Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:- Kabla ya kuanzishwa Shule za Kata, kulikuwa na mpango wa kujenga shule katika tarafa. Kwenye Jimbo la Ulyankulu kulijengwa shule tatu ambazo ni Kashishi, Ulyankulu na Mkindo; Shule ya Kashishi hivi sasa ina kidato cha tano na sita:- Je, ni lini Shule za Mkindo na Ulyankulu zitapewa hadhi ya kuwa na kidato cha tano na sita ili kuwapunguzia wanafunzi gharama za kufuata mbali masomo ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Kwa vile Naibu Waziri ameona aondoe sentensi moja, mimi nasema paragraph yote majibu hayafanani na swali nililouliza. Mimi sitaki kuuliza maswali mengi, nimwombe tu Mheshimiwa Naibu Waziri au Mawaziri wote watatu wa TAMISEMI wafike Ulyankulu kujionea haya yaliyoandikwa, je ni kweli? Kwa sababu haya yote yaliyoandikwa si kweli.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nimwombe Naibu Waziri au wenzake waweze kufika Ulyankulu na kujionea kile wanachopewa na wataalam na je, ndicho kilichoko site? Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, naomba sana nimwombe Mheshimiwa John Kadutu, awepo Jimboni tarehe 10 Julai, ili tuweze kutembelea shule hizo kwa pamoja.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:- Kabla ya kuanzishwa Shule za Kata, kulikuwa na mpango wa kujenga shule katika tarafa. Kwenye Jimbo la Ulyankulu kulijengwa shule tatu ambazo ni Kashishi, Ulyankulu na Mkindo; Shule ya Kashishi hivi sasa ina kidato cha tano na sita:- Je, ni lini Shule za Mkindo na Ulyankulu zitapewa hadhi ya kuwa na kidato cha tano na sita ili kuwapunguzia wanafunzi gharama za kufuata mbali masomo ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, shule za sekondari za kidato cha kwanza mpaka cha nne Serikali imezipandisha hadhi baadhi yake kuwa shule za kidato cha tano na cha sita, kwa mfano, Kibakwe, Berege, Mazae na Kongwa Mjini. Hata hivyo, watoto katika shule hizi wanasoma katika mazingira magumu sana kwanza madarasa, hosteli pamoja na mabweni lakini hata chakula wanachopewa hela ni kidogo sana. Mheshimiwa Naibu Waziri anasemaje kuhusu suala la kuboresha shule za form five na six katika kata hizi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nichukue nafasi hii kumpongeza, yeye ni Mbunge mzoefu wa siku nyingi na kutokana na Ubunge wake ndiyo maana ameweza kupata maendeleo makubwa katika Jimbo lake hadi shule hizo alizozitaja zimesajiliwa kuwa katika hadhi ya kidato cha tano na sita. Kuwa na shule tatu au nne kwenye Jimbo moja za kidato cha tano na sita siyo kazi ndogo, ni kazi kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, katika jibu hili, napenda kujibu kwa ujumla kwamba shule zote za kidato cha tano na sita na hata za kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, zote zinapewa fedha sawasawa kwa nchi nzima. Kwa hiyo, haiwezekani kwa mfano tukasema kwamba, kwa sababu shule hizi sasa Mheshimiwa Mbunge amesema zina matatizo makubwa, basi tuziongezee shule zile za Jimbo lake tu, ni kitu ambacho hakiwezekani. Kwa hiyo, nakaribisha maoni kama haya ili tuweze kuyajadili kwa pamoja kwa ajili ya shule zote nchini badala ya shule moja moja. Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:- Kabla ya kuanzishwa Shule za Kata, kulikuwa na mpango wa kujenga shule katika tarafa. Kwenye Jimbo la Ulyankulu kulijengwa shule tatu ambazo ni Kashishi, Ulyankulu na Mkindo; Shule ya Kashishi hivi sasa ina kidato cha tano na sita:- Je, ni lini Shule za Mkindo na Ulyankulu zitapewa hadhi ya kuwa na kidato cha tano na sita ili kuwapunguzia wanafunzi gharama za kufuata mbali masomo ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 3

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa swali la msingi la Ulyankulu liko katika Majimbo mengi ya nchi hii, kutokuwa na shule za form five na form six. Serikali inatoa commitment gani na lini itaanza kufanya operation katika kila jimbo kupata shule za form five na form six? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, maombi yaliyopo katika Wizara yetu ambayo sisi tukiyapokea tunayapeleka Wizara ya Elimu kwa ajili ya usajili kwa sababu anayesajili ni Wizara ya Elimu ni mengi, lakini mengi yamekuja hivi karibuni, mwezi wa Nne mwishoni, mwezi wa Tano wakati tayari masuala ya bajeti yalikuwa yameshakamilika. Kwa hiyo, naomba sana nimwahidi Mheshimiwa Bulembo pamoja na Waheshimiwa Wabunge wote na Bunge zima kwamba mwakani tutaweka utaratibu maalum wa kuhakikisha kwamba inavyofika Desemba, 2018, basi shule zote ambazo zina maombi maalum katika ofisi zetu za Serikali tutazisimamia ili ziweze kupata usajili.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimesimama kulihakikishia Bunge lako Tukufu Wizara yangu ambayo ndiyo ina jukumu la kusajili shule haina tatizo lolote la kusajili wakati wowote shule ambayo imekidhi vigezo. Kwa hiyo, nitoe wito kwa Waheshimiwa Wabunge na Wakurugenzi na Maafisa Elimu kwa ujumla kama kuna shule ambayo inahitaji usajili, tunasajili wakati wowote ilmradi shule imekidhi vigezo. (Makofi)