Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Vijana na Akinamama wengi kwa sasa wamewekeza katika kilimo cha mboga mboga, lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima hao kupata soko la uhakika la bidhaa zao?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, hata hivyo nina maswali mawili madogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa kilimo cha bustani kinamtoa mkulima na hasa akinamama na vijana kwenye umaskini kwa uharaka na kupata ajira, lakini licha ya kuwaunganisha na pamoja na TAHA na SAGCOT kuwasaidia wakulima hawa, tatizo kubwa wanalolipata ni mitaji. Je, kuna mkakati gani wa kuwasaidia kupata mikopo nafuu ili akinamama hawa na vijana wanaoshughulika na kilimo cha bustani waweze kupata mikopo hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, licha ya kuwaunganisha na kuanzisha viwanda kwenye mikoa mbalimbali, Mkoa wa Morogoro ni Mkoa unaolima sana mbogamboga na matunda. Je, kuna mkakati gani wa kuweka wawekezaji katika Mkoa wa Morogoro kuanzisha kiwanda cha matunda na mbogamboga? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tatizo la mitaji limekuwa ni moja ya changamoto zinazowafanya wakulima hao hasa ambao wanajihusisha na shughuli za mbogamboga na bustani washindwe kufanya vizuri zaidi. Hata hivyo, kwa kuwa halmashauri zetu zinayo asilimia 10 ambayo inawasaidia akinamama, vijana na watu wenye ulemavu katika kupata mitaji, ni vema Halmashauri basi zielekeze nguvu katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa kupitia Mfuko wetu wa NEDF ambao uko katika Shirika la SIDO, tutahakikisha kwamba hawa wananchi wanafikiriwa zaidi katika kuhakikisha kwamba wanapata mikopo ya aina hiyo pamoja na taasisi nyingine za kifedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili kuhusu kuhamasisha viwanda, Wizara imekuwa ikiendelea kuhamasisha viwanda mbalimbali viweze kuwekeza katika nchi yetu na Mkoa wa Morogoro ambao umeonesha kuwa na fursa kubwa za mbogamboga na matunda. Vilevile, sasa hivi nchi ipo katika majadiliano ya mkataba ambao utawezesha kuwa na soko huru la Afrika litakayowezesha mitaji ya aina mbalimbali kuweza kuingia katika nchi ikiwepo na Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huo tunaamini kwamba, wawekezaji wengi watakuwa na ari ya kuja hasa baada ya kuona kwamba sasa fursa hizo zinafunguliwa na baadhi ya kodi zisizo za lazima au vikwazo vinapunguzwa ili waweze kuwekeza zaidi. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Vijana na Akinamama wengi kwa sasa wamewekeza katika kilimo cha mboga mboga, lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima hao kupata soko la uhakika la bidhaa zao?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, katika maeneo ya Mkoa wa Dar es Salaam na hasa katika Bonde la Mzinga Mbagala, maeneo ya Chanika, Msongola, Kitunda, Mwanagati, Boko, Kibamba, Bunju, Yombo, Kimbiji, Pembamnazi, na Kisarawe II; akinamama na vijana wa maeneo haya wanashughulika sana na biashara ya mbogamboga na matunda. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia akinamama wajasiriamali wa Mkoa wa Dar es Salaam waweze kupeleka bidhaa zao za mboga na matunda nje ya nchi ukizingatia tuna fursa kubwa ya uwanja wa ndege mpya mkubwa wa Kimataifa katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutoa mafunzo ya namna bora ya kusindika matunda hayo kwa kupitia SIDO vilevile kuona kwamba hata uuzaji wa mboga hizo unakaa katika viwango na tija. Jambo ambalo linahuzunisha kidogo ni kwamba katika Halmashauri zetu au Serikali za Vijiji tumekuwa hatutengi maeneo mazuri mahsusi kwa ajili ya hawa wakulima ili sasa hizo bidhaa zao za mashambani ziweze kukaa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa rai kwamba, mkulima aweze kusaidiwa kuanzia shambani mpaka sokoni na pia kupewa mafunzo ya aina hiyo na hivyo kuweza kufanikisha hata inapokuja fursa ya kuweza kuuza nje ya nchi.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Vijana na Akinamama wengi kwa sasa wamewekeza katika kilimo cha mboga mboga, lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima hao kupata soko la uhakika la bidhaa zao?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ukitoka Dodoma hapa kama unaelekea Dar es Salaam, ukianza Wilaya ya Gairo kabla ya kufika Jimbo Mvomero, hapa katika maeneo ya Magole wapi kila sehemu unakuta vijana wamebeba nyanya, karoti, na kadhalika huko Morogoro na ukifika pale kituo cha mizani. Ni mkakati gani Serikali wanafanya maalum kwa ajili ya Morogoro kuwasaidia hawa vijana wadogo wadogo ili kukuza uchumi wao, kwa sababu wanashinda barabarani, mwisho watagongwa na magari. Naomba Serikali iseme ni mkakati gani kuhusu Morogoro mnawasaidia hawa vijana wanaoshinda barabarani? (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi kama ambavyo nimesema hapo awali, jukumu letu ni kuhamasisha kwanza kuwatambua hawa wafanyabiashara wadogowadogo sana yaani (Micro Entrepreneurs). Ninalosisitaza ni kwamba mara nyingi hata tunapozungumzia maeneo ya uwekezaji au katika shughuli za kuwezesha tumekuwa tunawaangalia zaidi hawa wakubwa kuliko hawa wadogowadogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kwa sasa imeshajipanga kuona kwamba hawa wajasiriamali wadogo wadogo wawe wa matunda, wawe wa biashara nyingine, wanasaidiwa ili kuweza kupata maeneo ambayo yatawawezesha kufanya shughuli zao vizuri na tunasema kwamba uchumi uanzie shambani hadi sokoni na maeneo mengine kama viwandani.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Vijana na Akinamama wengi kwa sasa wamewekeza katika kilimo cha mboga mboga, lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima hao kupata soko la uhakika la bidhaa zao?

Supplementary Question 4

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika msimu wa kilimo wa mwaka jana na hata mwaka juzi, mazao ya mbaazi na kilimo yalipata anguko kubwa kwenye masoko. Hivi sasa msimu wa mavuno wa mazao hayo umeanza katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Je, Serikali ina habari yoyote njema kwa wakulima kuhusu masoko ya mazao ya mbaazi na mahindi? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo mara ya mwisho nilijibu suala la soko la mbaazi, kwanza tumekuwa tukitegemea sana soko hilo kutoka nchi za nje hasa India lakini nao wakawa wamelima kiasi kwamba hawakuweza kununua mbaazi kutoka kwetu. Kupitia TanTrade tumewaagiza kuendelea kufuatilia masoko kwa ajili ya mbaazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huu kwa kutambua umuhimu wa zao hili la mbaazi na umuhimu wake katika afya naendelea kusisitiza kwamba Watanzania tupende pia kutumia mbaazi kwa sababu ni chakula bora na kina lishe nzuri. (Makofi)

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Vijana na Akinamama wengi kwa sasa wamewekeza katika kilimo cha mboga mboga, lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima hao kupata soko la uhakika la bidhaa zao?

Supplementary Question 5

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Vijana wote nchini wameamka na kuungana na Serikali yao katika kutekeleza kwa vitendo Sera ya Uchumi wa Viwanda, japokuwa katika majibu ya Serikali, Serikali imeshindwa ku-acknowledge jitihada za vijana katika kukuza uchumi wa nchi. Sasa Serikali ni lini itatambua na kuthamini jitihada za vijana katika kukuza uchumi wa nchi? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, naomba tu tufahamu kwamba, suala la kuwezesha vijana kiuchumi ni suala mtambuka. Sekta zote inabidi tushirikiane kwa pamoja ikiwemo Waheshimiwa Wabunge. Wizara kama ambavyo nimesema awali tumeshajipanga kuhakikisha kwamba tunakuwa na mkakati maalum wa kuwezesha makundi hayo ya kibiashara kuanzia katika maeneo yao ya kufanyia biashara na tunazidi kuhamasisha Halmashauri zetu, kwa mfano zitenge maeneo ambayo vijana wanaweza kufanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, si jambo jema kuwaona vijana wakiwa wanazunguka zunguka tu mitaani, halafu yanajengwa majengo makubwa yanaachwa vijana hawaingii humo kufanyia kazi. Kwa misingi hiyo, tumejipanga na tunataka kuona kwamba vijana wanasaidiwa ili iwe ni rahisi kuwatambua na vilevile kuweza kupata huduma zote za msingi zinazohusiana na uwezeshaji. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuwatambua vijana na kuwasaidia ili waweze kuingia kwenye sekta ya viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kulithibitishia Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali imekuwa ikiwasaidia sana vijana na kuwawezesha katika sekta mbalimbali. Wizara ya Habari ya Michezo na Utamaduni wameshafanya kazi kubwa sana katika kutambua vipaji vya vijana na kuwajengea uwezo. Ofisi ya Waziri Mkuu tumeshasema tumetambua vijana waliokwishafanya vizuri kwa mfano, wale vijana wa kutoka Chuo cha SUA, wamefanya vizuri sana kwenye sekta ya kilimo, sasa tunawatumia hao kuendesha mafunzo ya kilimo cha kitalu nyumba katika nchi nzima ya Tanzania, huko ni kutambua juhudi zao na kuwawezesha zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaendelea kutoa mafunzo yenye ujuzi wa namna mbalimbali ili vijana wajiajiri na waajiriwe katika maeneo mbalimbali ya sekta za viwanda na sekta za biashara. Serikali inatambua sana na tutaendelea kutambua juhudi hizo kila siku na kuwawezesha vijana wa Tanzania. (Makofi)

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Vijana na Akinamama wengi kwa sasa wamewekeza katika kilimo cha mboga mboga, lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima hao kupata soko la uhakika la bidhaa zao?

Supplementary Question 6

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa fursa. Moja ya jukumu kubwa walilopewa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ni pamoja na kuhakikisha usalama wa chakula lakini kubwa zaidi ni kuchangamkia fursa za upatikanaji wa masoko ya bidhaa za kilimo nje ya nchi. Nataka kujua benki hii imeshafanya juhudi hizo kwa kiasi gani?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI, VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani anaendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais katika hotuba yake ya hivi karibuni siku anazindua mradi wa ASDP kwamba benki hii imefanya kazi lakini ifanye kazi zaidi. Kwa sasa tunachosema ni kwamba isaidie zaidi katika suala la kuhakikisha kwamba pembejeo na nyenzo za kilimo zinawafikia wakulima wengi zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huo Wizara yetu tayari katika tractors ambazo tayari tumeshaziunganisha zaidi ya 148, Benki ya Kilimo (TAB) tayari tupo nao pamoja katika kuhakikisha kwamba tunawawezesha wakulima na wale ambao watahitaji kukopa trekta hizo. Kwa hiyo, niseme tu kwamba Mheshimiwa Mbunge ameunga mkono kwa kuuliza swali lakini tunataka Benki hiyo ifanye zaidi na zaidi.