Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Je, Serikali ina mikakati gani ya kukabiliana na vifo vya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa takwimu zinaonesha ni takribani asilimia 30 tu ya akina mama wajawazito ndio wanaohudhuria kliniki.
Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa akina mama wajawazito ili wahudhurie kliniki na waweze kuepuka matatizo hayo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; umbali kutoka mahali ambapo akina mama wajawazito wanapata huduma ni moja kati ya sababu zinazosababisha matatizo hayo. Kwa mfano, kwenye Jimbo la Ukerewe ambalo linaundwa na visiwa vingi, Visiwa kama Zeru, Kamasi, Bulubi, Gana vyote vile vinatumia zahanati moja.
Sasa kama Serikali ilivyofanya kwa Kituo cha Bwisya, tunashukuru, je, Serikali iko tayari kushirikiana na TAMISEMI, Wizara ya Afya ili ama kituo hiki cha Kamasi kiweze kupandishwa na kupata pesa za kutengeneza miundombinu kuweza kutoa huduma zilizo bora kwa kina mama wajawazito?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa takwimu za hali ya utoaji huduma za afya mwaka 2015 akina mama ambao wanakwenda kliniki angalau mara moja tuko asilimia 90, lakini tunataraji kina mama waende kliniki angalau mara nne katika kipindi chao cha ujauzito, na sasa hivi tuko kwenye zaidi ya asilimia 60 katika kiwango cha kitaifa. Kwa hiyo, rai yangu bado naendelea kutoa kwa wanawake wote wajawazito katika nchi yetu kuhakikisha kwamba wanapokuwa wajawazito angalau kufika katika vituo vyetu vya kutolea (Anti-Natal Clinic) angalau mara nne ili iweze kuwasaidia kupata ushauri na jinsi gani bora ya kuweza kuhudumia ujauzito waliokuwa nao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameongelea suala la umbali. Serikali inatambua hilo na tumekuwa tunaendelea kuboresha huduma za afya na hivi vituo 208 ambavyo tumeviboresha hivi karibuni na kuweza kutoa huduma nzuri za ujauzito na upasuaji pamoja na kujifungulia ni moja ya mkakati wa Serikali. Kuna mkakati wa kuongeza Hospitali za Rufaa za Wilaya, tuna mkakati wa kuongeza Hospitali za Rufaa za Mikoa na kadri tutakapokuwa tunaona mahitaji katika hivyo visiwa vingine vya Ukerewe ambavyo umevisema hatutasita kukaa na wenzetu wa TAMISEMI na kuangalia jinsi gani ya kuboresha huduma katika maeneo hayo husika.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Je, Serikali ina mikakati gani ya kukabiliana na vifo vya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna tatizo kubwa sana la watoto njiti lakini vile vile na watoto wanaozaliwa kwa maumbile. Tofauti hii ni kwa sababu labda wakina mama hawaendi hospitali kwa wakati. Hivi karibuni majuzi majuzi tu hapa kule Kyaka kuna watoto wamezaliwa wameungana.
Sasa nilikuwa naomba kujua kama Serikali ina taarifa hii na kama inayo wanachukua hatua gani ili kuwasaidia waweze kufanyiwa labda matibabu ya haraka ili isije ikatokea kama Ndugu zetu Marehemu Consolata na Maria? Ahsante.

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Susan Lyimo kwa swali lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tayari Serikali kupitia Wizara ya Afya inayo taarifa ya kuzaliwa kwa watoto wapacha ambao wameungana na tayari tumeshatoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Serikali kufanya mawasiliano na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera kuhakikisha watoto wale wanafikishwa Muhimbili haraka iwezekanavyo ili tuweze kufanya taratibu za kuwatenganisha kadri madaktari watakavyoshauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Waziri angejibu swali hili, lakini nimesimama hapa kutoa rai kwa Watanzania wote, pale ambapo anazaliwa mtoto mwenye maumbile angalau labda ni tofauti na ilivyozoeleka, wawalete Hospitali yetu ya Taifa Muhimbili haraka iwezekanavyo ili tuweze sasa kuhakikisha Madaktari wetu Bingwa wanawapa msaada ikiwemo kuwatenganisha.
Kwa hiyo, tunaangalia kama tutawatenganisha ndani ya nchi au tutawapeleka nje ya nchi. Kwa hiyo nimesimama hapa kutoa rai tusiwafiche watoto hawa, tuwapate mapema. Mtoto yeyote ambaye tunamuona yuko na maumbile tofauti wawasiliane na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ili tuhakikishe tunaokoa maisha ya watoto wetu. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Je, Serikali ina mikakati gani ya kukabiliana na vifo vya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati?

Supplementary Question 3

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi, na mimi nina maswali mawili ya nyongeza.
Moja kumbe, haya. (Kicheko)..... Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ziko sababu kadhaa ambazo nyingine hazizuiliki zinazosababisha watoto hawa kuzaliwa mapema, je, Serikali ina utaratibu gani wa kuziimarisha na kuziboresha hizi special care intensive nurseries zilizopo na zipo ngapi katika mikoa yetu?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika swali la msingi huduma kwa mtoto yeyote ambaye anatarajiwa kuzaliwa inaanza katika mahudhurio ya kliniki. Ninaendelea kusisitiza na kutoa rai kwamba wanawake wajawazito na baada ya kubaini wameshapata ujauzito ni muhimu sana kwenda kliniki mara nne, kwa sababu katika mahudhurio haya ya kliniki ndipo hapo ambapo tunaweza tukabaini changamoto kama hizo na uwezekano wa mtoto kuzaliwa akiwa njiti. Sambamba na hilo nimesema kwamba tumetoa elimu kwa watoa huduma wetu wote katika ngazi zote kuhusiana na jinsi gani wanaweza wakawahudumia watoto njiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali sasa hivi katika bajeti ambayo mmetupitishia katika moja ya kipaumbele ambacho tumesema tutaweza kuweka katika hospitali za rufaa za mikoa ni pamoja na huduma za Neonatal ICU. (Makofi)