Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasmine Tiisekwa Bunga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Vyuo Vikuu

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi sana vya utalii ambavyo vikitumika vizuri vinaweza kuchangia pato la Taifa na wananchi kwa ujumla; moja kati ya vivutio hivyo ni pamoja na Mbunga za Hifadhi ya Wanyama Mikumi ambayo inaongeza mapato mengi, lakini mbuga hizo hazina hoteli nzuri za kitalii zenye kukidhi viwango vya kimataifa, kutokana na kuungua kwa Hoteli ya Kitalii ya Mikumi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga hoteli kubwa za kitalii ndani ya Mbuga ya Mikumi ili kuvutia watalii wengi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri bado kidogo ayajaniridhisha kwa sababu mimi nilitembelea Mikumi pale 2016 na majibu niliyopewa ni haya haya kwamba mwekezaji amepatikana na ukarabati unaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri anihakikishie hapa huu ukarabati utamalizika lini ili tuweze kupata mapato ya uhakikika? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kwamba mbuga hii ya Mikumi ipo katikati ya barabara ambayo inaenda mikoani na nje ya Tanzania. Kulikuwa na mpango wa kuanzisha road toll ili kuweza kupata mapato zaidi katika mbuga hii ambayo inakumbana na changamoto nyingi, miundombinu na hata magari ya kuzuia ujangili.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua, ni lini Serikali itaanzisha ushuru huu kwa sababu mchakato ulishaanza, sasa kuna kigugumizi gani? Hii itasaidia mbuga hii iweze kupata mapato na kukabiliana na changamoto ili iweze kuboresha na kuongeza mapato zaidi? Ahsante. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia na ni kweli kabisa kwamba mwaka 2016 alifika pale kuangalia ni namna gani hoteli zinaweza kuongezeka katika lile eneo ili kukabiliana na hii changamoto ya uhaba wa vyumba vya watalii kulala pale Mikumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba ni kweli kabisa kwamba yule mwekezaji alipatikana siku nyingi toka mwaka 2016, lakini baada ya kupatikana, kwa mujibu wa taratibu za uwekezaji, lazima kwanza EIA ifanyike ili aweze kuendelea na huo mradi. Huo mradi baada ya kufanya hiyo tathimini ya mazingira, imekamilika mwezi Novemba, 2017. Baada ya kukamilika, mwezi Februari, 2018 ndipo mwekezaji amekabidhiwa rasmi lile eneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukabidhiwa lile eneo, sasa hivi ametoa mpango kazi, na mimi mwenyewe nilienda pale nikaona, sasa hoteli yenyewe inategemea kukamilika mwezi Novemba mwaka ujao yaani mwaka 2019. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kuweka road toll kule Mikumi, ni kweli hili suala limekuwepo na tumekuwa tukiliangalia ndani ya Serikali kuona kama kweli linaweza likatusaidia na kama linaweza likafanya kazi. Bado tuko kwenye hatua za majadiliano na kuona namna bora ya kuweza kulitekeleza hilo ili kusudi tusilete usumbufu kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Mheshimiwa Mbunge ni zuri na ninaomba niseme kwamba Serikali bado inaendelea kulifanyia kazi.

Name

Mbarouk Salim Ali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi sana vya utalii ambavyo vikitumika vizuri vinaweza kuchangia pato la Taifa na wananchi kwa ujumla; moja kati ya vivutio hivyo ni pamoja na Mbunga za Hifadhi ya Wanyama Mikumi ambayo inaongeza mapato mengi, lakini mbuga hizo hazina hoteli nzuri za kitalii zenye kukidhi viwango vya kimataifa, kutokana na kuungua kwa Hoteli ya Kitalii ya Mikumi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga hoteli kubwa za kitalii ndani ya Mbuga ya Mikumi ili kuvutia watalii wengi?

Supplementary Question 2

MHE. MBAROUK SALIM ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu nyingi ambazo zina vivutio vya utalii utakuta miundombinu yake ni mibovu sana. Hii ndiyo sababu kubwa ambayo inasababisha wawekezaji warudi nyuma na washindwe kuwekeza katika maeneo ambayo yana vivutio na hivyo kushusha utalii.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanaboresha miundombinu katika maeneo hayo ya utalii? Nashukuru. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kumekuwa na maeneo ya namna hiyo na bado kumekuwa na changamoto ya uwekezaji. Kazi kubwa tunayoifanya kama Serikali ni kuhakikisha kwamba tunaboresha kwanza mazingira ya uwekezaji na kuwahamasisha wawekezaji ili kusudi waweze kuwekeza katika maeneo yote hayo na yaweze kuchangia katika shughuli mbalimbali za utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tu kwamba tutakaa na Mheshimiwa Mbunge ili tuone namna gani tunaweza tukafanya hiyo kazi ili kusudi wananchi wa eneo lile waweze kufaidika na matunda ya hiyo kazi.

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi sana vya utalii ambavyo vikitumika vizuri vinaweza kuchangia pato la Taifa na wananchi kwa ujumla; moja kati ya vivutio hivyo ni pamoja na Mbunga za Hifadhi ya Wanyama Mikumi ambayo inaongeza mapato mengi, lakini mbuga hizo hazina hoteli nzuri za kitalii zenye kukidhi viwango vya kimataifa, kutokana na kuungua kwa Hoteli ya Kitalii ya Mikumi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga hoteli kubwa za kitalii ndani ya Mbuga ya Mikumi ili kuvutia watalii wengi?

Supplementary Question 3

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya utalii ni sekta ambayo ina fursa nyingi sana na kubwa za kulisaidia Taifa kimapato. Suala la Mikumi kama ambavyo limejibiwa sasa hivi, tunapoteza fursa kubwa sana. Mikumi ilikuwa ni kivutio katika vivutio vya mwanzo kabisa vya utalii nchi hii. Ilikuwa inatoa fursa kubwa sana kwa utalii wa ndani hasa kwa vijana, wanafunzi na taasisi mbalimbali wanaotaka kwenda kuangalia mambo ya utalii. Jinsi ilivyo sasa hivi imekwama kwa muda mrefu na hii sawa na sehemu nyingine nyingi tu.
Je, Serikali sasa hivi iko tayari kuja na mkakati mahususi unaohakikisha kuwa sehemu zote za kitalii zinaendelezwa kwa kutumia sekta binafsi? Ahsante. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba Mikumi ilikuwa ni moja ya hifadhi ambayo ilikuwa inatoa mchango mkubwa sana katika pato la Taifa, lakini kumekuwa na changamoto ya hivi karibuni kwamba mchango ule kidogo umeshuka sana kutokana na mambo mbalimbali. Ndiyo maana kwa kutambua hilo, Serikali tumekuja na mradi mkubwa wa kuboresha utalii Kusini. Katika mradi huo, moja ya maeneo ambayo yamepewa uzito ni pamoja na hifadhi ya Mikumi, kwa sababu ule mradi wa kukuza utalii wa Kusini, tunahudumia Selous upande wa Kaskazini, Udzungwa, Mikumi na Ruaha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, katika huo mradi tunaboresha miundombinu yote, tutatangaza ipasavyo kuhakikisha kwamba tunawavutia watalii mbalimbali wa ndani na nje ya nchi ili waweze kuingiza mapato na Serikali iweze kupata mapato ya kutosha na kuweza kuendeleza nchi yetu.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi sana vya utalii ambavyo vikitumika vizuri vinaweza kuchangia pato la Taifa na wananchi kwa ujumla; moja kati ya vivutio hivyo ni pamoja na Mbunga za Hifadhi ya Wanyama Mikumi ambayo inaongeza mapato mengi, lakini mbuga hizo hazina hoteli nzuri za kitalii zenye kukidhi viwango vya kimataifa, kutokana na kuungua kwa Hoteli ya Kitalii ya Mikumi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga hoteli kubwa za kitalii ndani ya Mbuga ya Mikumi ili kuvutia watalii wengi?

Supplementary Question 4

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza Swali la nyongeza. Kama ilivyo Morogoro kwamba kuna vivutio kwa watalii ndivyo ilivyo kwa Mkoa wa Dodoma ambako Wilayani Kondoa kuna michoro ambayo haipo Tanzania na michoro ile iko katika mapango ya Kolo na Pahi, lakini vivutio vile havijawahi kutangazwa na Serikali.
Je, Serikali ina mkakati gani? Pamoja na Wabunge wa Kondoa kuhangaika kuleta watalii, lakini bado haitoshelezi kama Serikali haitatia mkazo kutangaza vile vivutio.
Je ni lini sasa au Serikali ina mkakati gani kutangaza michoro ile ya mapango ya Kolo, Pahi na maeneo mengine katika Wilaya ya Kondoa?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba nichukue nafasi hii kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Felister Bura na Wabunge wote wa Mkoa wa Dodoma kwa jinis ambavyo wamekuwa wakilifanyia kazi hili suala. Hivi sasa tunajua kabisa kwamba Dadoma ndiyo Makao Makuu ya nchi na kweli lazima tuziimarishe hizi hifadhi zetu na maeneo maengine ya Utalii ili kuweza kuvutia watu mbalimbali kuja kuwekeza katika Mkoa huu wa Dodoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho tunategemea kukifanya katika kutangaza yale maeneo ya michoro ya Miambani kule Kondoa; yaani Kolo na pale Pahi; jitihada ambazo tunaweka kuanzia tarehe 1 Julai, 2018 tunategemea kuanzisha studio ya kutangaza utalii yaani kutangaza vivutio vyote nchi nzima. Hiyo ni pamoja na hilo eneo, tutalitangaza vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, tunategemea kuanzisha channel maalum kupitia TBC ambayo itakuwa inahusiana na masuala ya utalii. Kwa kutumia hilo basi, tunaamini kwamba basi matangazo, wananchi wengi wa ndani na wa nje wataweza kupata fursa ya kuweza kujua vivutio vyote tulivyonavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, tunategemea kutumia viongozi mbalimbali mashuhuri pamoja na mambo mengine mengi kutangaza ndani ya nchi na nje ya nchi kwa kutumia mitandao ya facebook, twitter na mambo mengineyo ili kusudi vivutio vyote vieleweke kwa watanzania lakini kwa watu wote walioko nchi za nje waweze kuijua Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie nafasi hii niseme kwamba sasa hivi Tanzania tumepata taarifa kwamba sasa imekuwa ni nchi inayoongoza kwa safari Afrika kupitia Serengeti. Kwa kweli huu ni ufahari mkubwa na Dodoma nayo itafaidika sana na haya mambo ambayo tunakwenda kuyafanya.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi sana vya utalii ambavyo vikitumika vizuri vinaweza kuchangia pato la Taifa na wananchi kwa ujumla; moja kati ya vivutio hivyo ni pamoja na Mbunga za Hifadhi ya Wanyama Mikumi ambayo inaongeza mapato mengi, lakini mbuga hizo hazina hoteli nzuri za kitalii zenye kukidhi viwango vya kimataifa, kutokana na kuungua kwa Hoteli ya Kitalii ya Mikumi. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga hoteli kubwa za kitalii ndani ya Mbuga ya Mikumi ili kuvutia watalii wengi?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa naibu Spika, ahsante sana. Kuhusu Hoteli ya Kitalii ya Mikumi: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anafahamu kwamba mwekezaji wa kwanza alifanya hujuma makusudi baada ya kuchukua shilingi bilioni nne na mpaka leo akaichoma hoteli ile?
Je, Serikali imechukua hatua gani kwa yule mwekezaji wa kwanza? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli kama Serikali hatuna taarifa kama kweli ile ilichomwa kama hujuma, lakini tunachojua ni kwamba ilipata janga la moto mwaka 2009 na ikaungua yote. Yule aliyekuwa amekabidhiwa baada ya hapo, alishindwa kuendeleza. Baada ya kuona ameshindwa kuendeleza, ndiyo maana Serikali tukaamua tena kuchukua hatua kuhakikisha kwamba tunamtafuta mwekezaji mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwekezaji huyu sasa liyepatikana amekuja na michoro mizuri sana na design nzuri sana ambazo ninazo hata baaadaye Mheshimiwa Keissy naweza nikamwonyesha hapa jinsi ilivyo ambapo tunategemea itakapofika mwaka 2019 hoteli yenyewe itakuwaje? Kwa hiyo hilo tunalo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hilo la kusema kwamba alifanya hujuma, hizo taarifa hatunazo kama Serikali.