Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Uanzishaji wa Vyuo vya Ufundi ulilenga kuwapatia elimu ya vitendo hasa vijana wetu, lakini Chuo cha Ufundi Kibaha kilicho chini ya Shirika la Elimu Kibaha hakina vifaa wala miundombinu ya kujifunzia:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka vifaa pamoja na kufufua miundombinu katika chuo hicho?

Supplementary Question 1


MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Amekiri kwamba kuna matatizo lakini swali langu la kwanza linasema, kama hivyo ndivyo, wanafunzi wamemaliza wakiwa hawana ufundi wowote, kwa sababu kile chuo kilikuwa cha madarasa kwa ajili ya vijana wetu na kilikuwa kinafundisha udereva hamna magari, karakana hamna, madarasa mabovu na wameondoka wakiwa hawana ujuzi wowote na intake yao imekwisha. Je, Serikali ina mpango gani kwa ajili ya vijana hao, baada ya kurekebisha upungufu huo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa hakuna vifaa vya kufundishia miundombinu hakuna na bado intake hii wanachukua wanafunzi, nini kauli ya Serikali katika hilo?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba pamoja na upungufu uliopo katika Chuo cha FDC Kibaha, elimu iliyokuwa inatolewa inakidhi viwango stahiki vya ufundi ambao Chuo kile kimesajiliwa kwa ajili ya kutoa. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba wale vijana waliomaliza Serikali imejiridhisha kwamba wamekuwa wakipata mafunzo vinginevyo chuo kile kingeshafungwa.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili kwamba ni namna gani sasa tunarekebisha hiyo hali, nimeshamjibu kwenye jibu letu la msingi kwamba tayari tupo kazini, tunafanya tathmini ili kuweza kujua upungufu uliopo katika vyuo vyote 50 vya FDC ili sasa tuanze utaratibu wa kukarabati, na kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia na kufundishia ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba kuna nguvukazi ya kutosha ili elimu inayotolewa iweze kuwa bora kuliko sasa. Kwa hiyo, nimwambie tu asubiri tayari zoezi linaendelea.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Uanzishaji wa Vyuo vya Ufundi ulilenga kuwapatia elimu ya vitendo hasa vijana wetu, lakini Chuo cha Ufundi Kibaha kilicho chini ya Shirika la Elimu Kibaha hakina vifaa wala miundombinu ya kujifunzia:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka vifaa pamoja na kufufua miundombinu katika chuo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa nami kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Chuo cha Ufundi VETA, Dodoma kilijengwa muda mrefu na kilikidhi kwa wakati ule na sasa hivi kuna ongezeko kubwa sana la vijana na miundombinu bado ni ile ile; je, Serikali haioni kwamba umefikia wakati wa kuongeza majengo na miundombinu ili kiendane na hadhi ya Jiji? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali ina mpango wa kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji katika vyuo vyote nchini, na sio Vyuo vya Ufundi tu. Kwa hiyo, tutaendelea kuangalia vyuo vile ambavyo vinahitaji matengenezo na ukarabati pamoja na kuongezewa Majengo, ili tuweze kufanya hivyo kadiri bajeti itakavyoturuhusu.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie tu kwamba, hata Chuo cha Dodoma nacho ni moja kati ya vyuo tulivyonavyo na kwa vyovyote vile kulingana na upatikanaji wa fedha tutaangalia uwezekano wa kukipanua.

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Uanzishaji wa Vyuo vya Ufundi ulilenga kuwapatia elimu ya vitendo hasa vijana wetu, lakini Chuo cha Ufundi Kibaha kilicho chini ya Shirika la Elimu Kibaha hakina vifaa wala miundombinu ya kujifunzia:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka vifaa pamoja na kufufua miundombinu katika chuo hicho?

Supplementary Question 3

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Moja ya Malengo ya Umoja wa Mataifa ni kuhakikisha kwamba hakuna anayeachwa nyuma na katika vyuo vingi hasa vya Ufundi, havizingatii mahitaji ya kundi maalum la watu wenye ulemavu na hivyo wamekuwa wakiachwa nyuma. Ni nini sasa, jitihada za Serikali katika kuhakikisha kwamba ili tunaendana sambamba na kauli hizo za Umoja wa Mataifa, watu wenye ulemavu hawaachwi nyuma?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Amina Mollel, kwa kweli amekuwa ni mtetezi mkubwa sana wa haki za watu wenye mahitaji maalum. Nimhakikishie tu kwamba, Wizara yangu imejipanga vizuri kuhakikisha kwamba changamoto ambazo zilikuwepo huko nyuma za kutotoa msisitizo mkubwa kwenye mahitaji maalum ya watu wenye ulemavu, kwa sasa tunahakikisha tunajaribu kutoa kipaumbele.
Mheshimiwa Spika, kwa kuanzia Wizara ya Elimu ina Kitengo Maalum kinachohusika na elimu ya mahitaji maalum. Vilevile kwa sasa tumetoa maelekezo kwamba katika ujenzi wowote ule utakaofanywa kwa fedha za Serikali ni lazima tuhakikishe kwamba mahitaji na mazingira ya watu wenye mahitaji maalum yanatiliwa maanani.
Mheshimiwa Spika, ukiacha hivyo, Serikali imewekeza sasa vilevile kwenye kutafuta Walimu na Wataalam wengine kwa ajili ya kuendeleza elimu ya watu wenye mahitaji maalum. Ndio maana tumefanya ukarabati mkubwa sana katika Chuo cha Patandi na tunaamini kwamba tunavyoendelea mbele, tutaendelea kuhakikisha kwamba kunakuwa na Walimu na wafanyakazi wengine ambao wana elimu ya kuweza kusaidia wanafunzi na watoto wenye mahitaji maalum. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba Serikali inayafanyia kazi vizuri sana.