Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. ESTER M. MMASI) aliuliza:- Kituo cha Afya Wilaya ya Siha kimeonekana kukidhi mahitaji yote muhimu tayari kwa usajili lakini hadi sasa kituo hicho hakijapata usajili wa Hospitali ya Wilaya. Je, ni nini kauli ya Serikali katika kupandisha hadhi kituo hicho ili kupunguza kadhia ya upatikanaji wa huduma za kiafya kwa wananchi wa Wilaya ya Siha?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hapa swali alilouliza lilikuwa ni kuhusu kupandisha hadhi Kituo cha Afya na amesema wana mpango wa kujenga Hospitali ya Wilaya ambayo wanazidi kuiboresha, je, ni lini sasa kituo hiki ambacho Mheshimiwa amekitaja kitapewa uwezeshaji kama ambavyo tumeona katika vituo mbalimbali nchini ili na chenyewe sasa kiweze kujitosheleza?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa katika Jimbo la Mlalo Halmashauri ya Lushoto, Zahanati ya Malindi na Zahanati ya Manolo zina miundombinu inayotosheleza kuwa na hadhi ya Vituo vya Afya na ukizingatia kwamba hizi ziko katika Tarafa ya Mtae ambayo haina hata kituo kimoja cha afya. Je, lini sasa Serikali itahakikisha inatusaidia katika ule mpango wa shilingi milioni mia nne mia tano ili Tarafa hii iweze kupata kituo cha afya chenye uhakika.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la msingi linauliza likiwa linataka suala zima la Hospitali ya Wilaya na katika majibu ambayo nimeyatoa nimeeleza jitihada ambazo zinafanywa na Serikali katika kujenga Hospitali ya Wilaya ndiyo maana kimetengwa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 ili ujenzi wa hospitali hiyo ambayo eneo tayari limeshatengwa ekari 40 ianze kujengwa. Sasa katika swali lake la msingi anataka hicho kituo cha afya ambacho kina hadhi ya kituo cha afya, labda Mheshimiwa Mbunge anadhani kwamba hakijakamilika. Kituo cha Afya kimekamilika na ndiyo maana kimekuwa kikitumika kama Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la msingi la pili, kuhusiana na Jimboni kwake ambalo angependa zahanati ambazo ziko na zinafanya kazi zipandishwe hadhi zifanane na vituo vya afya au kuanza ujenzi wa vituo vya afya. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni adhma ya Serikali kuhakikisha kwamba zahanati zinaendelea kuwepo lakini pia haiondoi haja ya kuwepo vituo vya afya. Wakati wowote ambapo pesa itapatikana hatutaacha kutizama maeneo ya kwake na ninaamini tutapata fursa pia kutembelea eneo la kwake.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. ESTER M. MMASI) aliuliza:- Kituo cha Afya Wilaya ya Siha kimeonekana kukidhi mahitaji yote muhimu tayari kwa usajili lakini hadi sasa kituo hicho hakijapata usajili wa Hospitali ya Wilaya. Je, ni nini kauli ya Serikali katika kupandisha hadhi kituo hicho ili kupunguza kadhia ya upatikanaji wa huduma za kiafya kwa wananchi wa Wilaya ya Siha?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Tabora Manispaa haina Hospitali ya Wilaya, je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kukosekana kwa Hospitali ya Wilaya na hata kwenye bajeti hii haikuwekewa, je, nini kauli ya Serikali?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, utakabaliana na mimi kwamba swali hili linaulizwa kwa mara ya tatu kama si mara ya nne, kuhusiana na suala zima la uwepo wa Hospitali ya Mkoa wa Tabora ili Hospitali ya Mkoa ya Kitete iweze kupata pahali pa kupumulia. Kama ambavyo imekuwa nikijibu ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba ili Hospitali ya Wilaya ambayo imeshaanza kujengwa, iendelee kujengwa. Ni suala tu la kibajeti, hali ikiruhusu hatuwezi kuacha kujenga Hospitali ya Wilaya ndani ya Manispaa ya Tabora ili Hospitali ya Kitete iweze kupumua.