Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. HASNA S. MWILIMA aliuliza:- Wananchi wa Humule, Ubanda, Tandala na maeneo mengine ya Itebula wamekuwa wakisosa maeneo ya kulima kwa madai kuwa wanaingilia maeneo ya hifadhi:- • Je, Serikali haioni sasa ni muhimu kusogeza mipaka kwa kushirikiana na TAMISEMI ili wananchi wapate maeneo ya kulima? • Je, ni lini Serikali itamaliza usumbufu wanaoupata Wananchi wa Kijiji cha Kalilani kwa kudaiwa kuwa wamo ndani ya Hifadhi wakati Kijiji hiki kimesajiliwa kwa mujibu wa sheria?

Supplementary Question 1

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimwombe Mheshimiwa Waziri kwenye swali langu la (a) amejibu kitu tofauti kabisa na swali ambavyo nilivyoliuliza. Pamoja na hayo, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; hivi karibuni tumemwona Mheshimiwa Rais wetu akitoa maelekezo kwenye Wizara hii ya Maliasili kugawa baadhi ya maeneo ya Hifadhi kwa ajili ya wakulima na wafugaji, kwa mfano Kagera Nkanda, Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo kwa wananchi wa Kagera Nkanda, Wilaya ya Kasulu wapewe eneo ndani ya hifadhi kwa ajili ya kulima na kufuga. Kwa nini sasa Mheshimiwa Waziri asitoe maelekezo yale yale yaliyotumika kuwagawia wananchi wa Kagera Nkanda awagawie sasa na wananchi wanaouzunguka maeneo ya Pakunda, Pachambi na maeneo ya Ipuguru?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kuwa tunafahamu kwamba utaratibu wa uwekaji wa vigingi unatakiwa ufuate sheria. Kijiji cha Kalilani na Kijiji cha Sigwesa kimesajiliwa kwa mujibu wa sheria. Je, Mheshimiwa Waziri akija akigundua kwamba GN hivi vigingi vilivyowekwa kwenye Kijiji cha Kalilani na Kijiji cha Sigwesa hakikufuata taratibu atakuwa yuko tayari kuondosha vile vigingi na kuviweka nyuma ili kupunguza migogoro iliyopo baina ya Vijiji vya Sigwesa na kijiji cha Kalilani? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza kwa jinsi ambavyo ameeleza, inawezekana kweli labda maeneo mengine majibu tuliyoyatoa hayajafikia, hayajawa katika kile kiwango alichokusudia, nimuahidi tu kwamba mimi nitapata nafasi ya kwenda kutembelea katika eneo hilo, ili niende kutembelea kijiji hadi kijiji na kitongoji hadi kitongoji kusudi tuweze kubaini kama kweli kuna upungufu wa namna hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuwagawia maeneo ya hifadhi naomba nimshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza utaratibu wa kugawa hifadhi kwa sasa jinsi ulivyo, kwa kweli kuna kazi kubwa sana. Hata hivyo, kama pale ikionekana kweli wananchi wa Jimbo husika wana matatizo ya ardhi na hawana mahali pa kulima, hawana mahali pa kufugia mifugo yao na mambo mengine, basi namuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri aangalie, afanye mchakato na awasiliane na Wizara ya Maliasili na Utalii ili tuangalie katika yale maeneo ambayo yanahifadhiwa chini ya Serikali za Vijiji, kama yanaweza yakamegwa na wananchi wakaweza kupatiwa hilo eneo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, kuhusu kuondoa vigingi pale ambapo itaonekana kuna makosa. Tuko tayari kabisa pale ambapo itaonekana vigingi vimewekwa katika maeneo ambayo siyo sahihi, tuko tayari kabisa kwamba tutaviondoa na tutaviweka katika maeneo ambayo yanastahili pale ambapo mipaka kisheria inatakiwa kuwekwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kuna matatizo hayo Nchi nzima, na ndiyo maana tuliahidi mbele ya Bunge hili tutakwenda kila eneo kuhakikisha kwamba vigingi vinawekwa katika maeneo yale yanayotakiwa. (Makofi)

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASNA S. MWILIMA aliuliza:- Wananchi wa Humule, Ubanda, Tandala na maeneo mengine ya Itebula wamekuwa wakisosa maeneo ya kulima kwa madai kuwa wanaingilia maeneo ya hifadhi:- • Je, Serikali haioni sasa ni muhimu kusogeza mipaka kwa kushirikiana na TAMISEMI ili wananchi wapate maeneo ya kulima? • Je, ni lini Serikali itamaliza usumbufu wanaoupata Wananchi wa Kijiji cha Kalilani kwa kudaiwa kuwa wamo ndani ya Hifadhi wakati Kijiji hiki kimesajiliwa kwa mujibu wa sheria?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa muda mrefu sana katika Wilaya ya Kasulu, eneo la Kagera Nkanda wananchi walikuwa wakizuiliwa kulima. Mwaka jana tarehe 21 Mheshimiwa Rais alipokuja Wilaya ya Kasulu wananchi walimpokea kwa nderemo na vigelegele akawaruhusu kwenda kulima katika pori la Kagera Nkanda, lakini hivi sasa ninavyoongea tarehe 21 mwezi huu, wananchi wameambiwa waondoe mazao katika eneo hilo la Kagera Nkanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kauli ya Serikali, ni kwa nini wananchi waliruhusiwa na Mheshimiwa Rais kulima katika eneo hilo na leo wanaondolewa kwa kutaka kupigwa ndani ya wiki moja? Naomba kauli ya Serikali. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Mheshimiwa Rais alitoa maagizo kwamba lile eneo ligawiwe kwa wananchi ili waweze kulitumia katika shughuli zingine za kibinadamu za uzalishaji. Naomba nimhakikishie tu kwamba agizo la Mheshimiwa Rais alilolitoa linatekelezeka na lazima liheshimike, kama kuna mtu analikiuka hilo tutashughulika nae. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa ambacho kinatakiwa sasa hivi kufanyika ni kuhakikisha kwamba baada ya Rais kutoa lile eneo, taratibu za kisheria ya kuondoa na kuweka mipaka mipya lazima zifanyike. Kwa hiyo, wale Watendaji ambacho tunakifanya sasa hivi ni kuhakikisha kwamba sasa tunarekebisha ile mipaka, ili kusudi yale maeneo yaliyogawiwa kwa wananchi yabaki kwa wananchi na yale mengine ambayo yanatakiwa kubaki kama hifadhi yaendelee kubaki kama hifadhi.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. HASNA S. MWILIMA aliuliza:- Wananchi wa Humule, Ubanda, Tandala na maeneo mengine ya Itebula wamekuwa wakisosa maeneo ya kulima kwa madai kuwa wanaingilia maeneo ya hifadhi:- • Je, Serikali haioni sasa ni muhimu kusogeza mipaka kwa kushirikiana na TAMISEMI ili wananchi wapate maeneo ya kulima? • Je, ni lini Serikali itamaliza usumbufu wanaoupata Wananchi wa Kijiji cha Kalilani kwa kudaiwa kuwa wamo ndani ya Hifadhi wakati Kijiji hiki kimesajiliwa kwa mujibu wa sheria?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo lililoko Kigoma Kusini linafanana kabisa na tatizo lililoko kwenye Jimbo la Ndanda hasa maeneo ya Namajani na Mahinga ambako mipaka kati ya Jeshi la Magereza pamoja na wananchi haieleweki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna tatizo kama hilo kwenye Kata ya Chingulungulu, Kijiji cha Misenjesi kati ya Hifadhi ya Taifa pamoja na wananchi. Sasa nataka kufahamu, ni lini Serikali itakwenda kutoa ufafanuzi mzuri na kuweka mipaka hii sahihi kati ya Mbuga ya Misenjesi na wanakijiji wa Kijiji cha Chingulungulu kwa sababu pametokea matatizo makubwa ya kutoelewana maeneo hayo? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kama nilivyosema kwenye nchi nzima kuna maeneo ambayo yana matatizo ya mipaka na kama alivyosema mwenyewe kwenye Jimbo lake kuna maeneo hayo. Nataka nimhakikishie tu kwamba, tuko tayari sasa hivi, tunapitia mipaka yote nchi nzima na tutakwenda huko pia kuangalia huo mpaka ili tuone kwamba ni nani ameingia nani hajaingia kusudi tuweze kurekebisha matatizo hayo na migogoro yote iweze kumalizika, hiyo tutaifanya karibu nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge awe na uvumilivu kidogo, baadaye tatizo lake hilo litamalizika. (Makofi)