Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Joram Gidarya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA J. GIDARYA aliuliza:- Kituo cha Wazee Sarame kilichopo Magugu, Wilaya ya Babati Vijijini ni kituo cha muda mrefu ambacho kinahudumiwa na kusimamiwa na Wizara ya Afya. Kituo hiki kina changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa watumishi, usafiri wa dharura, huduma ya kwanza, vifaatiba na miundombinu ya barabara:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma zote za msingi katika kituo hicho ikizingatiwa kuwa wazee wengi ni walemavu wa viungo, vipofu, waliopooza na viziwi pia?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali, natambua kazi kubwa wanayofanya Waziri wa Afya na Naibu wake. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba niseme tu kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri waliyompelekea haya majibu wamemdanganya, kwa sababu mimi ni tomaso, naomba niambatane naye, nikapapase mwenyewe. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, matatizo yaliyoko kwenye hiki kituo ni matatizo makubwa sana. Kama kuna kitu ambacho Wizara haifahamu katika kile kituo kuna wazee 52 na katika hao 52 kuna wazee wanne ni kati ya wazee waliyopigania Vita vya Pili vya Dunia.
Mheshimiwa Spika, tuna matatizo makubwa ya Watumishi wa Afya tuna Watumishi wawili tu, mmoja anakaa Babati Mjini na mwingine anakaa kilometa moja na nusu kutoka kwenye kituo, maana yake usiku kukitokea dharura wale wazee hawapati huduma za haraka. Je, ni lini sasa Serikali itawajengea nyumba wale watumishi wapate kuishi karibu na wale wazee?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa nchi nzima idadi ya wazee inajulikana na kwa kuwa umri mkubwa wa uzee ndiyo unaopatikana na magonjwa makubwa nyemelezi pamoja na kuwa Serikali imesema huduma ya wazee ni bure. Je, Serikali iko tayari kuwapatia bima wazee wote nchi nzima? (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, labda nianze kwa kusema kwamba kuwepo na idadi kubwa ya wazee ambao sasa hivi wanafikia milioni 2.7 ni ishara kwamba kumekuwa na maboresho makubwa sana katika huduma ambazo tumekuwa tunazitoa katika ngazi ya afya, vilevile hali ya lishe na matunzo ambayo tumekuwa tunayatoa kwenye jamii yetu, kwa hiyo ni kitu ambacho najivunia. Sasa hivi umri wa kuishi wa Mtanzania umefikia miaka 65 wastani, kwa hiyo, ni jambo jema ambalo tunapaswa kujivunia.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na maswali ambayo ameuliza Mheshimiwa Anna Gidarya ni kweli tunatambua kwamba Serikali tumeendelea kuwa tunaboresha makambi haya ya wazee kadri uwezo unavyoongezeka. Pia hili ombi la kuhakikisha kwamba tunakuwa na nyumba katika kituo hichi cha Magugu, tutalifanyia kazi katika bajeti kama nilivyokuwa nimesema kwamba tuna fedha ambazo tumezitenga katika bajeti hii ambayo ipo.
Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, sasa hivi Serikali ipo katika mapitio ya sera ya afya. Katika sera ambayo tunaenda nayo sasa hivi ya mwaka 2017/2018 ambayo tunayo sasa hivi, tumekuwa tunasema kwamba matibabu kwa wazee yatakuwa ni bure, lakini sasa hivi Serikali tunaelekea katika mfumo wa kuwa bima ya afya kwa wote na masuala ya haki ya wazee yatazingatiwa katika sera hii mpya.
Mheshimiwa Spika, nimalizie kwa kusema tu kwamba kuhusiana na ombi lake la ziara kwenda kupapasa niko tayari kufanya Jumapili. (Kicheko)

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA J. GIDARYA aliuliza:- Kituo cha Wazee Sarame kilichopo Magugu, Wilaya ya Babati Vijijini ni kituo cha muda mrefu ambacho kinahudumiwa na kusimamiwa na Wizara ya Afya. Kituo hiki kina changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa watumishi, usafiri wa dharura, huduma ya kwanza, vifaatiba na miundombinu ya barabara:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma zote za msingi katika kituo hicho ikizingatiwa kuwa wazee wengi ni walemavu wa viungo, vipofu, waliopooza na viziwi pia?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mkoa wa Manyara ni mkoa mkubwa tu na una wilaya tano na majimbo saba na haiwezekani kuwapeleka wazee wote katika kituo kimoja tu kinachopatikana Magugu. Je, ni nini juhudi za Serikali katika kuhakikisha Wilaya ya Hanang’, Simanjiro, Kiteto na Mbulu tunapata kituo kingine cha wazee? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Ester Mahawe kwa kufuatilia maendeleo ya Manyara na Babati Mjini. Kwanza kwa mujibu wa Sera ya Wazee tunahamasisha wazee walelewe katika familia. Kwa hiyo Serikali haina mpango wa kujenga makazi ya wazee zaidi ya makao ya wazee 17 ambayo tunayo.
Mheshimiwa Spika, tunakusudia kutunga Sheria ya Wazee ambayo itatoa wajibu kwa watoto kutoa matunzo kwa wazee wao. Kwa sababu katika yale makambi kuna wazee wana watoto wao, wametelekezwa na familia zao. Kwa hiyo nitoe wito, niwausie Watanzania wazee hawa, wazazi wetu, wametulea, wamepigania nchi na sisi ni wajibu wetu kuwalea. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na niwaambie hata Wabunge tukichukua mzee mmoja au wawili tukakaa nao kwenye familia zetu ni baraka kwa Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA J. GIDARYA aliuliza:- Kituo cha Wazee Sarame kilichopo Magugu, Wilaya ya Babati Vijijini ni kituo cha muda mrefu ambacho kinahudumiwa na kusimamiwa na Wizara ya Afya. Kituo hiki kina changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa watumishi, usafiri wa dharura, huduma ya kwanza, vifaatiba na miundombinu ya barabara:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma zote za msingi katika kituo hicho ikizingatiwa kuwa wazee wengi ni walemavu wa viungo, vipofu, waliopooza na viziwi pia?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza ninasikitika hiyo kauli aliyotoa Mheshimiwa Waziri hapo na wale wazee ambao, maana yake mzee anaanzia kijana, mtoto ambaye inawezekana mazingira yake yote alikuwa ni yatima. Sasa huyu pia unamfanyaje, maana yake Serikali mnakwepa wajibu. Swali langu ni kwamba Serikali ya Awamu ya Nne iliahidi kutoa pensheni kwa wazee na tafiti zilishafanyika, kauli ikatolewa hapa Bungeni. Je, ni lini Serikali itatoa pensheni kwa wazee wetu?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, naomba nisisitize majibu ambayo amesema Mheshimiwa Waziri, kwa mujibu wa Sera yetu ya Wazee ya mwaka 2003 ambayo inatamka kwamba majukumu ya kwanza ya kumtunza mzee ni familia, ndugu na jamii husika kabla Serikali haijabeba majukumu hayo.
Mheshimiwa Spika, hivi tunavyoongea tunahudumia wazee zaidi 500 ndani ya nchi yetu. Kwa hiyo bado tunaendelea kusisitiza kwamba majukumu ya awali ya msingi yawe katika ngazi ya familia na jamii kabla ya Serikali haijachukua majukumu hayo.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake ambalo anauliza kwamba ni lini na tumefikia wapi katika pensheni hii ya wazee, bado Serikali inaendelea kulitafakari jambo hili, kuangalia utaratibu mzuri zaidi wa kuweza kulitekeleza. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ANNA J. GIDARYA aliuliza:- Kituo cha Wazee Sarame kilichopo Magugu, Wilaya ya Babati Vijijini ni kituo cha muda mrefu ambacho kinahudumiwa na kusimamiwa na Wizara ya Afya. Kituo hiki kina changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa watumishi, usafiri wa dharura, huduma ya kwanza, vifaatiba na miundombinu ya barabara:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma zote za msingi katika kituo hicho ikizingatiwa kuwa wazee wengi ni walemavu wa viungo, vipofu, waliopooza na viziwi pia?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa tunaamini kwamba wazee ni hazina ya Taifa letu, kama ilivyotengwa kitengo kwa ajili ya vijana, asilimia tano ya vijana na wanawake, Wizara haioni sasa ni busara kutenga pesa kwa ajili ya kuwalipa wazee wetu iwe kama…

Mheshimiwa Spika, nakushuru. Tunaamini kwamba wazee ni busara ya Taifa na ni hazina ya Taifa letu. Kwa kuwa asilimia tano imetengwa kwa ajili ya vijana na wanawake, Wizara sasa haioni ni busara kutenga fedha kwa ajili ya kuwalipa wazee wetu kama baraka katika Taifa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Spika, nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyotoa kuhusu masuala ya wazee. Kama Serikali na kama ilivyosema katika Ilani ya Uchaguzi miundombinu yote ya kuwezesha wazee hawa kuweza kulipwa imekwishaandaliwa. Kama Naibu Waziri alivyosema ni taratibu za ndani zinaendelea na pindi taratibu hizi zikikamilika, basi Serikali itatekeleza azma yake ya kuweza kuwalipa wazee pensheni kama ilivyosema katika Ilani ya Uchaguzi. Mheshimiwa Spika, nashukuru.