Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU (K.n.y. MHE. MUSSA R. NTIMIZI) aliuliza:- Barabara ya Buhekela-Miswaki-Loya-Iyumbu inaunganisha Majimbo ya Igunga, Manonga, Igagula na Singida Magharibi, pia inaunganisha Mikoa miwili ya Tabora na Singida, ina Mbuga kubwa ya Wembele ambapo wananchi wanalima mpunga na kulisha Mikoa ya Tabora, Shinyanga na Singida lakini ni mbovu sana:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuitengeneza barabara hiyo kwa umuhimu wake huo wa kiuchumi na kimawasiliano?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Spika, nakushuru. Swali la kwanza, kwa kuwa barabara hii ya Buhekela-Miswaki-Loya mpaka Iyumbu na ile barabara ya Igunga-Itumba-Simbo ni barabara ambazo zinapita kwenye Mbuga ya Wembele mahali ambapo ni lazima ujenge tuta kubwa ili barabara iwezekane siyo kuchonga, kwa hiyo, kuna madaraja mengi yanahitajika kujengwa.
Mheshimiwa Spika, Sh.225,000,000 za barabara ya Iyumbu na zile Sh.297,000,000 za barabara ya Itumba hazitoshi kabisa kuzijenga barabara hizi. Waziri anatoa commitment gani kuhusu kuongeza bajeti ili kujenga hii barabara kwa kiwango ambacho zitaweza kupitika wakati wowote?
Swali la pili, kwa kuwa ile barabara ya Igunga-Itumba- Loya kipande cha Itumba - Loya hakina fedha, kwa sababu inaenda Simbo kwanza. Ni lini basi Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kile kipande cha Itumba-Loya? Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli swali hili amekuwa akiuliza sana kuhusu kipande hicho cha Mbuga ya Wembele ambayo inahitaji special consideration na ni ukweli usiopingika kwamba inahitaji bajeti kubwa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama Serikali tunalitambua hili, lakini kinachogomba ni suala la bajeti, pale hali itakavyokuwa imeimarika hatutasahau kwa sababu eneo lile linahitaji pesa nyingi. Naamini katika bajeti zijazo, kabla hatujafika 2020 tutakuwa tumeshaikamilisha. (Makofi)

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU (K.n.y. MHE. MUSSA R. NTIMIZI) aliuliza:- Barabara ya Buhekela-Miswaki-Loya-Iyumbu inaunganisha Majimbo ya Igunga, Manonga, Igagula na Singida Magharibi, pia inaunganisha Mikoa miwili ya Tabora na Singida, ina Mbuga kubwa ya Wembele ambapo wananchi wanalima mpunga na kulisha Mikoa ya Tabora, Shinyanga na Singida lakini ni mbovu sana:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuitengeneza barabara hiyo kwa umuhimu wake huo wa kiuchumi na kimawasiliano?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Vigwaza - Kwala - Kimaramasale inayounganisha Majimbo matatu ya Mkoa wa Pwani, Jimbo la Bagamoyo, Kibaha Vijiji na Kisarawe, ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ikizingatiwa kule kuna bandari kavu? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na nimshukuru Mheshimiwa Hawa Mchafu kwa swali lake.
Mheshimiwa Spika, niseme tu barabara hii inahudumiwa na TANROADS na katika ule mpango mkakati wetu tunao utaratibu wa kuitengeneza. Kwa sasa tunajitahidi kuhakikisha barabara hii inapitika wakati wote na kwa umuhimu wa kipekee kwa sababu ya kuwa na hii bandari kavu tutaipeleka kwenye kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge avumilie kidogo utaratibu upo wa kuifanya hii barabara iwe nzuri zaidi. Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU (K.n.y. MHE. MUSSA R. NTIMIZI) aliuliza:- Barabara ya Buhekela-Miswaki-Loya-Iyumbu inaunganisha Majimbo ya Igunga, Manonga, Igagula na Singida Magharibi, pia inaunganisha Mikoa miwili ya Tabora na Singida, ina Mbuga kubwa ya Wembele ambapo wananchi wanalima mpunga na kulisha Mikoa ya Tabora, Shinyanga na Singida lakini ni mbovu sana:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuitengeneza barabara hiyo kwa umuhimu wake huo wa kiuchumi na kimawasiliano?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nami nina swali dogo la nyongeza. Tatizo lililopo katika Jimbo la Igalula lipo vilevile katika Jimbo la Momba hususan katika barabara ya kutoka Kakozi-Kapele - Ilonga ambako ni Jimbo la Mheshimiwa Naibu Waziri, Mheshimiwa Kandege, Jimbo la Kalambo.
Mheshimiwa Spika, wakati tunasubiri ahadi ya TANROADS ya kutengeneza barabara hiyo na yeye sasa hivi ndiye Waziri, haoni sasa ni wakati muafaka kutengeneza barabara hiyo ambayo inaunganisha mikoa miwili ya Songwe pamoja na Mkoa wa Rukwa, lakini vilevile Jimbo la Momba na Jimbo lake la Kalambo? (Makofi). Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nataka nimwombe Mheshimiwa Silinde tu avumilie kwa sababu sijatembelea Mkoa wa Songwe, lakini utaratibu wa Serikali kisera ni kwamba umuhimu wa kwanza ni kuhakikisha tunaunganisha mikoa. Kwa hiyo, asiwe na wasiwasi na katika bajeti yetu tuna provision na nikienda kule tutazungumza kwa upana zaidi ili aone namna ambavyo tumejipanga kuijenga barabara hii Mheshimiwa. Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)