Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:- Mfumo wa ulipaji kodi za kusafirisha bidhaa kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara umekuwa ukilalamikiwa kwa muda mrefu kwamba unakwaza na kuvunja harakati za biashara Zanzibar na hivyo kusababisha uchumi wa Zanzibar kushuka:- Je, Serikali ipo tayari kuunda Kamati kwa ajili ya kushughulikia mfumo wa ulipaji kodi za mizigo kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA KOMBO HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante. Zanzibar ni Kisiwa kidogo chenye wakazi wachache sana, wakazi wa Zanzibar ni kati ya 1,000,000 mpaka 1,500,000 na kutokana na hali hiyo Zanzibar inategemea soko la bidhaa kutoka nje. Maana yake Zanzibar inategemea soko la bidhaa zinazotoka nje kusafirishwa nchi jirani au baadhi ya nchi nyingine ili kutafuta soko na ndiyo maana Zanzibar imejiandalia mfumo wake mahsusi ili kufanikisha wafanyabiashara kutoka nchi nyingine ikiwemo Tanzania Bara wafike Zanzibar wachukue bidhaa zinazotoka nje kwa ajili ya kwenda kufanya biashara sehemu nyingine.
Mheshimiwa Spika, sasa Serikali haioni kwamba kuilazimisha Zanzibar kufata mfumo wa TANCIS ndiyo maana ya kuua soko la bidhaa kutoka nje kwa pale Visiwa vya Zanzibar? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Waziri kasema haiwezekani kuunda Tume, Bunge haliwezi kuunda Tume. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, Je, Serikali kupitia Wizara ya Fedha ipo tayari kuunda Kamati Ndogo wakiwemo Wabunge, Maafisa wa TRA na yeye mwenyewe kwenda Zanzibar kukutana na wadau, wafanyabiashara wa Zanzibar hususan Taasisi ya Wafanyabishara Zanzibar ili kuangalia ukubwa wa tatizo hili na kulitafutia ufumbuzi? Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi ni kwamba hiki kinachotokea ni kuhakikisha kunakuwa na ushindani katika soko la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ndiyo maana bidhaa zinazouzwa kutoka Zanzibar zilizotoka nje kuja Tanzania Bara lazima zifanyiwe uthamini ili kuhakikisha wafanyabiashara wanaotumia Bandari za Serikali ya Jamhuri ya Tanzania Bara wanapata ushindani ulio sawia.
Mheshimiwa Spika, amesema kwamba wafanyabiashara kutoka nchi nyingine. Kumekuwa na tatizo la wafanyabiashara kutoka nchi nyingine kwenda kununua bidhaa Zanzibar na kuja kuzi-dump katika soko la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ndiyo maana kwa sababu bidhaa zile hazijazalishwa Zanzibar lazima zinapoingia Tanzania Bara ziweze kulipa kodi husika ili ushindani huo uweze kuwepo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, napenda kumwambia Mheshimiwa Kombo kwamba nimesema kwenye jibu langu la msingi Serikali zetu mbili, Serikali ya Zanzibar pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinalifanyia kazi tatizo hili na tuna uhakika kwamba changamoto hii itafika mwisho, kwa sababu majadiliano yamefika sehemu nzuri na tuna imani kubwa kwamba changamoto hii itafika mwisho sasa.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:- Mfumo wa ulipaji kodi za kusafirisha bidhaa kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara umekuwa ukilalamikiwa kwa muda mrefu kwamba unakwaza na kuvunja harakati za biashara Zanzibar na hivyo kusababisha uchumi wa Zanzibar kushuka:- Je, Serikali ipo tayari kuunda Kamati kwa ajili ya kushughulikia mfumo wa ulipaji kodi za mizigo kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara?

Supplementary Question 2


MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona. Ni lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria Bungeni ili umeme unaonunuliwa Tanzania Bara kwenda Zanzibar uweze kupatiwa msamaha wa kodi kama ilivyo bidhaa nyingine zinazozalishwa Tanzania Bara kwenda Zanzibar? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, wakati tunapitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati, Waziri wa Nishati alisema vizuri kabisa kuhusu jambo hili, kwamba nalo ni katika mambo ambayo yapo katika mijadala kuhakikisha kwamba kodi inayotozwa kwa umeme unaouzwa Zanzibar inafanyiwa kazi. Nimwombe Mheshimiwa Khadija Nassir pamoja na Wazanzibari wote na Watanzania wote jambo hili litafanyiwa kazi kwa muda muafaka kabisa.