Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Barabara ya Ubena, Ngerengere hadi Mvuha ina urefu wa zaidi ya kilometa 70 na inaunganisha Wilaya ya Bagamoyo na Halmashauri ya Morogoro ambako Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Mvuha yanatarajiwa kujengwa. Aidha, barabara hii inaunganisha Mkoa wa Pwani na Morogoro. Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina uwezo wa kuhudumia barabara hiyo:- (a) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la kupandisha barabara hiyo kuwa ya Mkoa? (b) Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hiyo ya Ubena – Mvuha kwa kiwango cha changarawe ili ipitike mwaka mzima?

Supplementary Question 1

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa umbali wa kutokea Ubena Zomozi mpaka Ngerengere ni kilomita 18 na kati ya hizo kilomita 11 zimetengewa kujengwa kwa kiwango cha lami katika Bajeti ya 2018/2019 na zimebaki kilomita saba tu; na kwa kuwa barabara hiyo inaunganisha majeshi yetu mawili kati ya Kizuka mpaka Sangasanga. Je, Serikali haioni umuhimu wa kumalizia hizo kilomita saba kwa kiwango cha lami ili barabara hii ifike Ngerengere Mjini na kule kwenye Kambi yetu ya Jeshi ya Sangasanga?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; ahadi kama hii ilitolewa na Rais wa Awamu ya Nne tangu 2010 na Rais wa Awamu ya Tano 2015 katika barabara ya Bigwa – Mvuha kujengwa kwa kiwango cha lami; na kwa kuwa barabara hii iko kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishamalizika muda mrefu. Ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami ukizingatia tumebakiza miaka miwili kwenda kwenye uchaguzi? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kipande cha barabara kati ya Ubena hadi Kizuka chenye urefu wa kilometa 11 kimewekewa lami na kipande cha kilometa saba kati ya Kizuka mpaka Ngerengere bado ni cha vumbi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mgumba ambaye kwa kweli Mheshimiwa Mwenyekiti nikiri kwamba ni Mbunge ambaye anafuatilia sana suala la barabara hii kwamba tunafahamu umuhimu na unyeti wa kipande cha barabara kutoka Kizuka kwenda Ngerengere cha kilometa saba, lakini vilevile kutoka Ngerengere kwenda Sangasanga cha kilometa sita na kipande cha kutoka Sangasanga kwenda Mdaula, tunajua umuhimu wa eneo hilo na unyeti wa eneo hilo. Namuomba Mheshimiwa Mbunge tutakapotoka hapa twende Wizarani tukamwoneshe taratibu na hatua ambazo tumekwishafikia kuhakikisha kipande hicho chote ambacho kina mzunguko kinawekewa lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili; ni kweli kwamba kuna ahadi mbalimbali zilishatolewa na viongozi wetu wakuu kuweka barabara kwa kiwango cha lami kutoka Bigwa kuja Mvuha mpaka Kisaki. Nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba mipango ipo, bahati nzuri upembuzi yakinifu ulishafanyika na usanifu wa kina tayari, kinachosubiriwa sasa ni upatikanaji wa pesa ili tuweze kutangaza tender, kumpata mkandarasi wa kujenga kwa kiwango cha lami. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Barabara ya Ubena, Ngerengere hadi Mvuha ina urefu wa zaidi ya kilometa 70 na inaunganisha Wilaya ya Bagamoyo na Halmashauri ya Morogoro ambako Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Mvuha yanatarajiwa kujengwa. Aidha, barabara hii inaunganisha Mkoa wa Pwani na Morogoro. Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina uwezo wa kuhudumia barabara hiyo:- (a) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la kupandisha barabara hiyo kuwa ya Mkoa? (b) Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hiyo ya Ubena – Mvuha kwa kiwango cha changarawe ili ipitike mwaka mzima?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kuna utaratibu wa kuunganisha wilaya kwa wilaya. Wilaya ya Bukoba Vijijini inapakana na Wilaya ya Misenyi kutoka katika Kijiji cha Msira kwenda katika Kijiji cha Bulembo, pale katikati kuna mto na watu wanaoishi pale wengi ni wakulima wa zao la kahawa. Je, ni lini Serikali itaamua kuunganisha vijiji hivi kwa kujenga barabara ili kuwarahisishia wakulima hawa wa zao la kahawa usafiri wa uhakika?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunafahamu umuhimu wa kuunganisha wilaya kwa wilaya kwa kiwango cha lami na nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mipango ipo kwa ajili ya kuunganisha Wilaya ya Bukoba Vijijini na Misenyi na taratibu mbalimbali za kiuhandisi zimeshaanza kuhakikisha kwamba kiwango hicho kinawekwa hivi karibuni pesa zitakapopatikana.

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Barabara ya Ubena, Ngerengere hadi Mvuha ina urefu wa zaidi ya kilometa 70 na inaunganisha Wilaya ya Bagamoyo na Halmashauri ya Morogoro ambako Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Mvuha yanatarajiwa kujengwa. Aidha, barabara hii inaunganisha Mkoa wa Pwani na Morogoro. Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina uwezo wa kuhudumia barabara hiyo:- (a) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la kupandisha barabara hiyo kuwa ya Mkoa? (b) Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hiyo ya Ubena – Mvuha kwa kiwango cha changarawe ili ipitike mwaka mzima?

Supplementary Question 3

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kuna barabara ya kutoka Nyororo mpaka Mtwango kilimeta 40, barabara ya kutoka Mafinga mpaka Mgololo kilometa 84 na upembuzi yakinifu Serikali ilishafanya miaka miwili iliyopita. Sasa ni lini itaanza kujenga ile barabara kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kigola kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina nia na lengo la kuunganisha kwanza mikoa kwa kiwango cha lami. Hatua zitakazofuata baada ya kuunganisha mikoa yote kwa kiwango cha lami, tutaunganisha wilaya zote kwa kiwango cha lami. Namwomba sana Mheshimiwa Mbunge awe na subira, tunafahamu suala lake na siyo la kwake peke yake, wilaya nyingi sana Tanzania hazijaunganishwa kwa kiwango cha lami. Tutakapofikia mahali pa kuunganisha kwa kiwango cha lami wilaya zote tutafahamishana na tutaanza taratibu hizo mara moja. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Barabara ya Ubena, Ngerengere hadi Mvuha ina urefu wa zaidi ya kilometa 70 na inaunganisha Wilaya ya Bagamoyo na Halmashauri ya Morogoro ambako Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Mvuha yanatarajiwa kujengwa. Aidha, barabara hii inaunganisha Mkoa wa Pwani na Morogoro. Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina uwezo wa kuhudumia barabara hiyo:- (a) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la kupandisha barabara hiyo kuwa ya Mkoa? (b) Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hiyo ya Ubena – Mvuha kwa kiwango cha changarawe ili ipitike mwaka mzima?

Supplementary Question 4

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali ina wajibu wa kulinda mipaka yake yote ya nchi hii kwa ajili ya kujilinda na maadui mbalimbali wanaovamia ndani ya nchi yetu na ili uweze kulinda mipaka ni lazima kuwe na barabara kwenye mipaka yote, barabara ambazo zinapitika kwa muda wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka wa kusini unaoanzia Mtwara Mjini kupita Mahurunga – Kitaya – Tandahimba – Newala mpaka Ruvuma, hii barabara ilipandishwa hadhi kwa muda mrefu sasa na inaitwa Barabara ya Ulinzi. Mpaka leo Serikali inasuasua kujenga. Naomba kujua ni lini barabara hii ya ulinzi ambayo nimeitaja itajengwa kwa kiwango cha lami ili kulinda mpaka wa kusini sawasawa?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba barabara zote za mipakani ndani ya nchi yetu ziko kwenye mpango wa kutengenezwa kwa kiwango cha lami na barabara hiyo aliyoitaja Mheshimiwa Maftaha ikiwemo. Nimhakikishie Mheshimiwa Maftaha kwamba upembuzi yakinifu umeshafanyika na usanifu wa kina tayari umekwishafanyika. Sasa hivi tuko kwenye taratibu za kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kiwango cha lami kwa barabara husika.

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Barabara ya Ubena, Ngerengere hadi Mvuha ina urefu wa zaidi ya kilometa 70 na inaunganisha Wilaya ya Bagamoyo na Halmashauri ya Morogoro ambako Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Mvuha yanatarajiwa kujengwa. Aidha, barabara hii inaunganisha Mkoa wa Pwani na Morogoro. Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina uwezo wa kuhudumia barabara hiyo:- (a) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la kupandisha barabara hiyo kuwa ya Mkoa? (b) Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hiyo ya Ubena – Mvuha kwa kiwango cha changarawe ili ipitike mwaka mzima?

Supplementary Question 5

MHE. ZAYNAB M. VULLU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa swali la msingi linafanana na hoja nitakayoitoa na kwa kuwa ujenzi wa barabara ni kiungo muhimu kwa ajili ya maendeleo na pia kuboresha hali halisi ya mwananchi; na kwa kuwa Serikali iliahidi kutoka kwenye Ilani yake ya 2005, 2010 na 2015 ujenzi wa barabara kutoka Makofia kwenda Mlandizi, kutoka Mlandizi kwenda Mzenga, kutoka Mzenga kwenda Vikumburu na Manerumango; na kwa kuwa hadi leo barabara hiyo haijajengwa kwa kiwango cha lami. Je, Serikali itaanza lini ujenzi angalau, narudia tena angalau kwa kiwango cha changarawe ili kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo kupata usafiri mzuri na hali kadhalika ukizingatia Mkoa wa Pwani tunaongoza kwa viwanda vya uchumi? Naomba kauli ya Serikali tumesubiri mpaka leo haijajengwa, ni lini Serikali italisimamia jambo hilo? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakiri kwamba Mheshimiwa Zaynab Vullu ni Mbunge ambaye amekuwa akifuatilia sana barabara nyingi sana za Mkoa wa Pwani ambazo ziko kwenye ahadi ya Serikali ya kujengwa kwa kiwango cha lami. Nampongeza sana kwa jitihada zake hizo, naamini kwamba Serikali tumeshasikia na nimhakikishie Mheshimiwa Vullu kwamba mpaka sasa hivi kuna pesa imekwishapitishwa kwenye bajeti hii ya Wizara yetu kutengeneza barabara husika kwa kiwango cha changarawe. Taratibu zinaendelea kufanyika ili pesa itakapopatikana wakati mwingine ujao tujenge kwa kiwango cha lami.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:- Barabara ya Ubena, Ngerengere hadi Mvuha ina urefu wa zaidi ya kilometa 70 na inaunganisha Wilaya ya Bagamoyo na Halmashauri ya Morogoro ambako Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Mvuha yanatarajiwa kujengwa. Aidha, barabara hii inaunganisha Mkoa wa Pwani na Morogoro. Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina uwezo wa kuhudumia barabara hiyo:- (a) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la kupandisha barabara hiyo kuwa ya Mkoa? (b) Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hiyo ya Ubena – Mvuha kwa kiwango cha changarawe ili ipitike mwaka mzima?

Supplementary Question 6

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nimuulize swali Mheshimiwa Waziri; barabara ya kutoka Mwanza kwenda Shinyanga Boarder yenye urefu wa kilometa 102 iliyojengwa mwaka 1994 -1998 ni mbaya sana kwa sasa, ina zaidi ya mashimo 3,032 na imekuwa ikifanyiwa utengenezwaji wa mara kwa mara. Je, Serikali inaweza sasa kusema ni lini barabara hii itajengwa upya?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakiri Serikali tunafahamu ubovu wa barabara aliyoitaja Mheshimiwa na kwa kweli ina mashimo mengi na ni kero sana kwa wapitaji na watumiaji wa barabara ile. Nimhakikishie Mheshimiwa Ndassa kwamba Serikali iko kwenye mpango wa kufanya ukarabati mkubwa kwenye barabara ile na hali ya kifedha itakapoimarika Mheshimiwa Ndassa atatuona tukiwa maeneo yale na wataalam kwa ajili ya kurekebisha kipande hicho cha barabara.