Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Edward Franz Mwalongo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Njombe Mjini
Primary Question
MHE. EDWARD F. MWALONGO - (K.n.y. MHE. DEO K. SANGA) aliuliza:- Mji wa Makambako unakabiliwa na tatizo kubwa la maji kutokana na ongezeko la watu na Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni aliahidi kuanza kwa ujenzi wa mradi wa maji na kazi ya usanifu wa mradi huo imeshafanyika:- Je, ni lini sasa ujenzi wa mradi huo wa maji utaanza?
Supplementary Question 1
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza. Utaratibu wa Serikali wa kutekeleza miradi ya maji ni ule ambao unamtaka Mkandarasi atekeleze alete madai na aweze kulipwa. Lakini utaratibu huu umeonesha kwamba Wakandarasi wengi hawana uwezo matokeo yake miradi mingi inachelewa sana kutekelezwa na mingine inaharibika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha utaratibu wa utekelezaji wa miradi wa maji inayoanza kuanzia tarehe 1 mwezi wa 7 ukiwemo huu mradi wa maji wa Makambako?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, mkopo nafuu kutoka Serikali ya India unahusu pia vilevile Mji wa Njombe ambao upembuzi yakinifu umefanyika kwa ajili ya kupata maji kutoka chanzo cha Mto Hagafilo na kusambaza katika Mji wa Njombe na sasa huu ni mwaka wa tatu, kila mwaka Serikali inatuambia kwamba mradi huu unaanza. Je, Serikali inatoa majibu gani ya uhakika sasa kuwahakikishia wananchi wa Mji wa Njombe kwamba mradi huu wa maji kutoka Mji wa Hagafilo unaanza kutelekezwa? Mheshimiwa Spika, ahsante.
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, pamoja na nia njema ya Wizara yetu ya Maji katika kuhakikisha Watanzania wanapata maji safi, salama na yenye kutosheleza, lakini imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo la Wakandarasi.
Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuona haja sasa Wahandisi wote wa maji kutoka Halmashauri waje kuweka katika Wizara yetu ya Maji ili tuwe na usimamizi wa ukaribu na majukumu ya pamoja katika kuhakikisha tunatatua matatizo hayo. Kwa hiyo, mkakati wa Serikali ni kuanzisha sasa Wakala wa Maji Vijijini katika kuhakikisha Watanzania waliokupo vijijini wanafikiwa na asilimia 85 ya upatikanaji wa maji.
Mheshimiwa Spika, pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha, kama nilivyomhakikishia kwamba tumeshasaini mkataba ule wa kupata fedha, niwahakikishie wananchi wa Njombe kwamba watapata maji hayo safi, salama na yenye kuwatosheleza. Sisi kama viongozi wa Wizara tutasimamia kwa ukaribu ili wananchi wake waweze kupata maji safi, salama na yenye kutosheleza.
Name
Goodluck Asaph Mlinga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ulanga
Primary Question
MHE. EDWARD F. MWALONGO - (K.n.y. MHE. DEO K. SANGA) aliuliza:- Mji wa Makambako unakabiliwa na tatizo kubwa la maji kutokana na ongezeko la watu na Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni aliahidi kuanza kwa ujenzi wa mradi wa maji na kazi ya usanifu wa mradi huo imeshafanyika:- Je, ni lini sasa ujenzi wa mradi huo wa maji utaanza?
Supplementary Question 2
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika Jimbo langu la Ulanga Kijiji cha Gombe kuna mradi mmoja mradi wa kiinimacho. Mawaziri wote anapokuja Waziri maji yanajazwa kwenye tanki usiku kucha, akija Waziri asubuhi anakuta yanatoka. Kaja Waziri kafanyiwa hivyo hivyo, kaja Naibu Waziri kafanyiwa hivyo hivyo. Sasa Mheshimiwa Waziri anatoa kauli gani kuhusiana na mradi huu kiini macho ambao unafanya wananchi wanashindwa kupata maji?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, nilifanya ziara katika Jimbo la Ulanga na tumefika katika eneo lile tumeona hali ya utekelezaji na moja ya majukumu nilichukua hatua ya kuhakikisha yule Mkandarasi anakamatwa kwa sababu ya kusuasua kwa utekelezaji wa mradi ule. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge nipo tayari kukutana naye leo baada ya saa saba tuangalie wapi walikofikia ili mwisho wa siku na sisi tuendelee kuongeza nguvu wananchi wake waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
Name
Philipo Augustino Mulugo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Songwe
Primary Question
MHE. EDWARD F. MWALONGO - (K.n.y. MHE. DEO K. SANGA) aliuliza:- Mji wa Makambako unakabiliwa na tatizo kubwa la maji kutokana na ongezeko la watu na Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni aliahidi kuanza kwa ujenzi wa mradi wa maji na kazi ya usanifu wa mradi huo imeshafanyika:- Je, ni lini sasa ujenzi wa mradi huo wa maji utaanza?
Supplementary Question 3
MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, kwa kweli nashukuru sana kwa kuniona maana yake nikasema mbona ni mrefu kuliko wote lakini nimesimama mara 20. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, nataka kumuuliza swali moja la nyongeza Mheshimiwa Naibu Waziri. Nakumbuka mwezi Machi alikuja Songwe Wilaya mpya tulikuwa naye kwenye Kata ya Chang’ombe, Kijiji cha Chang’ombe na Mbuyuni na yeye mwenyewe aliona ufisadi wa maji katika mradi wa Chang’ombe uliokuwa unashikiliwa na Mkurugenzi Chunya na sasa ni Wilaya Mpya na aliniahidi kwamba atafuatilia kumrudisha yule Mkandarasi aje amalizie ule mradi wa maji Chang’ombe, lakini mpaka leo kimya. Nini kauli ya Serikali?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, ni kweli nilishafika katika Halmashauri ya Songwe na tumeona changamoto hiyo na nilikwishatoa maagizo kwa Mhandisi wa Maji katika suala zima la kusimamia. Nimwombe Mhandisi wa Maji wa Songwe asimamie maagizo ambayo niliyompa na kama ameshindwa basi ajitathmini, kwa sababu sisi tunachotaka ni kazi na wananchi wale waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved