Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano katika Kata za Mpanda, Mpangatuzara, Ihanu na Ikweha?

Supplementary Question 1

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yenye kutia moyo lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa kuna minara imejengwa katika Kata ya Mapanda, Kijiji cha Mapanda na Kata ya Ikweha Kijiji cha Ikweha, lakini mpaka nauliza swali hili hakuna mawasiliano na Mheshimiwa Mahmoud Hassan Mgimwa ameonana na Mheshimiwa Waziri wa Mawasiliano. Je, ni lini watapata mawasiliano katika kata hizo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri baada ya Bunge hili yuko tayari kwenda katika Kata ya Mapanda, Ikweha, Mpangatazara, Ihanu kujionea mwenyewe matatizo ya mawasiliano yanayowapata wananchi wa maeneo hayo? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Khadija, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba kuna baadhi ya minara ambayo imewekwa lakini haijaanza kutoa mawasiliano kutokana na sababu mbalimbali. Sababu ya kwanza inaweza ikawa kutokuwepo umeme eneo hilo na wakategemea kutumia solar ambapo kama kunatokea hali ya mawingu, basi zile solar haziwezei kupeleka umeme wa kutosha kwenye minara na hivyo kusababisha wananchi kutokuwa na mawasiliano. Sababu nyingine ni za kijiografia. Hivyo, nawaelekeza Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote watembelee eneo alilolitaja Mbunge kuhakikisha kwamba wanatambua chanzo cha sababu ya minara hiyo kuwepo lakini haitoi mawasiliano. Nami nitafutilia kuhakikisha kwamba minara yote ambayo imewekwa na haina mawasiliano basi inaanza kupeleka mawaliano kwa wananchi kwa kuwa ndiyo lengo kuu la Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, niko tayari baada ya Bunge hili na nimeshaahidi hata Wabunge wengine kwamba nitafanya ziara ya miezi miwili na timu yangu ya watu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote kuhakikisha tunatambua maeneo yote ambayo hayana mawasiliano tuweze kuyapatia mawasiliano. (Makofi)

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano katika Kata za Mpanda, Mpangatuzara, Ihanu na Ikweha?

Supplementary Question 2

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kweli Wilaya ya Mufindi tuna tatizo kubwa sana la mawasiliano na Mheshimiwa Naibu Waziri amesema ni kutokana na jiografia ilivyo. Vijiji vya Idete, Kasanga, Ihowanza, ni sehemu kubwa sana hawana mawasiliano kabisa na amesema kwamba atakuja na timu yake, je, yuko tayari sasa timu hiyo iende ikafanye survey kwenye vijiji hivi ili wananchi wale waweze kupewa mawasiliano?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Kigola, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kifupi, niko tayari kwenda naye kuangalia maeneo hayo. Ahsante.

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano katika Kata za Mpanda, Mpangatuzara, Ihanu na Ikweha?

Supplementary Question 3

MHE MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu la Serengeti, Kata za Ikoma hususani ndani ya hifadhi maeneo ya Robo, Kata za Sedeko, Nyansurura na Nyambureti, hakuna mawaliano ya simu. Mheshimiwa Naibu Waziri anasema nini kuhusu kupeleka minara katika maeneo hayo?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe maelezo kwa ujumla tu kwamba tunayo changamoto kwenye maeneo ambayo yanapakana na Hifadhi ya Taifa na tuko kwenye mawasiliano mazuri sana na Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo yako kwenye hifadhi tunaweka minara kwa mapatano maalum. Tunapata changamoto kwa sababu wanaohudumia ile minara hatuwezi kuwa na control nao ya moja kwa moja. Tunajipanga kuhakikisha kwamba tunakuwa na control nao ya moja kwa moja ili hata mnara unapowekwa kwenye hifadhi, basi usalama wa hifadhi zetu unaendelea kuzingatiwa lakini wakati huo huo wananchi wanapata huduma ya mawasiliano bila kukwamishwa. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano katika Kata za Mpanda, Mpangatuzara, Ihanu na Ikweha?

Supplementary Question 4

MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya mpya ya Songwe maeneo ya Rukwa, Udinde, Guwa na Some hayana kabisa mawasiliano. Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza akanihakikishia ni lini Serikali itaweka mawasiiano katika kata hizo?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la ndugu yangu Mheshimiwa Mulugo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza natoa shukurani za dhati kwa Mheshimiwa Mulugo kwa jinsi ambavyo anapambana kwa ajili ya Jimbo lake na wananchi wa eneo lake. Nashukuru vilevile kwa kuwa ameshaniletea barua ya maombi ya kuimarisha masuala ya mawasiliano kwenye maeneo aliyoyataja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mulugo kwamba tutafanya ziara baada ya Bunge hili kuhakikisha maeneo yake na maeneo mengine yote ambako Waheshimiwa Wabunge wameandika barua kuomba mawasiliano tunayatembelea na kuhakikisha tunaingiza kwenye bajeti ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ambao tutaanza kuutekeleza kuanzia mwezi Septemba, 2018. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano katika Kata za Mpanda, Mpangatuzara, Ihanu na Ikweha?

Supplementary Question 5

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Kata ya Mchauru, Kata ya Sindano na maeneo ya Njawara na Ntona yako mpakani mwa Tanzania na Msumbiji na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ulithibitisha kwamba pembezoni au kwenye mipaka ya nchi yetu watahakikisha minara inajengwa. Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atahakikisha kwamba wananchi wale wanapatiwa mawasiliano? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Bwanausi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Bwanausi kwamba kati ya Waheshimiwa Wabunge walioleta barua zao mwanzoni kabisa kuhusu masuala ya mawasiliano alikuwa ni yeye. Namshukuru Mungu vilevile kwamba tumeendelea kupokea barua kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge wengine wanaoeleza changamoto ya mawasiliano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Bwanausi na wananchi wa Jimbo lake kwamba tutafanya ziara pale, tutaainisha maeneo ambayo tunaweza tukaweka minara kwa sababu siyo lazima ukiomba minara mitano uwekewe mitano. Unaweza ukaomba minara mitano, ukawekewa miwili na ikaweza ku-cover eneo kubwa sana; lakini unaweza ukaomba minara mitatu ukawekewa hata mitano kutokana na jiografia. Ndiyo maana naeleza kwamba ni lazima twende tukajiridhishe tukiwa na timu ya wataalam kuhakikisha kwamba tunaweka mawasiliano ambayo yatahakikisha yanawafaidisha wananchi kwa ujumla wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya mipakani vilevile kuna programu maalum ambapo tunashirikiana Mfuko wa Mawasiliano na TCRA kuhakikisha mawasiliano yanayohusu Watanzania yanabaki kuwa ya Watanzania na yanayohusu nchi nyingine yanaendelea kuwahusu wao.