Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHIDI M. CHUACHUA) aliuliza:- Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Masasi halina nyumba za makazi na usafiri kwa muda mrefu sana:- a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea askari hao nyumba za kuishi kwa sababu nyumba wanazoishi sasa zimechakaa sana na pia hazitoshelezi mahitaji yao? b) Je, ni lini Serikali itawapatia usafiri wa uhakika Askari hao ili waweze kusimamia usalama wa raia na mali zao kwa uhakika?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Wizara inayo dira na inayo dira na mpango mkakati ambapo inatambua matatizo yaliyopo na hayo matatizo yanaiwekea katika mipango yake mikakati. Je, kwa mujibu wa mpango mkakati wake hizo nyumba za Askari wa Masasi zitajengwa lini?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa mujibu wa mpango wa mkakati huohuo na dira yake haya magari mawili au zaidi kwa Wilaya ya Masasi yatatolewa lini badala ya kuacha tu bila kuwekewa muda?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, kwamba kulingana na mipango tuliyokuwa nayo kuhusiana na ujenzi wa nyumba za Polisi Masasi pamoja na kupeleka gari, kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi kwamba mipango hii inategemea na upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Spika, katika eneo hili la nyumba bahati njema ni kwamba tayari tumeshapata fedha za kuanzia ambayo tunatarajiwa kujenga nyumba 400. Kwa hiyo, katika Mkoa wa Lindi pia nyumba hizo zitajengwa, naomba baada ya Bunge hili niangalie ili niweze kumpa takwimu halisi za wilaya ya Masasi kuhusiana na nyumba hizo zipoje.
Mheshimiwa Spika, katika eneo la gari nimezungumza kwamba, kulingana na hali ya uhalifu, hasa kubwa zaidi jiografia ya Masasi ilivyo inastahili kupata gari. Nikaeleza kwamba, pale ambapo magari yatapatikana basi katika maeneo ya vipaumbele vilevile Wilaya ya Masasi ni mojawapo. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge avute subira magari yakipatikana tutapeleka na bajeti ikikaa vizuri nyumba tutajenga. (Makofi)

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHIDI M. CHUACHUA) aliuliza:- Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Masasi halina nyumba za makazi na usafiri kwa muda mrefu sana:- a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea askari hao nyumba za kuishi kwa sababu nyumba wanazoishi sasa zimechakaa sana na pia hazitoshelezi mahitaji yao? b) Je, ni lini Serikali itawapatia usafiri wa uhakika Askari hao ili waweze kusimamia usalama wa raia na mali zao kwa uhakika?

Supplementary Question 2

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri, kama Waziri mwenye dhamana, nyumba za Magereza zilizoko pale Isanga hazifai, hazifai, hazifai kabisa kukaliwa na binadamu.
Mheshimiwa Spika, hata wewe kwa sababu ni mtu wa Dodoma, ukienda pale ukiona zile nyumba utasema hizi nyumba wanakaa binadamu? Naomba kupata tamko la Serikali, lini nyumba hizo zitajengwa upya kwa ajili ya Askari wetu hawa wa magereza katika Gereza Kuu la Isanga?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, ni kweli hata katika Jeshi la Magereza tuna changamoto ya uhaba wa nyumba na uchakavu wa nyumba za Askari Magereza. Ndiyo maana tunatumia njia mbalimbali ukiachilia mbali utaratibu wa kawaida wa kibajeti, tumekuwa tukitumia rasilimali katika maeneo husika kuzikarabati nyumba hizo, hasa ukitilia maanani kwamba,
Jeshi la Magereza lina kitengo madhubuti kabisa kinachojishughulisha na ujenzi pamoja na nguvu kazi ya wafungwa.
Mheshimiwa Spika, tumekuwa tukifanya hivyo maeneo mbalimbali katika nchi, lakini fursa kubwa ambayo inaangukia katika Gereza la Isanga lililopo Dodoma ni juu ya hatua ya Serikali kuhamisha Makao Makuu yake rasmi kuja Dodoma. Jambo hilo limesababisha sasa hivi kuwa na fursa pana ya kutanua wigo wa mazingira ya ufanyaji kazi pamoja na makazi ya Askari wa vyombo vyetu vyote. Ndiyo maana mtaona sasa hivi kwamba, katika eneo la Magereza, Uhamiaji na Jeshi la Polisi kuna maendeleo makubwa ya kuboresha makazi ya Askari Dodoma ili kwenda sambamba na kasi ya ongezeko la ukuaji wa Mji wa Dodoma kutokana na maamuzi thabiti ya Serikali ya kuhamishia Makao Makuu Dodoma.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHIDI M. CHUACHUA) aliuliza:- Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Masasi halina nyumba za makazi na usafiri kwa muda mrefu sana:- a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea askari hao nyumba za kuishi kwa sababu nyumba wanazoishi sasa zimechakaa sana na pia hazitoshelezi mahitaji yao? b) Je, ni lini Serikali itawapatia usafiri wa uhakika Askari hao ili waweze kusimamia usalama wa raia na mali zao kwa uhakika?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kituo cha Himo kiko mpakani na kinahudumia zaidi ya watu 500,000 na ukiangalia hali ya uhalifu, hasa mambo ya biashara za magendo mpakani ni kubwa. Serikali imekuwa ikiahidi kupatia kituo hiki gari, gari lililopo ni la zaidi ya miaka 10 na tulipewa na CRDB na gari hili limekuwa ni kazi ya Mbunge kulikarabati kila mwaka. Serikali imeshawahi kutoa ahadi zaidi ya mara tatu kuhakikisha wanapeleka gari Kituo cha Himo ili haki ya ulinzi na usalama wa Taifa ni kazi namba moja ya Serikali. Serikali watamke hapa ni lini wanapeleka gari hilo waliloahidi hapa immediately kabla Bunge hili halijamalizika kituo cha Himo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbatia amekuwa akiguswa sana na hili suala, nadhani si mara yake ya kwanza kuuliza hapa, mara ya mwisho nilimjibu na narudia jibu ambalo nimempa mara ya mwisho.
Mheshimiwa Spika, tunatambua changamoto za vituo vya Polisi vilivyopo mipakani, kikiwemo kituo cha Himo kama ambavyo amezungumza. Changamoto ambayo tunaipata sasa hivi ni kwamba, bado hatujapata magari mapya. Kwa hiyo, nikazungumza kwamba, tutaangalia sasa magari yatakapokuja yamekuja magari mangapi na wapi panahitaji zaidi.
Mheshimiwa Spika, natambua kituo ambacho amezungumza ni moja kati ya maeneo ambayo yanahitaji zaidi, itategemea wapi panahitaji zaidi sana na idadi ya magari yaliyopo. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge avute subira naamini kabisa kama siyo leo, kesho kama siyo kesho keshokutwa, lakini Serikali inatambua sana umuhimu wa maeneo haya, hasa mipakani kuwa na usafiri imara zaidi ili kudhibiti uingiaji na utokaji wa watu na bidhaa haramu katika nchi yetu.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHIDI M. CHUACHUA) aliuliza:- Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Masasi halina nyumba za makazi na usafiri kwa muda mrefu sana:- a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea askari hao nyumba za kuishi kwa sababu nyumba wanazoishi sasa zimechakaa sana na pia hazitoshelezi mahitaji yao? b) Je, ni lini Serikali itawapatia usafiri wa uhakika Askari hao ili waweze kusimamia usalama wa raia na mali zao kwa uhakika?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa, matatizo yanayotokea Masasi ni sawa kabisa na matatizo ya ndani ya Jimbo la Mlimba lenye kata 16, halina Kituo cha Polisi wala halina gari la Askari, hivyo kusababisha mahabusu kukaa muda mrefu kwenye kituo kidogo cha Polisi kilichopo pale TAZARA. Je, ni lini sasa na Waziri Mwigulu alishatembelea, Halmashauri tumeshatenga kiwanja na tuna baadhi ya matofali. Je, ni lini sasa Serikali itafikiria kuweka kituo cha Polisi Mlimba na kupata Askari wa kutosha ili kuwatawanya kwenye vituo ambavyo wananchi wamejitolea na tunakosa Askari kwa sababu hatuna mahali pa kuwaweka Askari kwa wingi pale Jimbo la Mlimba na hatuna kabisa usafiri na anajua? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni kweli mazingira yale aliyoyasema Mheshimiwa Mbunge nimeyashuhudia. Nilifika mazingira yale yanafanana kabisa na mazingira ya Jimbo la Mheshimiwa Joram Ismail Hongoli.
Mheshimiwa Spika, niseme tu Serikali inatoa uzito mkubwa kwenye maeneo kama hayo ambayo jiografia yake inalazimisha tuwe na usafiri wa kujitegemea ili kuweza kuwatengenezea mazingira mazuri Askari wetu ya kufanya kazi. Kwa hiyo, tunaweka uzito kwenye jambo hilo la usafiri pamoja na kituo hicho kikubwa anachokisemea. Punde tutakapoanza kutekeleza bajeti yetu na balance itakapokuwa imeruhusu tutatengeneza hili la kituo, lakini na hilo la gari tutakapokuwa tumeanza kugawa magari tutaweka uzito mkubwa katika Jimbo hilo.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHIDI M. CHUACHUA) aliuliza:- Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Masasi halina nyumba za makazi na usafiri kwa muda mrefu sana:- a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea askari hao nyumba za kuishi kwa sababu nyumba wanazoishi sasa zimechakaa sana na pia hazitoshelezi mahitaji yao? b) Je, ni lini Serikali itawapatia usafiri wa uhakika Askari hao ili waweze kusimamia usalama wa raia na mali zao kwa uhakika?

Supplementary Question 5

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 43 sasa, licha ya kukosa nyumba za Askari walioko kule hata kituo cha Polisi hatuna, umri wa miaka 43. Ni lini Serikali itatujengea Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Liwale, kuondokana na adha ya kupanga kwenye nyumba ambayo wamepanga, nyumba yenyewe nayo ni mbovu? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, ni sahihi. Liwale pia, inahitaji kuwa na kituo, niliwahi kuongea na Mheshimiwa Mbunge tukakubaliana kwamba, mara litakapomalizika Bunge twende pamoja mimi na yeye Jimboni kwake tuweze kushirikiana tuone jinsi gani tunaweza tukafanya ili kuharakisha huu mchakato wa ujenzi wa kituo hiki ikiwezekana kwa kuanzia kuwashirikisha wananchi na wadau mbalimbali wakati tukisubiri jitihada za Serikali za kukamilisha ujenzi wa kituo hiki zitakapokuwa zimekamilika. Kwa hiyo, ahadi yangu na Mheshimiwa Mbunge kama tulivyozungumza iko pale pale. (Makofi)