Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Je, kwa nini Serikali isianzishe utaratibu wa kupima mizigo na usajili wa abiria katika vyombo vyote vya majini kama inavyofanyika Airport ili kuepusha ajali za mara kwa mara?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naamini kabisa kwamba Mheshimiwa Waziri kwa maneno yake ya mwisho amekubaliana na mimi kwamba vipo vyombo ambavyo vinatumia bandari bubu na havijafanyiwa usajili na wala havikaguliwi mzigo yake. Sasa kama wanavyosema watu nywele nyeupe ni sababu ya kuwa na busara zaidi. Sasa je, atakubaliana na mimi kwamba sasa Serikali ipo haja ya kuhakikisha hata hivi vyombo vinavyotumia bandari bubu sasa vinakuwa na vyombo/zana za uokoaji kama life jacket na vitu vingine? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la nyongeza la pili ni kwamba, kwa nini kuna bandari bubu ni kwa sababu kuna tozo na kodi za kuudhi kwa watu wanaotoka Zanzibar na maeneo mengine katika bandari zetu ndiyo maana wanatumia bandari bubu. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuondoa hizi kodi kama kwenye TV moja, redio moja au nguo chache kwa watu wanaotoka Zanzibar na Pemba wanaokuja maeneo ya Tanga. Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kama nilivyoeleza mwanzo, umuhimu wa kutumia bandari rasmi tunapata data na kuhakikisha uimara na utayari wa chombo husika kusafirisha abiria kwa usalama zaidi. Kama Serikali, hatuwezi kuruhusu bandari bubu zitumike.
Mheshimiwa Spika, suala la tozo nikijibu swali lake la pili, tozo zinazotozwa kwenye vyombo vya baharini na maziwa makuu siyo kubwa sana kiasi cha kuruhusu watu waendelee kutumia bandari bubu. Namwomba Mheshimiwa Mbunge akubaliane na Serikali kwamba tozo zinazotozwa na affordable kabisa na zinatumika na watu ambao wanataka kufanya kazi kwa uhakika na kwa usalama zaidi kwa ajili ya abiria wao.

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Je, kwa nini Serikali isianzishe utaratibu wa kupima mizigo na usajili wa abiria katika vyombo vyote vya majini kama inavyofanyika Airport ili kuepusha ajali za mara kwa mara?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYNABU M. VULLU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa, bandari ya Nyamisati na bandari ya Kilindoni zimekidhi kigezo cha Serikali; na kwa kuwa wananchi wa kutoka Nyamisati kwenda Mafia au kutoka Mafia kwenye Nyamisati wanapata shida ya usafiri, uwezo wa majahazi yao hauzidi abiria 50 pamoja na mizigo yao. Je, ni lini Serikali itaondoa kadhia hiyo kwa wananchi wanaoishi maeneo hayo kwa kuwapelekea boti ambayo itakuwa salama na uhakika wa kusafirisha, ukizingatia kunakuwa na wazee, akinamama wajawazito, watoto, wanaokaa sana bandarini na kukosa usafiri wa uhakika? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana kwa jinsi anavyofuatilia hasa Bandari ya Nyamisati mpaka nimeshaizowea kuisikia kutoka kwake na Mheshimiwa Dau na wadau wote ambao wako Mkoa wa Pwani bila kumsahau Makamu Mwenyekiti wa Kamati yangu Mheshimiwa Hawa Mchafu.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna vyombo vinafanya kazi maeneo yale, lakini niwapongeze sana Wabunge wa eneo lile kwa sababu vyombo karibu vyote vinavyofanya safari kati ya Mafia na Nyamisati vimesajiliwa na ndiyo maana hata ikitokea ajali, huwa kuna utaratibu maalum ambao tunaweza kupata taarifa rasmi za ajali hiyo. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali ina mpango wa kupeleka boti muda huu wakati tunaendelea na utengenezaji wa land craft kubwa tumewapatia TEMESA Sh.3,800,000,000 kwa ajili hiyo.
Mheshimiwa Spika, hivyo nawaomba Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Pwani wasiwe na wasiwasi Serikali ina utaratibu wa kutengeneza kivuko kile pamoja na boat la kuwasafirisha abiria. (Makofi)

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Je, kwa nini Serikali isianzishe utaratibu wa kupima mizigo na usajili wa abiria katika vyombo vyote vya majini kama inavyofanyika Airport ili kuepusha ajali za mara kwa mara?

Supplementary Question 3

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa Serikali imebaini kuwa kuna bandari bubu na haziepukiki bandari bubu hizo. Je Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha hizi bandari bubu, wenye vyombo katika bandari bubu wanasajiliwa ili kuepusha ajali za mara kwa mara? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna changamoto ya bandari bubu na kama Serikali tumekuwa tukiendelea kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kuzirasimisha bandari hizo kwa msaada mkubwa sana wa Mamlaka ya Bandari Tanzania.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kuwasiliana na wadau ambao wanaendesha bandari bubu. Kwa sababu nyingine huwa zinakuwa zinachangamka kabisa na zinatakiwa zipewe miundombinu mbalimbali ya Kiserikali ili ziwe salama kwa ajili ya Watanzania. Nimhakikishie tu kwamba tutaendelea kuzitembelea na kuwapa elimu na inapotakiwa tutaendelea kuzirasimisha ili kuokoa maisha ya Watanzania waweze kusafiri salama. (Makofi)

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MUSSA B. MBAROUK aliuliza:- Je, kwa nini Serikali isianzishe utaratibu wa kupima mizigo na usajili wa abiria katika vyombo vyote vya majini kama inavyofanyika Airport ili kuepusha ajali za mara kwa mara?

Supplementary Question 4

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Toka asili bandari bubu ndiyo msaada mkubwa kwa wananchi hususani wa Visiwani baina ya Zanzibar na Mwambao wote huu wa Bahari ya Hindi. Linapokuja suala la bandari bubu na vyombo hivi mara nyingi vinaangaliwa vyombo vya baharini na vyombo vya maziwa vinakuwa vinaachiwa huru. Nataka kujua ni kwa nini bandari bubu ambazo wanazisema lakini zinakidhi viwango mfano Kipumbwi, Kigombe Tanga ambazo zinakidhi viwango hawazirasimishi haraka na kufanya kazi wananchi wakapata tija kwa safari zao?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, bandari bubu ni bandari bubu tu, hakuna namna ambavyo unaweza ukaifanya ikawa rasmi kwa kuibadilisha kwa maneno. Ni lazima taratibu za Kiserikali na Sheria zifuatwe kuifanya bandari bubu iweze kuwa rasmi. Nimewahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba bandari bubu zote ambazo zinakidhi vigezo tumekuwa tukizitembelea na kutoa elimu na kuwapa mapendekezo mbalimbali Kiserikali ambayo yatasababisha ziweze kuwa bandari rasmi.
Mheshimiwa Spika, Serikali haiwezi kufurahia kuendelea kuwa na bandari bubu na wala hatuwezi kuruhusu bandari bubu ziwepo, kikawaida bandari bubu zote hatuziruhusu. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tu kwamba, hizo bandari alizozitaja tutazitembelea, tutaongea na wadau, tukiona zinakidhi vigezo tutazisajili halafu zitakuwa bandari rasmi. (Makofi)