Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika kampeni za uchaguzi tarehe 18 Novemba, 2005 aliwaahidi wananchi wa Kibiti kuwa Serikali yake itajenga barabara ya Kibiti-Kikale ili kupunguza adha kubwa ya usafiri wanayopata wananchi wa Vijiji vya Mchukwi, Rungungu, Nyamatanga na Kikale ambamo barabara hiyo inapita:- a) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza? b) Je, ujenzi huo unaotarajiwa utakuwa ni wa kiwango gani?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; wananchi wa Mtunda – Kikale -Myuyu bado wanapata shida kwani njia ile haipitiki kabisa kutokana na mvua nyingi zilizonyesha. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati huo kwa haraka ili barabara hiyo iweze kutoa huduma?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, barabara ya kutoka Bungu - Msolo nayo haipitiki kabisa, tena hatari zaidi kuna shimo kubwa pale Bungu ambalo linaweza likakata mawasiliano baina ya wananchi wa Bungu na Msolo. Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati barabara hiyo ili wananchi hawa sasa wapeleke mazao yao sokoni na wapate faida haraka iwezekanavyo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepata fursa ya kutembelea Jimboni kwa Mheshimiwa Mbunge, nikafika mpaka Delta na changamoto anazozitaja nazifahamu. Naomba nitumie fursa hii kumwagiza Meneja wa TARURA aende site akatazame kilichopo ili aweze kutushauri nini kifanyike ili wananchi wa Jimbo analolisema Mheshimiwa Mbunge wasije wakapata adha ya kukosa usafiri ili mazao yao yaweze kufika sokoni. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika kampeni za uchaguzi tarehe 18 Novemba, 2005 aliwaahidi wananchi wa Kibiti kuwa Serikali yake itajenga barabara ya Kibiti-Kikale ili kupunguza adha kubwa ya usafiri wanayopata wananchi wa Vijiji vya Mchukwi, Rungungu, Nyamatanga na Kikale ambamo barabara hiyo inapita:- a) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza? b) Je, ujenzi huo unaotarajiwa utakuwa ni wa kiwango gani?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali ndogo la nyongeza. Ahadi hizi ambazo zimetolewa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ziko nyingi nchi nzima na kwa kweli zipo ambazo hazijatekelezwa kabisa, ikiwemo ujenzi wa kilomita mbili za lami katika Mji wa Karatu. Ahadi hiyo ilitiliwa msisitizo na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano akasema ataongeza kilomita nane jumla ziwe kilomita 10, lakini mpaka leo utekelezaji haujafanyika. Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli kwamba kuna ahadi ambazo zimetolewa na Marais waliotangulia na katika utaratibu wa kawaida ni kupokezana kijiti, pale ambapo mwenzako ametekeleza yale ambayo hakuyamaliza wewe unahakikisha unayachukua na wewe unaongeza ahadi za kwako ili kutekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Paresso ni azma ya Serikali ndani ya kipindi cha miaka mitano ambayo ndiyo mkataba wa Mheshimiwa Rais na wapiga kura wake, barabara yake hiyo itaweza kutekelezwa kama ambavyo ahadi ya Mheshimiwa Rais ilivyoahidiwa.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika kampeni za uchaguzi tarehe 18 Novemba, 2005 aliwaahidi wananchi wa Kibiti kuwa Serikali yake itajenga barabara ya Kibiti-Kikale ili kupunguza adha kubwa ya usafiri wanayopata wananchi wa Vijiji vya Mchukwi, Rungungu, Nyamatanga na Kikale ambamo barabara hiyo inapita:- a) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza? b) Je, ujenzi huo unaotarajiwa utakuwa ni wa kiwango gani?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kata ya Kapalamsenga sasa hivi iko kisiwani kwa kukosa miundombinu baada ya mvua zilizonyesha kuharibu kabisa miundombinu ya barabara. Serikali ina mpango gani wa kuharakisha kuifanyia matengenezo barabara hiyo ambayo kimsingi inawasaidia kwa ajili ya shughuli za maendeleo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba mvua za safari hii zimekuwa nyingi pamoja na neema ambayo inasababishwa na mvua lakini ni ukweli usiopingika kwamba barabara zetu nyingi zimeharibika. Naomba nitumie fursa hii nimuagize Meneja wa TARURA aende huko barabara ya Kapalamsenga ili akatizame uhalisia na nini ambacho tunaweza tukafanya ili wananchi waendelee kupata huduma. (Makofi)