Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Wastani wa juu wa kuzaa kwa mwanamke wa Kigoma ni mara saba juu ya wastani wa kitaifa, lakini wanawake hawa wana hatari ya kupoteza maisha wakiwa wanajifungua kutokana na miundombinu mibovu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha uzazi salama na kutokomeza kabisa vifo vya mama na mtoto?

Supplementary Question 1

MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, naomba kuuliza maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-
(a) Wanawake wengi ndani ya Mkoa wa Kigoma hawana elimu ya kutosha kuhusu uzazi wa mpango na hata wale ambao ni wajawazito bado hawaelewi ni hatua zipi waweze kuziona na wakimbie katika vituo vya afya. Serikali mmejipangaje katika kuwapatia elimu wananchi wa Kigoma?
(b) Wilaya ya Kigoma Vijijini katika Vijiji vya Zashe, Mtanga, Kalalangabo, vijiji hivi vinakabiliwa na ukosefu wa wauguzi; hospitali ina muuguzi mmoja. Nini kauli ya Serikali katika kusaidia vijiji hivi viweze kupata wauguzi wa kutosha kwa haraka? Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi wastani wa taifa wa matumizi ya njia za uzazi salama ni asilimia 38; asilimia 32 kwa njia za kisasa na asilimia sita kwa njia za asili, bado tuko nyuma sana, lengo letu lilikuwa tuifikie asilimia 45. Kwa hiyo, na sisi kama Serikali tumeliona hilo, tunaendelea kuweka afua mbalimbali za kutoa elimu kwa jamii, na mimi niendelee kusisitiza jamii kwamba njia za uzazi bora ni salama na tuachane na imani potofu na zitatusaidia sana kuhakikisha kwamba tunazaa, tunapata watoto kwa idadi na kwa wakati ambao na sisi tunawahitaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusiana na hali ya watumishi. Tunatambua baadhi ya maeneo kumekuwa na changamoto kubwa sana ya watumishi. Katika mwaka huu wa fedha Serikali imetoa vibali vya kuajiri watumishi wa afya 8,000; watumishi 6,200 kati ya hao katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI na 1,800 katika Wizara ya Afya. Kwa hiyo zoezi hili litakapokamilika maeneo ambayo niliyoyataja yatakuwa ni sehemu ambayo yatapata watumishi.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Wastani wa juu wa kuzaa kwa mwanamke wa Kigoma ni mara saba juu ya wastani wa kitaifa, lakini wanawake hawa wana hatari ya kupoteza maisha wakiwa wanajifungua kutokana na miundombinu mibovu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha uzazi salama na kutokomeza kabisa vifo vya mama na mtoto?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kigoma ni mkoa ambao huduma za afya zipo chini sana. Katika mikoa mitano ambayo huduma za afya ziko chini ni pamoja na Mkoa wa Kigoma.
Sasa ningependa kumuuliza Waziri, ni kwa nini Mkoa wa Kigoma haupewi kipaumbele (priority) ikiwa hali ya akina mama na vifo vya watoto ni kubwa sana? Hata ambulance tu kwenye Hospitali ya Wilaya hatuna, naomba commitment ya Wizara.

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza si kweli kwamba Mkoa wa Kigoma haupewi kipaumbele katika utoaji wa huduma za afya. Hata hivyo ni kweli kwamba Mkoa wa Kigoma ni mmojawapo ya mikoa ambayo yaani viashiria vya afya hasa afya ya mama na mtoto ni mbaya, iko duni. Kwa hiyo, Serikali ina mpango tunaita result based finance (lipa malipo kwa ufanisi). Kwa hiyo Mkoa wa Kigoma ni moja ya mikoa nane ambayo tunaipatia fedha mahsusi kila zahanati, kila kituo cha afya, kila hospitali Kigoma tunaipa fedha kwa ajili ya kuhakikisha akina mama na watoto wajawazito wanapata huduma bora. Tanga haipati, Dodoma haipati na Rukwa haipati. Kwa hiyo, utakavyoona Kigoma tunaipendelea, I mean siyo tunaipendelea tunaipa kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumegawa magari ya wagonjwa sita katika Mkoa wa Kigoma, hatukugawa katika mikoa mingine. Kwa hiyo, nachotaka kumuomba Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Nsanzugwanko unafanya kazi nzuri Kasulu endelea kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Serikali kwa ujumla katika kuimarisha huduma za afya ikiwemo afya ya mama na mtoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mengine ni masuala ya uelewa/attitude. Ameongea Naibu Waziri, wanawake kuhudhuria kliniki wanajivuta. Kwa nini wanawake wa Kilimanjaro wengi wanahudhuria kliniki na si wanawake wa Kigoma? Kwa hiyo, tumeona tunakuja na kampeni ya kitaifa tunaita Jiongeze Tuwavushe Salama; ataizindua Mama Samia Suluhu Hassan. Tunataka wanawake wa Kigoma wajiongeze kwenda kliniki kabla ya kuanza kulaumu mambo mengine. Wakijiongeza na sisi Serikali tutajiongeza tutawapa 25,000 kila mama anayejifungulia I mean Kituo cha Afya kitalipwa 25,000 kwa kila mama anayejifungulia katika Kituo cha Afya cha Kigoma. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kukushukuru.
(Makofi)