Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Kituo cha Afya Mlandizi kimetimiza vigezo vyote vya kuwa Haspitali ya Wilaya:- Je, ni lini sasa Serikali itapandisha hadhi Kituo hicho kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kinachoendelea kwa sasa katika Kituo cha Afya cha Mlandizi ni kuelemewa na lundo la wagonjwa, hususan upande wa afya ya uzazi. Ndani ya mwezi mmoja kuna wanawake zaidi ya 250 wanaojifungua. Idadi hii ni mara tatu ya walengwa wa Kituo hiko cha Afya cha Mlandizi, kitu ambacho kinapelekea kituo chetu kuwa na mahitaji makubwa ya matumizi ya dawa, vifaa tiba na huduma za kujifungua. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, sasa napenda kujua, wakati huu ambao hatuna Hospitali ya Wilaya na Serikali haina mpango wa kujenga Hospitali hiyo ya Wilaya: Je, Serikali itakuwa tayari kutupatia fungu maalum la fedha kila mwaka kwa ajili ya huduma hii ya afya ya uzazi? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kufuatia ongezeko hilo la wagonjwa kuwa mara tatu ya walengwa wa Kituo hicho cha Afya na kupelekea kituo chetu kuwa na deni kubwa takriban shilingi milioni 83 linalojumuisha matumizi ya dawa, vifaatiba, huduma ya uzazi na huduma nyingine, nangependa kujua, sasa Serikali itatusaidiaje ku-clear deni hilo, ukizingatia idadi hiyo ya fedha au kiasi hicho cha fedha ni mara mbili, tatu, nne mpaka tano ya mapato yote ya Kituo cha Afya cha Mlandizi? (Makofi) Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE): Mheshimiwa nakushukuru. Katika jibu langu la msingi, nimesema kwamba Serikali imeona uhitaji wa kujenga Hospitali ya Wilaya na tayari katika bajeti ya 2018/2019 tumetenga shilingi bilioni 1.5, ni kwa sababu tunatambua umuhimu na uhitaji mkubwa sana wa wananchi kwa suala zima la Afya. Kwa hiyo, tuko tayari na ndiyo maana tunajua kabisa kuna kuelemewa ndiyo maana tunaenda kujenga Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, anauliza, tunafanyaje katika kuwasaidia deni la jumla kama shilingi milioni 80? Ni vizuri kwanza tukajua chimbuko la deni hili nini na tukikaa baada ya kipindi cha maswali na majibu, tujue tatizo ni nini ili tuweze kusaidiana ili wananchi waendelee kupata huduma, lakini wakiwa wamevuta subira, Serikali yao ya CCM inawajali na ndiyo maana tunaenda kujenga Hospitali ya Wilaya.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Kituo cha Afya Mlandizi kimetimiza vigezo vyote vya kuwa Haspitali ya Wilaya:- Je, ni lini sasa Serikali itapandisha hadhi Kituo hicho kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami nataka niombe tu kwamba Kituo cha Afya cha Kata ya Vunta, Tarafa ya Mamba Vunta kimepandishwa hadhi kuwa Kituo cha Afya takriban miaka 10 iliyopita, lakini hakijafunguliwa rasmi kutokana na kwamba kilikuwa hakijapata ukarabati unaofaa.
Mheshimiwa Spika, pamoja kwamba tunashukuru Serikali ilipeleka Ambulance, namwomba Mheshimiwa Waziri kwamba ni lini Kituo hiki kitafunguliwa rasmi ili kitambulikane kwamba kweli ni Kituo cha Afya cha Tarafa ya Mamba Vunta yenye kata tano? Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kwa sababu kuna sifa ya zahanati kupanda kutoka zahanati kuwa kituo cha afya, naye mwenyewe amekiri, ingekuwa vizuri baada ya kutembelea eneo hilo ambalo mimi nipo tayari, ili tukaone kama kweli inakidhi haja ya kuwa Kituo cha Afya itakuwa ni furaha kwangu mie kuhakikisha kwamba inapata hadhi ya kuwa Kituo cha Afya kwa mujibu wa kukidhi vigezo ambavyo vimewekwa ili kiweze kuwa Kituo cha Afya.

Kimeshapandishwa? Kama tayari kimeshapandishwa, maana yake kuna baadhi ya taratibu ambazo hazijafuatwa. Naomba tukishamaliza hiki kipindi cha maswali na majibu, nipate fursa ili tuweze kuongea na DMO tujue hasa nini ambacho kimetokea kama tayari kimeshapandishwa, lakini hakiwi treated kama Kituo cha Afya.