Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y. MHE. DKT. MARY M. NAGU) aliuliza:- Katika msimu wa mwaka 2015/2016, Wilaya ya Hanang ilikumbwa na mvua kubwa sana iliyosababisha kuharibika kwa miundombinu ikiwemo ya barabara. (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilitengwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo? (b) Je, ni lini Serikali itajenga na kukamilisha barabara iliyofunguliwa na Wachina inayopita katika Vijiji vya Mig’enyi, Milongoli, Gawidu hadi Ngamu na barabara inayounganisha Sechet, Wilaya ya Babati Vijijini kupitia Vijiji vya Basodesh, Basotu mpaka Mulbadaw?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara kutoka Babati - Basodesh kuna korongo kubwa sana ambalo linawazuia watoto kwenda shule na kutokana na mvua hizi, ndiyo kabisa hali imekuwa mbaya. Je, Serikali ina mpango gani kuwasaidia watu hawa wa Hanang ili daraja au korongo hili likaweza kujengwa kwa sababu bajeti ya Halmashauri ya Hanang ni ndogo haiwezi kujenga barabara?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Wilaya ya Hanang na Jimbo la Mbulu Vijijini lilikuwa pacha. Kuna barabara nyingine inayotoka Dongobesh kupitia Maretadu kwenda Haydom hapitiki kabisa kwa sababu ya mvua hizi ambazo zimekuwa nyingi maeneo ya kule Mbulu. Je, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ina mpango gani wa kusaidia kukarabati barabara hizi ambazo mvua nyingi zimeharibu kabisa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge mtakubaliana nami kwamba mvua zilizonyesha ni nyingi, mvua ni neema lakini wakati mwingine zikizidi pia zinaleta uharibifu mkubwa sana wa miundombinu. Kwa hiyo, kwa ujumla wake, naomba niwaagize Mameneja wa TARURA wa Wilaya zote mbili wakatazame uharibifu ulivyo, halafu waweze kushauri Serikali nini tuweze kufanya katika kusaidia ili wananchi waendelee kupata huduma.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y. MHE. DKT. MARY M. NAGU) aliuliza:- Katika msimu wa mwaka 2015/2016, Wilaya ya Hanang ilikumbwa na mvua kubwa sana iliyosababisha kuharibika kwa miundombinu ikiwemo ya barabara. (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilitengwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo? (b) Je, ni lini Serikali itajenga na kukamilisha barabara iliyofunguliwa na Wachina inayopita katika Vijiji vya Mig’enyi, Milongoli, Gawidu hadi Ngamu na barabara inayounganisha Sechet, Wilaya ya Babati Vijijini kupitia Vijiji vya Basodesh, Basotu mpaka Mulbadaw?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi mvua za mwaka 2017 mwishoni na mwaka huu 2018 zimevuruga sana miundombinu katika Jimbo la Kondoa Mjini. Moja ya barabara iliyoharibika sana ni barabara ya Kingale ambapo mpaka daraja lenye mawasiliano makubwa sana kati ya Kingale na maeneo ya jirani lilivunjika. Daraja hilo limekuja kuangaliwa na watu wa TARURA Mkoa na watu wote wamelichunguza, mpaka sasa hivi bado halijafanyiwa kazi.
Je, ni lini sasa Serikali italeta mpango wa dharura wa kurudisha mawasiliano pale Kingale?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba tumekuwa na mvua nyingi ambazo zimesababisha uharibifu mkubwa kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge anasema katika swali lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika pesa ya dharura ambayo ilikuwa imetengwa kwa ajili ya matengenezo ya dharura, theluthi mbili ya pesa hiyo imetumika katika kurudishia miundombinu katika Mkoa wa Dar es Salaam, kwa sababu uharibifu uliotokea kwa Mkoa wa Dar es Salaam ulikuwa mkubwa sana. Hata hivi leo hii navyoongea almost pesa yote iliyokuwa imetengwa ya dharura imeisha kwa sababu mvua zimenyesha, miundombinu mingi ikawa imeharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Sannda na sababu sasa hivi na mvua nazo hata huko Kondoa hazinyeshi, kabla hatujaanza utekelezaji wa hiyo bajeti ambayo tulipitishiwa na Waheshimiwa na Wabunge, kama Serikali tutaona kuna haja ya kuchukua hatua zozote endapo maeneo hayo hayapitiki, tutafanya hivyo ili wananchi waendelee kupata huduma.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y. MHE. DKT. MARY M. NAGU) aliuliza:- Katika msimu wa mwaka 2015/2016, Wilaya ya Hanang ilikumbwa na mvua kubwa sana iliyosababisha kuharibika kwa miundombinu ikiwemo ya barabara. (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilitengwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo? (b) Je, ni lini Serikali itajenga na kukamilisha barabara iliyofunguliwa na Wachina inayopita katika Vijiji vya Mig’enyi, Milongoli, Gawidu hadi Ngamu na barabara inayounganisha Sechet, Wilaya ya Babati Vijijini kupitia Vijiji vya Basodesh, Basotu mpaka Mulbadaw?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia fursa niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kama alivyosema Naibu Waziri kwamba mvua za mwaka huu na miaka mingine zimekuwa zikileta adha kubwa sana kwa Jiji la Dar es Salaam.
Nataka Serikali ituambie, wana utaratibu gani sasa kuhakikisha kwamba miundombinu hasa ile ya mwendokasi pale walipoweka Makao Makuu pale Jangwani, inahamishwa ili kuhakikisha kwamba wananchi wa Dar es Salaam wanapata usafiri bora, hasa ikizingatiwa kwamba Serikali iliwaondoa watu Jangwani lakini imejenga kituo kikubwa cha mwendokasi; ni lini mtakiondoa kituo kile?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimetangulia kutoa majibu yangu, mvua za safari hii zimekuwa nyingi ukilinganisha na miaka ya nyuma. Katika swali lake anaongelea juu ya suala zima la kuondoa ile stand au tuite garage ya mabasi yaendayo kasi kwa maana ya pale Jangwani, lakini issue siyo kuiondoa bali kuhakikisha kwamba miundombinu ipi inakuwepo ili hata kama mvua zikinyesha pale pasiweze kuathirika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna mpango mahsusi kwa ajili ya Jiji la Dar es Salaam wa kuhakikisha kwamba Bonde la Msimbazi linakuwa na miundombinu ambapo maji ambayo yatakuwa yanatoka kule juu yanaenda baharini kama ambavyo mkondo unaelekeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa avute subira tarehe 20 Julai, kandarasi inafunguliwa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba miundombinu ile inakuwa na ukarabati ambao utakuwa ya uhakika kabisa. (Makofi)