Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- (a) Je, Ranchi ya Missenyi ina ng’ombe wangapi kwa sasa? (b) Je, wananchi wanaoizunguka ranchi hiyo wananufaikaje kutokana na uwepo wake?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Ranchi ya Missenyi ni miongoni mwa ranchi za mifano na ina hekta 23,000 na ng’ombe 1,670. Je, Mheshimiwa Waziri anayo mambo mengine anayoweza kunieleza ili na mimi nianze kufikiria kama yeye kuiita Ranchi ya Missenyi ranchi ya mfano huku ikiwa na hekta 23,000 na ng’ombe 1,600? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa swali langu nimeuliza wananchi wanaozunguka Ranchi ya Missenyi wamepata faida zipi, sasa hii kusema mitamba 12 na mbuzi sita inanipa mashaka. Nimsaidie Mheshimiwa Waziri kwamba Kata ya Mabale ipo mbali, eneo tofauti kabisa na Ranchi ya Missenyi, Kata ya Mabale imezunguka Ranchi ya Mabale. Sasa yupo tayari kukubaliana na mimi kwamba waliomasidia kumtafutia majibu wamemdanganya na awawajibishe ili wasimdanganye tena? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimthibitishie kwamba ni kwa nini nimesema Ranchi ya Missenyi ni miongoni mwa ranchi za mfano katika nchi yetu. Nadhani yeye amechukulia kigezo cha idadi ya mifugo na ukubwa wa eneo pekee; lakini nataka nimwambie kwamba tuna sababu nyingine kadha wa kadha za kuifanya Ranchi ya Missenyi kuwa ni ranchi ya mfano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya sababu hizo ni eneo la kijiografia (geographical location) yake Ranchi ya Missenyi yenyewe. Sisi sote tunafahamu kwamba ranchi hii ipo katika mpaka wetu na nchi kadhaa zinazozunguka nchi yetu. Kwa hiyo, sisi kama Taifa na hata ambao waliasisi ranchi hii walikuwa wanajua kwa sababu gani ambapo tumeenda kuiweka ranchi hii. Hii ndiyo maana kutokana na sifa zake kadha wa kadha ambazo ni pamoja na hii ya idadi ya mifugo na geographical location tunasema kwamba Ranchi ya Missenyi ni ranchi ya mfano na tutaendelea kuiboresha ili kuhakikisha kwamba tasnia ya mifugo katika nchi yetu inaendelea kuwa na kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili amelieleza kuhusiana na Mabale kwamba haipo katika Ranchi ya Missenyi ama ipo mbali na Ranchi ya Missenyi na kwamba labda nimedanganywa na waandishi wangu wa majibu. Naomba nichukue maelezo haya ya Mheshimiwa Mbunge, na kama upo uboreshaji sisi tupo tayari kukosolewa maana kukosolewa ndiyo kuimarika pia, ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- (a) Je, Ranchi ya Missenyi ina ng’ombe wangapi kwa sasa? (b) Je, wananchi wanaoizunguka ranchi hiyo wananufaikaje kutokana na uwepo wake?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kama alivyosema Ranchi ya Missenyi ni ya mfano na huo mfano ni kutokuwa na mifugo.
Swali langu la msingi sababu inayosababisha Ranchi ya Missenyi isiwe na mifugo ni kwa sababu zile blocks mmewapa watu ambao siyo wafugaji wa mbali, wao kazi yao ni kukodisha. Je, kwa utaratibu mpya mlionao mtawajali wakazi wa eneo la Misenyi, kwamba ndio wapewe maeneo hayo ya ranchi. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli kwamba palikuwa na kasoro kadha wa kadha ambazo zilisababishwa na kuwapatia watu ambao si wafugaji na matokeo yake wakawa wanakwenda kuwakodisha watu wengine. Hivi sasa baada ya kuingia sisi tumekubaliana kufanya mabadiliko na ndiyo maana tumezirudisha ranchi zile Wizarani kwa ajili ya kuanza kugawa upya na tumeanza kazi hiyo ya kupokea maombi, kuyapitia na kujiridhisha kwamba huyu kweli ni mfugaji na tuweze kumpatia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa faida tu ni kwamba pamoja na kufanya hivyo, tumekubaliana kwamba hatupo tayari kuona ng’ombe yoyote aliyepo katika maeneo yanayozunguka ranchi zetu anakufa kwa sababu ya kukosa malisho na maji, hivyo tumekubaliana ya kwamba wafugaji wanaozunguka pamoja na wafugaji wa Jimbo la Mheshimiwa Dkt. Diodorus Kamala waweze kulipia kwa muda wa miezi mitatu. Ng’ombe mmoja analipia shilingi 10,000 anaingia katika ranchi, anapewa eneo, ananenepeshwa na akimaliza anatoka badala ya ile kuendelea kuwapga faini kwa sababu ya kuingia katika eneo la ranchi. Hivyo, tumekubaliana kurasimisha hatua hizi.