Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. ZAINAB M. BAKAR) aliuliza:- Maji ni muhimu katika maisha ya mwanadamu na bila maji safi na salama afya za wananchi zinaweza kuwa hatarini:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa vijiji ambavyo havina vyanzo vya maji, hasa ikizingatiwa kuwa, bila maji safi na salama ni kuhatarisha afya na maisha ya wananchi hao?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nina maswali mawaili ya nyongeza. Swali la kwanza; katika Manispaa ya Mtwara Mikindani tatizo kubwa ni miundombinu ya usambazaji wa maji, maji yapo, lakini miundombinu ndilo tatizo. Namuuliza Mheshimiwa Waziri ni lini miundombinu ile itaboreshwa, ili kusudi zile kata za pembezoni zipate maji ya uhakika? Maana tumekuwa tukiliongea suala hili siku nyingi sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kumekuwa na kero, watumiaji wa maji katika Manispaa ya Mtwara Mikindani wanalalamika kwamba, wanabambikiwa bill na hiyo inatokana na mamlaka kushindwa kusoma bill katika nyumba zote kutokana na ufinyu wa wafanyakazi. Je, Mheshimiwa Waziri, anatambua kama kuna ufinyu wa wafanyakazi katika mamlaka na kuna jitihada gani za kuhakikisha wanapatikana wafanyakazi wa kutosha? Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimtaarifa Mheshimiwa Mbunge tu kwamba tumesaini mkataba wa shilingi bilioni tano kwenye Mamlaka ya Maji ya Mtwara ambayo katika huo mradi utaongeza vyanzo lakini pamoja na miundombinu ya kusambaza maji katika Mji wa Mtwara na hiyo ni hatua ya kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na usomaji wa bills kwenye nyumba za watu tayari sasa hivi malalamiko yaliyokuwepo baada ya muda mfupi, yatakwisha kwa sababu, sasa tunatumia teknolojia mahususi ambayo kwanza hakutakuwa na mtu kuzidishiwa bill. Ni kwamba, zile mita zitasoma unit baada ya maji kupita sio baada ya hewa kupita, kwa hiyo, suala hilo Mheshimiwa Mbunge tutalimaliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na hayo Mheshimiwa Mbunge Ilani ya Chama cha Mapinduzi tayari itatekeleza mradi mkubwa wa kutoa maji kutoka Mto Ruvuma ambao utaleta maji Mjini Mtwara na baada ya hapo Mji wa Mtwara hautakuwa na tatizo tena la maji, maji yatakuwa mengi, yatahudumia maji ya majumbani pamoja na maji ya viwanda. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira tu, Serikali yake ya Chama cha Mapinduzi inafanyia kazi hili na tayari baada ya muda mfupi utekelezaji wa mradi huo mkubwa utaanza.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. ZAINAB M. BAKAR) aliuliza:- Maji ni muhimu katika maisha ya mwanadamu na bila maji safi na salama afya za wananchi zinaweza kuwa hatarini:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa vijiji ambavyo havina vyanzo vya maji, hasa ikizingatiwa kuwa, bila maji safi na salama ni kuhatarisha afya na maisha ya wananchi hao?

Supplementary Question 2

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Kuna mpango wa kujenga mradi mkubwa wa maji ambao unatakiwa kutekelezwa na SADC katika Mji wa Tunduma pamoja na Mji wa Nakonde upande wa Zambia. Ni nini mkakati na Serikali imefikia wapi katika kujenga mradi huu mpaka sasa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, tayari Serikali ya Chama cha Mapinduzi inatekeleza mradi wa muda mfupi, imechimba visima viwili pale Mjini Tunduma, imeweka pump na juzi nilienda kule kwenda kuangalia. Changamoto ni kwa kisima kimoja ambacho waliweka bomba lenye diameter ndogo, kwa hiyo, maji yakawa hayatoki kwa wingi, lakini na matenki tumeshajenga, tumetoa maelekezo tunaboresha hiyo huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na mradi mkubwa wa Tunduma/Nakonde, tayari consultant ameanza kazi ya kufanya feasibility study. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi tutatekeleza huo mradi kwa ajili ya Tunduma kwa upande wa Tanzania na Nakonde kwa upande wa Zambia na hasa kwa sababu chanzo cha maji kinatoka upande wa Zambia.

Name

Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. ZAINAB M. BAKAR) aliuliza:- Maji ni muhimu katika maisha ya mwanadamu na bila maji safi na salama afya za wananchi zinaweza kuwa hatarini:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa vijiji ambavyo havina vyanzo vya maji, hasa ikizingatiwa kuwa, bila maji safi na salama ni kuhatarisha afya na maisha ya wananchi hao?

Supplementary Question 3

MHE. MAULID S. MTULIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Wakazi wa Jimbo la Kinondoni wanasumbuliwa na ukosefu wa maji hasa kutokana na mtandao wa maji, kwa maana ya mabomba mengi kuharibika au kutokuwa na huo mtandao. Je, Waziri ana mpango gani wa kutuletea mtandao wa maji katika Kata zetu za Tandale, Makumbusho, Kijitonyama, Kigogo, Hananasifu, Magomeni, Mzimuni ili kuhakikisha watu wote wanapata mtandao wa maji? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpe taarifa, wakati tunatekeleza miradi ya kupanua vyanzo vya maji vya Ruvu Juu na Ruvu Chini idadi ya wananchi Dar-es-Salaam ilikuwa milioni tano, leo hii idadi ya wananchi Jiji la Dar-es-Salaam ni milioni sita na laki nne, kwa hiyo, mahitaji ya maji yameongezeka, sio lita milioni 500 tena ni lita milioni zaidi ya 800. Kwa bahati nzuri tumeshachimba visima vya Kimbiji, Mpera, kwa hiyo, hatuna wasiwasi na maji yapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, wiki moja iliyopita, Mheshimiwa Mbunge mwenyewe ni shahidi, tumetangaza tenda kwa ajili ya usambazaji wa maji katika Jiji la Dar-es- Salaam baada ya kupata mkopo wa fedha Dola za Kimarekani milioni hamsini na saba. Kwa hiyo, maeneo yote aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge tunahakikisha kwamba, tunapeleka maji ili wananchi waweze kufaidi Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi, wananchi wote watapata huduma ya maji safi na salama.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. ZAINAB M. BAKAR) aliuliza:- Maji ni muhimu katika maisha ya mwanadamu na bila maji safi na salama afya za wananchi zinaweza kuwa hatarini:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa vijiji ambavyo havina vyanzo vya maji, hasa ikizingatiwa kuwa, bila maji safi na salama ni kuhatarisha afya na maisha ya wananchi hao?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Mradi wa Maji wa Ziwa Viktoria ni mradi mkubwa na ni mradi wa muda mrefu. Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa ambayo wananchi wake wana matatizo makubwa ya maji. Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi wa kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Tabora wanapata maji safi na salama? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimuulize kweli, yupo? Kwa sababu, katika Mkoa wa Tabora tumekamilisha mradi mkubwa kutoka lile bwawa kubwa la pale Tabora, Bwawa la Igombe, ambao sasa hivi unatoa lita milioni 30 kwa siku na mahitaji ya maji kwa Tabora ilikuwa lita milioni 24 na kwa hiyo tulikuwa na excess ya lita milioni sita.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na hayo tunatekeleza mradi mkubwa wa maji ambao tumepata fedha kutoka Serikali ya India. Ndiyo maana tumeamua sasa, kwa sababu maji yatakuwa mengi tutapeleka mpaka Sikonge, tutapeleka mpaka Urambo na tunaweza tukayafikisha mpaka Kaliua. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge sasa hivi tayari kuna mradi mwingine unaendelea pale Tabora kwa sasa, tunasambaza maji kupeleka kwa wananchi, maji yapo, Ilani ya Chama cha Mapinduzi inafanya kazi yake.

Name

Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. ZAINAB M. BAKAR) aliuliza:- Maji ni muhimu katika maisha ya mwanadamu na bila maji safi na salama afya za wananchi zinaweza kuwa hatarini:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa vijiji ambavyo havina vyanzo vya maji, hasa ikizingatiwa kuwa, bila maji safi na salama ni kuhatarisha afya na maisha ya wananchi hao?

Supplementary Question 5

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mji Mdogo wa Kilwa Kivinje kuna vitongoji tisa ambavyo vyote havina maji; na kuna mradi mkubwa wa maji ulikuwa wa kutoka Mavuji kuja Kilwa Kivinje, mpaka sasa hivi hatujajua hatima yake. Je, Waziri anazungumzia vipi upatikanaji wa maji katika Mji Mdogo wa Kilwa Kivinje?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Kivinje naufahamu uko baharini, lakini juzi nilimpa Mheshimiwa Mbunge shilingi milioni 500, tumetoa fidia kwa ajili ya kutunza eneo la chanzo cha maji. Kwa hiyo, chanzo hicho sasa tutatekeleza mradi mmoja mkubwa wa kuchukua maji yaliyo baridi pale na kuyapeleka katika eneo la Kivinje. Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi Ilani ya Chama cha Mapinduzi iko makini, itatekeleza huo mradi kuhakikisha wananchi wa Kivinje wanapata huduma ya maji.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. ZAINAB M. BAKAR) aliuliza:- Maji ni muhimu katika maisha ya mwanadamu na bila maji safi na salama afya za wananchi zinaweza kuwa hatarini:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa vijiji ambavyo havina vyanzo vya maji, hasa ikizingatiwa kuwa, bila maji safi na salama ni kuhatarisha afya na maisha ya wananchi hao?

Supplementary Question 6

MHE. INNOCENT L. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa kuleta maji kwenye Mji wa Lubwera pale Makao Makuu ya Wilaya, lakini maji yale yaliyoletwa hayawatoshelezi wananchi. Naiuliza Serikali,ni lini itapanua ule mradi ili uweze kuwatosheleza wananchi kwa sababu ule mji unapanuka sana? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana kwa jinsi anavyofuatilia matatizo ya maji katika jimbo lake, jimbo ambalo lina vyanzo vingi vya maji, lakini lilikuwa halina maji ambayo yalikuwa yamewafikia wananchi; na jana alikuja ofisini kwangu kuendelea kufuatilia huo mradi wa maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, hapo Lubwela tulichimba visima viwili, lakini mtandao umekuwa mkubwa, maji hayatoshi. Namwongezea kisima kimoja, tutaanza kuchimba mwezi huu pamoja na kujenga tenki, lakini hiyo ni sambamba na kupitia sasa huo mradi mkubwa ambao tayari usanifu wake unakamilika ambao utapeleka maji kwenye vijiji 57 katika jimbo lake.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaambie tu wananchi wa Mheshimiwa Mbunge kwamba, yeye yuko makini, atahakikisha kwamba, wananchi wake wanapata huduma ya maji safi na salama.