Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA (K.n.y. MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:- Sekta ya utalii inachangia pato kubwa la fedha za kigeni katika nchi yetu. Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara ya Serengeti ambayo ni mbovu kiasi cha kufanya watalii kukataa kupita huko?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto za miundombinu katika hifadhi ya Serengeti zinafanana na changamoto za Hifadhi mpya ya Kimisi na Burigi.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka miundombinu katika hifadhi mpya ya Kimisi na Burigi ili hifadhi hii iweze kuchangia mapato katika Halmashauri zetu za Wilaya zilizopo katika Mkoa wa Kagera pamoja na kuchangia pato la Taifa?
Swali la pili, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuambatana na mimi kwenda kwenye Kata za Bweranyange, Rugu, Nyakasimbi, Nyakabanga na Nyakakika ili kutatua migogoro ya mipaka kati ya vijiji kwenye Kata hizi na Hifadhi? Ahsante sana.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza sana Wabunge wa Mkoa wa Kagera kwa jinsi ambavyo wameshirikiana na Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yale yanapandishwa hadhi na sasa Burigi na Kimisi yatakuwa ni mojawapo ya Hifadhi za Taifa. Kwa hiyo, itakuwa ni hadhi ya juu kabisa ya uhifadhi katika nchi yetu. Kwa kweli hongereni sana.
Mheshimiwa Spika, sasa baada ya kupandisha hadhi maeneo hayo, hatua inayofuata sasa ni kuhakikisha kwamba miundombinu ya maeneo yote yale inaimarishwa, barabara zipitike wakati wote ili kusudi watalii waweze kutembelea katika yale maeneo na Serikali iweze kupata fedha nyingi zinazotokana na mapato ya utalii. Kwa hiyo, hilo litafanyika.
Swali la pili, kuhusu kuambatana naye kwenda katika maeneo hayo, naomba nimhakikishie tu kwamba mara baada ya Mkutano huu wa Bunge tutaambatana pamoja, kwa sababu tunataka kwenda kuangalia sasa baada ya kupandisha hadhi mapori yetu yote yale matano, tuone je, nini kinatakiwa kufanyika? Tufanyeje kuhakikisha kwamba utalii sasa unakua katika ile Kanda ya Magharibi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli hilo lote, tutalifanya vizuri kabisa na ninaomba tushirikiane ili tuweze kufanyakazi vizuri zaidi.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA (K.n.y. MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:- Sekta ya utalii inachangia pato kubwa la fedha za kigeni katika nchi yetu. Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara ya Serengeti ambayo ni mbovu kiasi cha kufanya watalii kukataa kupita huko?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Kutokana na swali la msingi la ubovu wa barabara ya Serengeti, Wizara ya Maliasili inaniambiaje; kwa sababu barabara zimekuwa mbovu, Hoteli ya Seronera, Lobo, Ngorongoro na Lake Manyara zilikuwa ni hoteli katika nchi hii katika Hifadhi ya Serengeti? Leo hii watalii wakienda, wanabebewa maji kwenye ndoo. Wizara inayajua hayo? Inazirudisha lini hoteli hizi Serikalini? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba tulikuwa na hoteli ambazo zilikuwa zinamilikiwa na Serikali katika miaka ya nyuma na hoteli hizi nyingi zilibinafsishwa. Kati ya hoteli 17 ambazo zilikuwa zimebinafsishwa ilionekana karibu hoteli 11 zilikuwa hazifanyi vizuri ikiwemo hizi hoteli chache ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tumeliona hilo, tumeanza kufuatilia kupitia mikataba ile ambayo walipewa ili kuhakikisha kwamba kama tumeona kwamba hawakufanya yale waliyostahili kuyafanya na uwekezaji waliotakiwa kuufanya, Serikali iweze kuzichukua hizo hoteli na kuwapa wawekezaji wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baadhi ya hoteli sasa hivi zimechukua hatua, zinaboresha huduma zao. Hili analolisema la maji, kwa kweli sasa litaendelea kupungua hasa baada ya kuanza kutekeleza miradi mbalimbali ya kuhakikisha maji yanakuwepo katika maeneo hayo. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA (K.n.y. MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:- Sekta ya utalii inachangia pato kubwa la fedha za kigeni katika nchi yetu. Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara ya Serengeti ambayo ni mbovu kiasi cha kufanya watalii kukataa kupita huko?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Katika Mkoa wetu wa Rukwa tumejaaliwa kuwa na maporomoko ya Kalambo ambayo kama Mkoa sisi tumejipanga.
Sasa napenda kujua katika Wizara ya Maliasili na Utalii mmejipangaje katika kutengeneza mazingira rafiki ili kuweza kuwavutia watalii?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba katika Mkoa wa Rukwa tunalo eneo lile la maporomoko ya Kalambo ambayo ni maporomoko ya aina yake ambayo tena ni urithi wa dunia. Kwa kweli lile eneo ni zuri sana. Baada ya kuona hivyo, mimi mwenyewe nimefika pale kuangalia mazingira yalivyo, tumechukua hatua ya kuanza kujenga ngazi kubwa ambayo inatoka kule juu kushuka kule chini ambayo ni mita karibu 230. Tunatarajia lile daraja litasaidia sana katika kuboresha na kuvutia watalii kuweza kutembelea yale maporomoko.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya pili, tumewaagiza Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kuhakikisha kwamba wanawekeza katika lile eneo; wanaweka hoteli ambayo itakuwa ndiyo kivutio kizuri cha kuwavutia watalii katika lile eneo kusudi waweze kutumia muda mrefu wa kukaa katika lile eneo. Ni tofauti na sasa hivi ambapo unakuta kwamba wenzetu wa Zambia wameweka hoteli upande wao, lakini upande wetu huduma hizi zimekuwa hazipo. Hivyo tumekuwa tukikosa watalii. Nina imani baada ya kuchukua hizi hatua, sasa watalii wataongezeka sana kwa upande wa Tanzania kwa sababu ndiyo sehemu pakee unayoweza ukaiona Kalambo vizuri kuliko maeneo mengine.

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA (K.n.y. MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:- Sekta ya utalii inachangia pato kubwa la fedha za kigeni katika nchi yetu. Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara ya Serengeti ambayo ni mbovu kiasi cha kufanya watalii kukataa kupita huko?

Supplementary Question 4

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi. Changamoto zilizopo maeneo ya Serengeti na kwingine, zinafanana kabisa na Mbuga yetu ya Katavi ambayo inakosa watalii kutokana na miundombinu mibovu.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ndani ya Mbuga ya Katavi ili kuvutia watalii?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba tunayo hifadhi kubwa ya Katavi ambayo ina wanyama wa kila aina.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa Setikali imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kwamba kwanza tunaboresha miundombinu iliyopo ndani ya ile hifadhi ili tuweze kuwavutia watalii wengi kutoka maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua nyingine ni kwa sababu ule uwanja wa Ndege wa Katavi umekuwa mzuri kabisa na tunaamini katika hizi jitihada ambazo Serikali imechukua za kuongeza ndege, basi safari za ndege zikianza kutumia uwanja ule wa Katavi basi ina maana watalii wataongezeka sana katika lile eneo na hivyo miundombinu ikiwa inapitika, watalii wengi sana wataweza kuvutiwa na kutembelea katika ile mbuga ya Katavi.