Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Utumishi wa umma ndiyo injini ya maendeleo katika nchi. Watumishi wa umma hawatakiwi kuwa na mrengo wowote wa itikadi ya kisiasa ili kutumikia wananchi kwa muda wote hata yanapotokea mabadiliko ya vyama tawala baada ya uchaguzi. i. Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati gani wa kuhakikisha utumishi wa umma ni thabiti na wa kuaminika wakati wote? ii. Je, ni watumishi wangapi wa umma ambao wamegombea vyeo katika chama tawala wakati wapo katika ajira ya utumishi wa umma?

Supplementary Question 1

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakurugenzi wa Halmashauri ambao wameteuliwa wengi wao walikuwa ni wana-CCM walioshindwa katika kura za maoni, nao ndio wasimamizi wa uchaguzi. Kuna wengine hata kwa mfano huyo wa Ubungo mpaka leo anahudhuria vikao vya CCM.
Swali langu, ikiwa tutaleta orodha ya Wakurugenzi ambao tunajua ni wana-CCM na walikuwa katika kura za maoni; je, Serikali itakuwa tayari kuwaondoa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tunao Wakuu wa Mikoa ambao wanalipwa kwa pesa za walipa kodi, Watanzania wenye vyama na wasiokuwa na vyama, lakini wengi wameonesha itikadi za mrengo wa kisiasa; tukiangalia Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mkuu Mkoa wa Manyara na wengine; je, Serikali ina kauli gani kuhusu hilo? Ahsante. (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nianze kumpongeza Waziri Kivuli wa Wizara yangu, mdogo wangu Mheshimiwa Ruth Mollel kwa jinsi anavyofuatilia utendaji kazi wa Wizara yangu na hiyo ndiyo kazi ya Waziri Kivuli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkurugenzi yeyote utakayemchagua katika nchi hii lazima kuna chama anachokipenda. Huyu yuko pale baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi na Waraka ule wa Utumishi wa Umma unasema; “Mtumishi wa umma anayeteuliwa na Rais, endapo hataridhia kufanya ile kazi, ana ruhusa ya kumwambia Mheshimiwa Rais, naomba niendelee na kazi yangu.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hawa Wakurugenzi walipokuwa wanafanya kazi, wameshakoma kazi waliyokuwa wanaifanya, kazi iliyobaki sasa hivi ni Mkurugenzi wa Halmashauri. Nataka niseme nchi zote duniani baada ya uchaguzi, Rais anayeingia madarakani, anapanga safu yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda Marekani, State House yote, wahudumu, wafagizi wote, akiingia Rais mpya, anaondoa anapanga watu wake. Sasa kama Mheshimiwa Rais kafanya hivyo kwa hao Wakurugenzi, ndivyo alivyoona inafaa, nasi ndani ya Serikali, tunaona wanachapa kazi vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yule wa Ubungo kuhudhuria vikao, nataka niseme hivi, mkishakuwa na chama tawala, siku zote wajibu wenu ni kuihoji Serikali. Mkurugenzi wa Ubungo sio Mjumbe katika vikao vya CCM, lakini anaweza kuitwa saa yoyote aende kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi katika Jimbo la Ubungo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusu Wakuu wa Mikoa; kauli gani Wakuu wa Mikoa wanaoshiriki siasa, wanaoonesha wanapendelea upande mmoja, nataka niseme hivi, Mkuu wa Mkoa ndio mwakilishi wa Rais katika Wilaya ile. Mkuu wa Mkoa ndio Rais wa Mkoa ule. Rais ni neno la kiarabu, maana yake kichwa. Kwa hiyo, kichwa cha Mkoa ule ni Mkuu wa Mkoa. Huyu Mkuu wa Mkoa anamwakilisha Rais. Hutegemei huyu Mkuu wa Mkoa afanye mambo tofauti na anavyofanya Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie kusema kwamba nchi hii tuna chombo kinaitwa Mahakama. Mhimili wa Mahakama kazi yake ni kutafsiri sheria. Pale mtu ameona kwamba amekuwa aggrieved, au pale mtu ameona kwamba ametendewa ndivyo sivyo, basi tufuate mkondo wa sheria. Baadhi yao mnaowasema, walikuja hapa kwenye maadili, wakasikiliza, wakawa cleared, wakaonekana hawana makosa. (Makofi)

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Utumishi wa umma ndiyo injini ya maendeleo katika nchi. Watumishi wa umma hawatakiwi kuwa na mrengo wowote wa itikadi ya kisiasa ili kutumikia wananchi kwa muda wote hata yanapotokea mabadiliko ya vyama tawala baada ya uchaguzi. i. Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati gani wa kuhakikisha utumishi wa umma ni thabiti na wa kuaminika wakati wote? ii. Je, ni watumishi wangapi wa umma ambao wamegombea vyeo katika chama tawala wakati wapo katika ajira ya utumishi wa umma?

Supplementary Question 2

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na baada ya maelezo ya Mheshimiwa Waziri, nina swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Tanzania ni nchi ya Mfumo wa Vyama Vingi na kwa kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ndio Msimamizi wa Uchaguzi.
Je, Serikali sasa iko tayari kuleta mabadiliko ya Sheria ya Mkurugenzi wa Halmashauri asiwe msimamizi wa uchaguzi hasa kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019? (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria zilizopo sasa, zilizotungwa na Bunge hili zinasema Mkurugenzi wa Halmashauri, Mkurugenzi wa Jiji, Manispaa unapofika wakati wa uchaguzi ndiyo msimamizi wa uchaguzi. Pale inapotokea kwamba Bunge hili litaona haja ya kubadili, hoja iletwe, tutaijadili. Ikibadilishwa, mimi mtumishi wa Bwana nitatenda kama Bwana anavyotaka. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Utumishi wa umma ndiyo injini ya maendeleo katika nchi. Watumishi wa umma hawatakiwi kuwa na mrengo wowote wa itikadi ya kisiasa ili kutumikia wananchi kwa muda wote hata yanapotokea mabadiliko ya vyama tawala baada ya uchaguzi. i. Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati gani wa kuhakikisha utumishi wa umma ni thabiti na wa kuaminika wakati wote? ii. Je, ni watumishi wangapi wa umma ambao wamegombea vyeo katika chama tawala wakati wapo katika ajira ya utumishi wa umma?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza naomba nianze kwa kuwapongeza Wakurugenzi wote nchini akiwemo Kayombo wa Ubungo na Arusha Mjini kwa kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu kwa kuwa ili kuwa thabiti katika utumishi wa umma ni pamoja na kuwajali watumishi; na Mheshimiwa Rais alianza kuonyesha mfano kwa kuwajali walimu wa shule za msingi kwa kuwapatia tablets, napenda kufahamu, je, Serikali ina mikakati gani kuwajali watumishi wa umma katika maslahi yao? (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anataka kujua Serikali inafanyaje katika kuwajali watumishi. Tarehe 1 Mei, 2018 Mheshimiwa Rais alipohutubia Uwanja wa Samora pale Iringa alipokuwa mgeni rasmi, alipokuwa anajibu risala ya wafanyakazi alisema; Serikali yake inatumia fedha kadri zinavyokusanywa. Kwa hiyo, ataboresha maslahi ya watumishi wa umma kulingana na uwezo wa Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia alisema;“mimi sitangoja May Day, siku yoyote nitakapotosheka kwamba hali ya Mfuko wa Serikali inaniruhusu kufanya nyongeza, kuboresha maslahi ya Watumishi wa Umma nitafanya hivyo.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka niseme kwamba Serikali inawajali watumishi, inawapeleka mafunzo, wanapewa mikopo, wengine tunawadhamini katika kupewa mikopo, tunawapeleka kusoma nchi za nje katika taaluma mbalimbali, hiyo yote ni kujali watumishi, maana kumjali mtumishi siyo lazima kumpatia fedha tu, hata ukimpeleka mafunzo, unamjali mtumishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hayo yote niseme kwa kifupi kwamba tunaendelea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma, lakini kwa upande wa mishahara kama nilivyosema tutapandisha mishahara pale hali ya nchi itakaporuhusu.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Utumishi wa umma ndiyo injini ya maendeleo katika nchi. Watumishi wa umma hawatakiwi kuwa na mrengo wowote wa itikadi ya kisiasa ili kutumikia wananchi kwa muda wote hata yanapotokea mabadiliko ya vyama tawala baada ya uchaguzi. i. Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati gani wa kuhakikisha utumishi wa umma ni thabiti na wa kuaminika wakati wote? ii. Je, ni watumishi wangapi wa umma ambao wamegombea vyeo katika chama tawala wakati wapo katika ajira ya utumishi wa umma?

Supplementary Question 4

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kauli ambayo Wakurugenzi walielezwa kwamba wamepewa ajira, wamepewa magari na wanalipwa mshahara na Mheshimiwa Rais, ole wake Mkurugenzi ambaye atamtangaza mpinzani. Kauli hii imeleta sintofahamu, kutojiamini na hofu katika chaguzi mbalimbali. Nini kauli ya Serikali sasa juu ya kauli hii ya tishio la uchaguzi ulio huru na haki? (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ndugu yangu Mheshimiwa Waitara hajalieleza Bunge hili kwamba kauli hiyo imetoka lini? Alisema nani? Katika shughuli gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mzee wa zamani, nilifundishwa kwamba government moves on paper. Kwa hiyo, huwezi ukaja Bungeni hapa ukasema fulani alisema hivi na hivi na hivi. Kwa kifupi tu nataka nimjibu ndugu yangu Mheshimiwa Waitara kwamba Wakurugenzi tumewafundisha na tumewafanyisha semina wafanye kazi kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni zilizopo.