Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wananchi wa Kagera wana tatizo la umeme na umeme wa REA II umeingia katika center za vijiji tu. Je, ni lini wananchi hao watapatiwa umeme ili waondokane na adha ya kutumia vibatari?

Supplementary Question 1

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nyingine. Nina maswali mawili ya nyongeza, naomba kuyauliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, katika Wilaya yetu ya Bukoba Vijijini kuna baadhi ya kata nitazisema japokuwa ni nyingi. Katika Kata ya Rubafu -Kijiji cha Bwendangabo, Kata ya Buma - Kijiji cha Bushasha, Kata ya Bwendangabo - Kijiji cha Kashozi, Kata ya Nyakato - Kijiji cha Ibosa; hizo ni baadhi ya Kata ambazo nimezitaja, lakini ni kata nyingi sana katika Wilaya yetu ya Buboka Vijijini au niseme Mkoa mzima wa Kagera tuna shida ya umeme.
Je, Serikali inaona umuhimu wa kuwapa kipaumbele cha kuweza kuwawekea umeme haraka iwezekanavyo? Hilo ni swali la kwanza.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi wa kata hizo hizo nilizozitaja wamenunua solar. Solar hizo tayari zimeshaharibika. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakiki hizo solar kabla hazijaingia sokoni? Ahsante. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza, amezitaja kata mbalimbali katika Wilaya yake ya Bukoba Vijijini na amewakilisha Mkoa mzima na ameeleza ni namna gani Serikali itaweka kipaumbele. Nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkoa huo wa Kagera kwa awamu hii ya tatu inayoendelea jumla ya vijiji 141 vitapatiwa umeme. Katika Wilaya yake ya Bukoba Vijijini, Kijiji cha Burugo kimeshasambaziwa nguzo na kazi zinaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Kata zile alizozitaja na vijiji alivyovitaja, kwa awamu hii ya kwanza vijiji kwa Bukoba vijijini ni 22, lakini kwa awamu ambayo itaendelea mzunguko wa pili unaoanza Julai vijiji vyote vilivyosalia vitapatiwa umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ameuliza masuala ya sola ambazo zimewekwa katika maeneo hayo ya Bukoba Vijijini na maeneo mengine ya Mkoa wake kwamba nyingi zimeharibika. Serikali ina utaratibu ndani ya Serikali na kwa Taasisi mbalimbali. Kwa mfano, kuna masuala ya TBS yanavyoangalia viwango na taasisi nyingine za kiserikali za kuangalia bidhaa zinazoingia ndani ya nchi zisiwe bidhaa ambazo kwa kweli ni fake.
Mheshimwia Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali yetu itaendelea kuziimarisha zile taasisi zinazohusika na kuzuia bidhaa feki ndani ya nchi ili kujiridhisha na vifaa hususani vya masuala ya nishati viingie vifaa bora na wananchi wapate huduma bora. (Makofi)
Mheshimwia Naibu Spika, nakushuruku Mheshimiwa. (Makofi)

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wananchi wa Kagera wana tatizo la umeme na umeme wa REA II umeingia katika center za vijiji tu. Je, ni lini wananchi hao watapatiwa umeme ili waondokane na adha ya kutumia vibatari?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM A. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la umeme lililopo Wilaya ya Kagera linafanana kabisa na tatizo la umeme mradi ule wa Makambako - Songea. Ule mradi umepita katika Kata tatu; Kata ya Kichiwa, Kata ya Igongoro na Kata ya Ikuna. Kwenye maeneo hayo kuna baadhi ya maeneo yana huduma muhimu kama shule, zahanati na vituo vya afya umeme haujapelekwa huko. Nini kauli ya Serikali kwa mkandarasi aliyesambaza umeme kwenye maeneo haya, kuhakikisha kwamba umeme unaenda kwenye maeneo yenye huduma muhimu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Katika mradi unaoendelea Makambako - Songea kwa kweli tunarajia mwezi Septemba mradi ule utakamilika na kuzinduliwa rasmi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi inayoendelea ya kusambaza umeme katika maeneo ambayo yameainisha, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa miradi hii ya kupeleka umeme vijiji ipo ya aina mbalimbali, kuna mradi wa Makambako - Songea ambao unalenga vijiji 121, lakini sambamba na hilo kuna mradi ambao unaendelea wa densification kwa maeneo ya Mkoa wa Njombe na Mkoa wa Iringa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mradi huu, densification ya awamu ya kwanza ina vijiji kama 305 na mradi umekamilika umefikia asilimia 98.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, maeneo ambayo hajasalia kama ambavyo tunafahamu mradi wa REA Awamu ya Tatu unaendelea na maeneo yale na maelekezo yetu kama Serikali, tumesema taasisi za umma iwe shule, iwe zahanati, iwe miradi ya maji na taasisi zote kwamba kipaumbele kwa wakandarasi waelekeze kwenye maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama Serikali tunaendelea kusisitiza hayo maelekezo na yaendelee kutekelezwa na Wakandarasi wote. Nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, kwa kweli kwa awamu inayoendelea, changamoto hizi hazitakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)