Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa wananchi wa Nyamisati wamekuwa wakipata adha kubwa sana katika eneo la kivuko. Je, ni lini Serikali itajenga Gati la Nyamisati?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri ya swali hilo, nina maswali mawili ya nyongeza.
(i) Wananchi wa Nyamisati walipisha ujenzi huo lakini sehemu waliyopelekwa miundombinu yao imekuwa siyo rafiki. Mfano hakuna choo, banda la abiria ni kifusi katika hilo gati la muda. Je, lini sasa Serikali itakamilisha ujenzi huo?
(ii) Vijana wa maeneo hayo wamejiunga na vikundi vyao vya ujasiriamali kama mkombozi. Je, sasa Serikali ina mpango gani wa kuwapa kipaumbele katika ujenzi huo ili vijana hao wafaidike, wapate vibarua ukizingatia watu wa Pwani wanasema mgeni njoo mwenyeji apone? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Ungando kwa jinsi alivyofuatilia kwa muda mrefu sana ujenzi wa gati hili la Nyamisati. Ninakumbuka kuna kipindi fulani tuliwahi kwenda naye mpaka kufanya kikao na watu wa TPA kwa ajili ya kufuatilia kwa ukaribu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza kujibu swali lake la kwanza, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi, tayari TPA wanamtafuta mkandarasi kwa ajili ya kujenga choo cha umma pamoja na sehemu ya kupumzikia kwa maeneo ambako wananchi wamepisha ujenzi wa gati uendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo, tutakapopata mkandarasi hilo eneo litajengwa kwa ajili ya wananchi kupumzika vilevile kutakuwa na maeneo rafiki kwa ajili ya wananchi ambao watakuwa wanasubiri huduma za gati hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu la swali lake la pili, ninaielekeza TPA, ninajua kwamba kwenye mkataba ambao wameingia na hawa wakandarasi wawili kuna kipengele ambacho kinawataka wakandarasi wawachukue wazawa katika shughuli zile ambazo siyo za kitaalam kuweza kufanya kazi kama vibarua na vitu kama hivyo. Ninawaagiza TPA wahakikishe wanafanya kazi kama walivyoingia mkataba na wakandarasi kutumia wazawa katika shughuli ambazo siyo za kitaalam. Ahsante. (Makofi)

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa wananchi wa Nyamisati wamekuwa wakipata adha kubwa sana katika eneo la kivuko. Je, ni lini Serikali itajenga Gati la Nyamisati?

Supplementary Question 2

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ukweli kwamba mkandarasi yupo site, lakini kasi ya mobilization na vifaa duni anavyovitumia vinatia mashaka sana kama mkandarasi anaweza akamaliza kazi hii katika muda uliotajwa.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari baada ya kikao hiki cha bajeti, mimi, Mheshimiwa Ungando, Mbunge wa Kibiti na mama yetu Mheshimiwa Salma Kikwete ambaye ni mdau mkubwa sana wa Gati la Nyamisati, tufanye ziara ya pamoja ili kuhakikisha kwamba gati hili linakwisha kwa muda uliopangwa?(Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikiri kwamba kati ya Wabunge ambao wamekuwa wakifuatilia suala la Gati hili la Nyamisati ni pamoja na Mheshimiwa Dau na Mheshimiwa Mama Salma Kikwete, wote kwa pamoja wamekuwa wakifuatilia na wakitaka kujua hatua mbalimbali ambazo zinaendelea katika ujenzi wa gati hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vifaa wakandarasi wanavyo, bado wanaendelea kukusanya, kama nilivyozungumza kwenye majibu ya awali kwamba wako kwenye mobilization kwa hiyo vifaa bado vinaendelea kuletwa na wana vifaa vya kutosha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo, ndiyo maana tumeweka deadline, huu mradi utakabidhiwa mwezi mapema Machi mwakani. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba vifaa vitafika kwa wakati na nipo tayari kwenda nao Waheshimiwa Wabunge wote kwa ajili ya kwenda kuukagua mradi huo.(Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa wananchi wa Nyamisati wamekuwa wakipata adha kubwa sana katika eneo la kivuko. Je, ni lini Serikali itajenga Gati la Nyamisati?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kisiwa cha Izumacheri hawana usafiri tofauti na usafiri wa Meli ya MV Chato, leo ni mwaka wa tatu toka tumeingia Bungeni Mheshimiwa Rais aliahidi, meli hiyo inapaki juu ya jiwe, na ni mwaka wa pili tunaahidiwa kuletewa pesa kwa ajili ya ujenzi wa gati.
Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kuambatana nami baada ya Bunge kwenda kuona adha ya meli inayo-park juu ya jiwe ili uweze kuachia pesa kwa ajili ya ujenzi wa gati hilo?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Rais aliahidi ujenzi wa gati kwa eneo hilo na bado Serikali inatambua na inaendelea kufuatilia namna ya utekelezaji wa ahadi hiyo ya Rais.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumewaagiza TPA toka mwaka jana mwanzoni, wanaendelea na utaratibu wa kutuletea gharama halisi za kutengeneza gati eneo hilo ili wananchi waweze kupata huduma kwa usahihi. Nieleze tu kwamba niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Musukuma kwenda kuangalia eneo hilo kwa ajili ya kuweka gati. Ahsante. (Makofi)

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa wananchi wa Nyamisati wamekuwa wakipata adha kubwa sana katika eneo la kivuko. Je, ni lini Serikali itajenga Gati la Nyamisati?

Supplementary Question 4

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa na mimi fursa ya kuuliza swali la nyongeza:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa vivuko vya Kigamboni vimekuwa vikiharibika mara kwa mara; je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha inavitengeneza vivuko hivi ili kuondosha maafa yasitokee kwa wananchi ambao wanavitumia?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia TEMESA Serikali imeendelea kuvihudumia vivuko mbalimbali vilivyopo nchini kwetu kuhakikisha vinafanya kazi kama vinavyotakiwa.
Mimi nina taarifa kwamba hicho kivuko kilikuwa na hitilafu kidogo na ninamuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari kufuatilia baada ya muda, hata tukitoka nje tutawasiliana na watu wa TEMESA kuona kuna changamoto gani kwenye hicho kivuko ili ziweze kutatuliwa. Ahsante.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa wananchi wa Nyamisati wamekuwa wakipata adha kubwa sana katika eneo la kivuko. Je, ni lini Serikali itajenga Gati la Nyamisati?

Supplementary Question 5

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali kwa kutupatia Kivuko cha Msinjahili, Kitumbikwera kule Lindi. Je, ni lini Serikali itakamilisha eneo la kituo cha kupumzikia wasafiri au cha kusubiria wasafiri kati ya Msinjahili na upande wa Kitumbikwera? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Ni kweli kwamba tumerekebisha kivuko alichozungumza Mheshimiwa Mbunge na kwa kweli sasa hivi kimeshaanza kutumika. Kwenye package ya tenda aliyopata mkandarasi wa kujenga kivuko kile, tulimwambia aweke na sehemu ambako wananchi watapumzika. Nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba nitafuatilia kuona kwamba sehemu ya kupumzika inatengenezwa.