamba tunaboresha vituo vya afya.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika kampeni za uchaguzi mwaka 2010 Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga Kituo cha Afya katika Mji wa Nalasi na kutoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka:- (a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nalasi? (b) Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka?

Supplementary Question 4

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri alibahatika kufanya ziara katika Jimbo letu la Babati Mjini, nasi tukamuonesha jinsi gani tumeathirika baada ya vyanzo vyetu vya Halmashauri kuchukuliwa na Serikali Kuu. Hivi karibuni mliwaita Wakurugenzi, Wenyeviti wa Halmashauri na Maafisa Mipango mkasema kwamba mtatupatia fedha na gawio letu lilikuwa shilingi milioni 900 kwa ajili ya kukamilisha vituo hivi na miradi mingine. Naomba nifahamu, fedha hizo shilingi milioni 900 zinafika lini Babati maana Vituo vya Singe, Mutuka na Sigino tumeshapaua, tunasubiri hela za finishing?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gekul, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuliwaita Wenyeviti na Wakurugenzi ili waainishe vipaumbele katika maeneo ambayo yataenda kuanza kutumika pindi pesa itakapokuwa imepelekwa kule kwao na wakaainisha. Ofisi ya Rais, TAMISEMI zoezi lile tulishalikamilisha na tulishakabidhi Hazina. Ni matarajio yetu kwamba Hazina wakishakuwa na pesa ya kutosha kutoa, tutaweza kupeleka ili zikafanye kazi ambazo zilikusudiwa. (Makofi)