Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Papa aina ya potwe (whale shark) ni samaki ambaye duniani kote anapatikana Australia na Tanzania katika Kisiwa cha Mafia tu:- Je, ni lini Serikali itakuja na mpango mkakati wa kumtangaza samaki huyo pamoja na vivutio vingine vya utalii kama vile scuba diving na sport fishing duniani ili kuvutia watalii nchini?

Supplementary Question 1

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, moja ya matishio ya samaki aina hii ni anapoingia katika mitego ya wavuvi huwa anajeruhiwa kwa sababu wao wanakuwa hawamli lakini anapata majeraha katika kumnasua kwenye zile nyavu. Matokeo yake kwa kuwa ngozi yake iko very delicate, akipata michubuko anakufa. Sasa kwa kuwa samaki huyu ni wa season anapatikana kuanzia miezi ya mwanzo ya Septemba mpaka Machi, je, Serikali haioni sasa ipo haja ya kutengeneza quota system ambapo msimu wa potwe maeneo ya Kilindoni anapopatikana papigwe marufuku ya kuvua samaki wengine ili kumnusuru samaki huyu kwa sababu huenda akaondoka Mafia? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, utalii katika Kisiwa cha Mafia una gharama kubwa sana. Kila mtalii anayeingia eneo la hifadhi ya bahari analazimika kulipa dola 24 kwa siku moja. Kutokana na ughali huu, inalazimisha baadhi ya watalii kuanza kushindwa kuja Mafia. Je, Serikali sasa ina mpango gani kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupunguza kiwango hiki cha entrance fees za kuingia maeneo ya marine park ili kuweza kuvutia watalii wengi kuja Kisiwani Mafia? Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya kaka yangu Mheshimiwa Mbaraka Kitwana Dau kama ifuatavyo;
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri wa Utalii Mheshimiwa Hasunga kwa majibu mazuri ya msingi hasa pale aliposema anaitaka jamii iweze kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa samaki hawa au papa huyu anayeitwa papa potwe ama pia ninachukua pongezi nyingi sana kwa kaka yangu Dau kwa kuwa mshirika mzuri wa kulinda rasilimali zetu za Taifa ambazo zimekuwa ni kivutio kikubwa cha watalii katika visiwa vyetu hivi vya Mafia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala alilolisema la kuweka utaratibu maalum Wizara yetu tunalichukua ili kusudi sasa tuwe na wakati wa uvuvi katika eneo la Kilindoni na kuna wakati ambapo tutazuia ili kuwapisha papa potwe waweze kustawi. Bila ya kufanya hivyo, papa potwe watahama Mafia na tutasababisha utalii wa papa potwe uweze kutoweka katika eneo hili la Mafia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili juu ya tozo mbalimbali ambzo zinachukuliwa na Wizara yetu kupitia kitengo chetu cha MPRU kwa maana ya hifadhi ya bahari na zile zinazokwenda Wizara ya Utalii, mimi naomba nimhakikishie kwamba sisi Wizara yetu ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Maliasili na Utalii tutakaa kwa pamoja na kufanya review ya hizi tozo na kodi hizi zinazohusika katiak utalii huu ili kusudi tuweze kuhakikisha kwamba watalii waweze kuvutika kwa wengi zaidi. (Makofi)

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Papa aina ya potwe (whale shark) ni samaki ambaye duniani kote anapatikana Australia na Tanzania katika Kisiwa cha Mafia tu:- Je, ni lini Serikali itakuja na mpango mkakati wa kumtangaza samaki huyo pamoja na vivutio vingine vya utalii kama vile scuba diving na sport fishing duniani ili kuvutia watalii nchini?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF HUSSEIN SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kidogo nimeguswa hapa. Huyu papa ni papa mmoja na hadhuru mwanadamu na mara nyingi kwa kule kwetu sisi huwa mwezi Desemba wanatoka Somalia wanakuja zao mpaka wanakuja kupiga kambi Minai – Zanzibar wanakuwa kwa wingi sana na huyu papa huwa anawafuata wale dolphins. Mara nyingi huwa anawafuata wale dolphins, swali langu kwa Mheshimiwa Waziri, kipindi cha Desemba mpaka Februari wanakuja na kurudi ni kipindi ambacho tunaweza tukafanya utalii mkubwa sana katika eneo letu la kuanzia mpakani na Kenya Duga mpaka Zanzibar. Je, Wizara yako imejipangaje sasa kutumia fursa hii ambayo wale dolphins na huyu papa wanatangaza nchi yetu wenyewe, sisi tutumie tu hiyo fursa. Lini tutatumia hiyo fursa ya kujenga hoteli katika ukanda huo. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba katika kipindi hiki hawa potwe wanakuwa wengi sana katika maeneo haya au wanakuja katika maeneo haya. Pia kuna vivutio vingi sana ambavyo vipo katika ukanda wa bahari yetu hasa katika fukwe zetu hizi za bahari ambazo tunaweza tukafanya na ndiyo maana Serikali sasa hivi iko mbioni katika kuhakikisha kwamba tunaanzisha mamlaka ya kusimamia fukwe zote za bahari kusudi tuweze kufaidika na huu utalii wa baharini ambao tulikuwa hatujautumia kwa muda mrefu sana. Kwa hiyo, naamini katika hizi jitihada, pale ambapo zitakuwa zimekamilika na sheria itakapokuwa imeletwa hapa Bungeni basi hizi jitihada zitakuwa zimekwenda sambamba na hilo wazo la Mheshimiwa Mbunge. Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)