Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali haioni haja sasa ya kuziagiza rasmi Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwezesha Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) kutekeleza baadhi ya majukumu yake ili walimu wapate huduma stahiki kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri. Kwa kuwa hawa Makatibu Wasaidizi wa Tume wote hawajawahi kuteuliwa na hawatambuliki kisheria.
Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuwateuwa hawa ili waweze kufanya kazi yao ipasavyo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa mashauri mengi ya walimu yamekaa kwa muda mrefu kwa sababu ya ukosefu wa fedha na fedha nyingi haziendi, na leo Serikali imekiri imetenga shilingi bilioni 4.6; Mheshimiwa Waziri anawahakikishiaje viongozi hawa kwamba fedha hizi zitaenda kwa wakati?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama nilivyosema katika swali la kwanza kuhusu uteuzi. Uteuzi huwa ni hatua ya mwisho ya mchakato, na mchakato wenyewe huanza na upekuzi, kumpekua yule mtu unayempendekeza kwenye nafasi fulani. Kwa hiyo mchakato huo uko katika hatua za mwisho.
Napenda kulithibitishia Bunge hili na Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato huo wa upekuzi ambao Idara ambazo zinazofanya upekuzi anazifahamu Mheshimiwa Mbunge zitakapokamilisha upekuzi huo, Makatibu Wasaidizi wote katika Wilaya watateuliwa kwa mujibu wa mapendekezo ya huo upekuzi utakapokamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili naomba nimhakikishie kwamba wakati wa mazungumzo yetu wakati wa bajeti tumehakikishiwa na Waziri wa Fedha kwamba kwa mwaka ujao wa fedha, fedha hizi zitatoka kwa wakati. Ahsante sana.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali haioni haja sasa ya kuziagiza rasmi Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwezesha Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) kutekeleza baadhi ya majukumu yake ili walimu wapate huduma stahiki kwa wakati?

Supplementary Question 2

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri anasema kwamba anaiagiza Tume ya Taifa ya Walimu kutatua changamoto za walimu, lakini Serikali iliwaahidi walimu kuwapatia posho ya kufundishia (teaching allowance)ili iwe motisha kwao lakini hadi sasa Serikali imekuwa na kigugumizi, fedha hizo (teaching allowance) bado hawatoi kwa walimu.
Je, sasa Serikali inataka ituambie mliwadanganya walimu au mna nia ya kutoa teaching allowance iwe kama ni motisha?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niwapongeze Naibu Mawaziri wote kwa majibu mazuri sana ya awali na ufafanuzi na ningependa kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Masoud kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mjuavyo kwamba Serikali kwa kubaini kwamba kuna changamoto nyingi, si kwa walimu pekee isipokuwa kwa watumishi wa kada mbalimbali; kupitia Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma iliunda bodi maalum kwa ajili ya kupitia swala zima la kazi mbalimbali za mazingira magumu. Sehemu nyingine posho nyingine huwa zinaingizwa katika mishahara kwa kadiri itakavyoonekana inafaa.
Kwa hiyo, Serikali imeangali kwa ujumla wake ndiyo maana kwa upande wa walimu, kwanza ilianza baadhi ya kada mbalimbali hasa katika Walimu Wakuu wa Sekondari na Msingi na hali kadhalika kwa Maafisa wale wetu wa Kata wa Elimu (Waratibu wa Elimu) kwa ajili ya kuwapatia responsibility allowance. Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kuangalia nini cha kufanya kwa ajili ya kuboresha si maslahi ya walimu peke yake isipokuwa kwa watumishi wote wa umma kwa kadiri itakavyoona inafaa kwa ajili ya kuboresha maisha yao.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali haioni haja sasa ya kuziagiza rasmi Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwezesha Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) kutekeleza baadhi ya majukumu yake ili walimu wapate huduma stahiki kwa wakati?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, kwa kuwa hivi sasa mashtaka mengi ya walimu yanachukua muda mrefu na kwa kuwa walimu hawa wanalipwa mishahara na kitendo kinachofanya wasitoe mchango wao.
Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kutoa waraka au maelekezo ya mashtaka haya kuchukua muda mfupi ili walimu warudi kwenye masuala yao ya utumishi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna baadhi ya maeneo kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge mashauri yamechukua muda mrefu. Hata hivyo utaratibu mwingine unaosababisha mashauri kuchukua muda mrefu ni kwa sababu kutakuwa na baadhi ya mambo ambayo yanahitajika katika huo mchakato wenyewe wa kusikiliza hayo mashauri. Mimi napenda niungane naye, kwamba tutatoa maelekezo hivi karibuni; kwa mashauri ambayo yako shuleni ambayo hayahitaji gharama kubwa na yako chini ya Mwalimu Mkuu wa shule yaweze kusikilizwa haraka iwezekavyo. Mashauri ambayo yako kwenye halmashauri ya wilaya au katika wilaya kwa Katibu Msaidizi tutatoa maelekezo hivi karibuni ili kusudi kasi yake iweze kuongezeka ya kusikiliza.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali haioni haja sasa ya kuziagiza rasmi Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwezesha Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) kutekeleza baadhi ya majukumu yake ili walimu wapate huduma stahiki kwa wakati?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Mimi nataka kujua kutoka Serikalini ni lini Walimu waliohamishwa kutoka shule za sekondari kwenda shule za msingi watalipwa stahiki zao. Kule Karagwe kuna walimu 131 mpaka hivi sasa wanasubiri stahiki zao. Serikali ilitoa shilingi milioni 52 na hela ambayo inayohitajika ni shilingi milioni 430. Sasa nataka kusikia kutoka Serikalini, walimu hawa mnawaambia nini? Ahsante sana.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipende kusisitiza kauli ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa kuanzia mwezi wa pili kwamba uhamishaji wa watumishi usifanyike hadi pale kunapokuwa na fedha za kuwalipa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo kuna walimu ambao walikuwa tayari wakati huo tamko linatolewa walikuwa wameshahamishwa na ni wengi sio wachache; na kwa sababu walikuwa wameshahamishwa haiwezekani tena kuwarudisha kwenye vituo vyao vya zamani kwa sababu tayari wameshahama na wengine tayari walikuwa wameshapewa baadhi ya fedha na Halmashauri kwa ajili ya kujikimu. Sisi tunawaomba walimu wote wenye stahiki za kulipwa stahili basi waweze kuwa na subira unapoanza mwaka ujao wa fedha kwa bajeti mpya tutahakikisha wamelipwa stahili zao.